1 Wakorintho 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Wakorintho 3 (Swahili) 1st Corinthians 3 (English)

Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. 1 Wakorintho 3:1

Brothers, I couldn't speak to you as to spiritual, but as to fleshly, as to babies in Christ.

Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, 1 Wakorintho 3:2

I fed you with milk, not with meat; for you weren't yet ready. Indeed, not even now are you ready,

kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? 1 Wakorintho 3:3

for you are still fleshly. For insofar as there is jealousy, strife, and factions among you, aren't you fleshly, and don't you walk in the ways of men?

Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu? 1 Wakorintho 3:4

For when one says, "I follow Paul," and another, "I follow Apollos," aren't you fleshly?

Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa. 1 Wakorintho 3:5

Who then is Apollos, and who is Paul, but servants through whom you believed; and each as the Lord gave to him?

Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. 1 Wakorintho 3:6

I planted. Apollos watered. But God gave the increase.

Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. 1 Wakorintho 3:7

So then neither he who plants is anything, nor he who waters, but God who gives the increase.

Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. 1 Wakorintho 3:8

Now he who plants and he who waters are the same, but each will receive his own reward according to his own labor.

Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu. 1 Wakorintho 3:9

For we are God's fellow workers. You are God's farming, God's building.

Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. 1 Wakorintho 3:10

According to the grace of God which was given to me, as a wise master builder I laid a foundation, and another builds on it. But let each man be careful how he builds on it.

Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. 1 Wakorintho 3:11

For no one can lay any other foundation than that which has been laid, which is Jesus Christ.

Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. 1 Wakorintho 3:12

But if anyone builds on the foundation with gold, silver, costly stones, wood, hay, or stubble;

Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. 1 Wakorintho 3:13

each man's work will be revealed. For the Day will declare it, because it is revealed in fire; and the fire itself will test what sort of work each man's work is.

Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. 1 Wakorintho 3:14

If any man's work remains which he built on it, he will receive a reward.

Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto. 1 Wakorintho 3:15

If any man's work is burned, he will suffer loss, but he himself will be saved, but as through fire.

Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 1 Wakorintho 3:16

Don't you know that you are a temple of God, and that God's Spirit lives in you?

Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi. 1 Wakorintho 3:17

If anyone destroys the temple of God, God will destroy him; for God's temple is holy, which you are.

Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima. 1 Wakorintho 3:18

Let no one deceive himself. If anyone thinks that he is wise among you in this world, let him become a fool, that he may become wise.

Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao. 1 Wakorintho 3:19

For the wisdom of this world is foolishness with God. For it is written, "He has taken the wise in their craftiness."

Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili. 1 Wakorintho 3:20

And again, "The Lord knows the reasoning of the wise, that it is worthless."

Basi, mtu ye yote na asijisifie wanadamu. Kwa maana vyote ni vyenu; 1 Wakorintho 3:21

Therefore let no one boast in men. For all things are yours,

kwamba ni Paulo, au Apolo, au Kefa; au dunia, au uzima, au mauti; au vile vilivyopo sasa, au vile vitakavyokuwapo; vyote ni vyenu; 1 Wakorintho 3:22

whether Paul, or Apollos, or Cephas, or the world, or life, or death, or things present, or things to come. All are yours,

nanyi ni wa Kristo, na Kristo ni wa Mungu. 1 Wakorintho 3:23

and you are Christ's, and Christ is God's.