1 Wakorintho 6 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Wakorintho 6 (Swahili) 1st Corinthians 6 (English)

Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? 1 Wakorintho 6:1

Dare any of you, having a matter against his neighbor, go to law before the unrighteous, and not before the saints?

Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 1 Wakorintho 6:2

Don't you know that the saints will judge the world? And if the world is judged by you, are you unworthy to judge the smallest matters?

Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? 1 Wakorintho 6:3

Don't you know that we will judge angels? How much more, things that pertain to this life?

Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa? 1 Wakorintho 6:4

If then, you have to judge things pertaining to this life, do you set them to judge who are of no account in the assembly?

Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake? 1 Wakorintho 6:5

I say this to move you to shame. Isn't there even one wise man among you who would be able to decide between his brothers?

Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao wasioamini. 1 Wakorintho 6:6

But brother goes to law with brother, and that before unbelievers!

Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang'anywa mali zenu? 1 Wakorintho 6:7

Therefore it is already altogether a defect in you, that you have lawsuits one with another. Why not rather be wronged? Why not rather be defrauded?

Bali kinyume cha hayo ninyi wenyewe mwadhulumu watu na kunyang'anya mali zao; naam, hata za ndugu zenu. 1 Wakorintho 6:8

No, but you yourselves do wrong, and defraud, and that against your brothers.

Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, 1 Wakorintho 6:9

Or don't you know that the unrighteous will not inherit the Kingdom of God? Don't be deceived. Neither the sexually immoral, nor idolaters, nor adulterers, nor male prostitutes, nor homosexuals,

wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi. 1 Wakorintho 6:10

nor thieves, nor covetous, nor drunkards, nor slanderers, nor extortioners, will inherit the Kingdom of God.

Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu. 1 Wakorintho 6:11

Such were some of you, but you were washed. But you were sanctified. But you were justified in the name of the Lord Jesus, and in the Spirit of our God.

Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote vifaavyo; vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu cho chote. 1 Wakorintho 6:12

"All things are lawful for me," but not all things are expedient. "All things are lawful for me," but I will not be brought under the power of anything.

Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. 1 Wakorintho 6:13

"Foods for the belly, and the belly for foods," but God will bring to nothing both it and them. But the body is not for sexual immorality, but for the Lord; and the Lord for the body.

Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake. 1 Wakorintho 6:14

Now God raised up the Lord, and will also raise us up by his power.

Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha! 1 Wakorintho 6:15

Don't you know that your bodies are members of Christ? Shall I then take the members of Christ, and make them members of a prostitute? May it never be!

Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja. 1 Wakorintho 6:16

Or don't you know that he who is joined to a prostitute is one body? For, "The two," says he, "will become one flesh."

Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye. 1 Wakorintho 6:17

But he who is joined to the Lord is one spirit.

Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. 1 Wakorintho 6:18

Flee sexual immorality! "Every sin that a man does is outside the body," but he who commits sexual immorality sins against his own body.

Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 1 Wakorintho 6:19

Or don't you know that your body is a temple of the Holy Spirit which is in you, which you have from God? You are not your own,

maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu. 1 Wakorintho 6:20

for you were bought with a price. Therefore glorify God in your body and in your spirit, which are God's.