1
Basi, ndugu zangu, nawaarifu ile injili niliyowahubiri; ambayo ndiyo mliyoipokea, na katika hiyo mnasimama,
Now, brothers, I want to remind you of the gospel I preached to you, which you received, and in which you stand firm.
2
na kwa hiyo mnaokolewa; ikiwa mnayashika sana maneno niliyowahubiri isipokuwa mliamini bure.
By this gospel you are saved, if you hold firmly to the word I preached to you. Otherwise, you have believed in vain.
3
Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko;
For what I received I passed on to you as of first importance: that Christ died for our sins according to the Scriptures,
4
na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;
that He was buried, that He was raised on the third day according to the Scriptures,
5
na ya kuwa alimtokea Kefa; tena na wale Thenashara;
and that He appeared to Cephas and then to the Twelve.
6
baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;
After that, He appeared to more than five hundred brothers at once, most of whom are still living, though some have fallen asleep.
7
baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;
Then He appeared to James, then to all the apostles.
8
na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake.
And last of all He appeared to me also, as to one of untimely birth.
9
Maana mimi ni mdogo katika mitume, nisiyestahili kuitwa mitume, kwa sababu naliliudhi Kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles and am unworthy to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
10
Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.
But by the grace of God I am what I am, and His grace to me was not in vain. No, I worked harder than all of them—yet not I, but the grace of God that was with me.
11
Basi, kama ni mimi, kama ni wale, ndivyo tuhubirivyo, na ndivyo mlivyoamini.
Whether, then, it was I or they, this is what we preach, and this is what you believed.
12
Basi, ikiwa Kristo anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu, mbona baadhi yenu husema kwamba hakuna kiyama ya wafu?
But if it is preached that Christ has been raised from the dead, how can some of you say that there is no resurrection of the dead?
13
Lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka;
If there is no resurrection of the dead, then not even Christ has been raised.
14
tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.
And if Christ has not been raised, our preaching is worthless, and so is your faith.
15
Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
In that case, we are also exposed as false witnesses about God. For we have testified about God that He raised Christ from the dead, but He did not raise Him if in fact the dead are not raised.
16
Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.
For if the dead are not raised, then not even Christ has been raised.
17
Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.
And if Christ has not been raised, your faith is futile; you are still in your sins.
18
Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.
Then those also who have fallen asleep in Christ have perished.
19
Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.
If our hope in Christ is for this life alone, we are to be pitied more than all men.
20
Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.
But Christ has indeed been raised from the dead, the firstfruits of those who have fallen asleep.
21
Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu.
For since death came through a man, the resurrection of the dead comes also through a man.
22
Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.
For as in Adam all die, so in Christ all will be made alive.
23
Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja.
But each in his own turn: Christ the firstfruits; then at His coming, those who belong to Him.
24
Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
Then the end will come, when He hands over the kingdom to God the Father after He has destroyed all dominion, authority, and power.
25
Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
For He must reign until He has put all His enemies under His feet.
26
Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
The last enemy to be destroyed is death.
27
Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo.
For “God has put everything under His feet.” Now when it says that everything has been put under Him, this clearly does not include the One who put everything under Him.
28
Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.
And when all things have been subjected to Him, then the Son Himself will be made subject to Him who put all things under Him, so that God may be all in all.
29
Au je! Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu watafanyaje? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?
If these things are not so, what will those do who are baptized for the dead? If the dead are not raised at all, why are people baptized for them?
30
Na sisi, kwa nini tumo hatarini kila saa?
And why do we endanger ourselves every hour?
31
Naam, ndugu, kwa huku kujisifu kwangu niliko nako juu yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu, ninakufa kila siku.
I face death every day, brothers, as surely as I boast about you in Christ Jesus our Lord.
32
Ikiwa, kwa jinsi ya kibinadamu, nalipigana na hayawani wakali kule Efeso, nina faida gani? Wasipofufuliwa wafu, na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.
If I fought wild beasts in Ephesus for human motives, what did I gain? If the dead are not raised, “Let us eat and drink, for tomorrow we die.”
33
Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
Do not be deceived: “Bad company corrupts good character.”
34
Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.
Sober up as you ought, and stop sinning; for some of you are ignorant of God. I say this to your shame.
35
Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
But someone will ask, “How are the dead raised? With what kind of body will they come?”
36
Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;
You fool! What you sow does not come to life unless it dies.
37
nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;
And what you sow is not the body that will be, but just a seed, perhaps of wheat or something else.
38
lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake.
But God gives it a body as He has designed, and to each kind of seed He gives its own body.
39
Nyama yote si nyama moja; ila nyingine ni ya wanadamu, nyingine ya hayawani, nyingine ya ndege, nyingine ya samaki.
Not all flesh is the same: Men have one kind of flesh, animals have another, birds another, and fish another.
40
Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali.
There are also heavenly bodies and earthly bodies. But the splendor of the heavenly bodies is of one degree, and the splendor of the earthly bodies is of another.
41
Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota.
The sun has one degree of splendor, the moon another, and the stars another; and star differs from star in splendor.
42
Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika;
So will it be with the resurrection of the dead: What is sown is perishable; it is raised imperishable.
43
hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu;
It is sown in dishonor; it is raised in glory. It is sown in weakness; it is raised in power.
44
hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko.
It is sown a natural body; it is raised a spiritual body. If there is a natural body, there is also a spiritual body.
45
Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.
So it is written: “The first man Adam became a living being”; the last Adam a life-giving spirit.
46
Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho.
The spiritual, however, was not first, but the natural, and then the spiritual.
47
Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni.
The first man was of the dust of the earth, the second man from heaven.
48
Kama alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na kama alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni.
As was the earthly man, so also are those who are of the earth; and as is the heavenly man, so also are those who are of heaven.
49
Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni.
And just as we have borne the likeness of the earthly man, so also shall we bear the likeness of the heavenly man.
50
Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika.
Now I declare to you, brothers, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God, nor does the perishable inherit the imperishable.
51
Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,
Listen, I tell you a mystery: We will not all sleep, but we will all be changed—
52
kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.
in an instant, in the twinkling of an eye, at the last trumpet. For the trumpet will sound, the dead will be raised imperishable, and we will be changed.
53
Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.
For the perishable must be clothed with the imperishable, and the mortal with immortality.
54
Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda.
When the perishable has been clothed with the imperishable and the mortal with immortality, then the saying that is written will come to pass: “Death has been swallowed up in victory.”
55
Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?
“Where, O Death, is your victory? Where, O Death, is your sting?”
56
Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati.
The sting of death is sin, and the power of sin is the law.
57
Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
But thanks be to God, who gives us the victory through our Lord Jesus Christ!
58
Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.
Therefore, my beloved brothers, be steadfast and immovable. Always excel in the work of the Lord, because you know that your labor in the Lord is not in vain.