1 Wakorintho 16 Swahili & English
Listen/Download Audio1 Wakorintho 16 (Swahili) | 1st Corinthians 16 (English) |
---|---|
Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi fanyeni vivyo. 1 Wakorintho 16:1 |
Now concerning the collection for the saints, as I commanded the assemblies of Galatia, you do likewise. |
Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja; 1 Wakorintho 16:2 |
On the first day of the week, let each one of you save, as he may prosper, that no collections be made when I come. |
nami nitakapofika nitawatuma kwa nyaraka wale mtakaowachagua, wachukue hisani yenu mpaka Yerusalemu. 1 Wakorintho 16:3 |
When I arrive, I will send whoever you approve with letters to carry your gracious gift to Jerusalem. |
Na kama ikifaa niende na mimi, watasafiri pamoja nami. 1 Wakorintho 16:4 |
If it is appropriate for me to go also, they will go with me. |
Lakini nitakuja kwenu, nikiisha kupita kati ya Makedonia; maana napita kati ya Makedonia. 1 Wakorintho 16:5 |
But I will come to you when I have passed through Macedonia, for I am passing through Macedonia. |
Labda nitakaa kwenu; naam, labda wakati wote wa baridi, mpate kunisafirisha ko kote nitakakokwenda. 1 Wakorintho 16:6 |
But with you it may be that I will stay, or even winter, that you may send me on my journey wherever I go. |
Maana sipendi kuonana nanyi sasa, katika kupita tu, kwa sababu nataraji kukaa kwenu muda kidogo, Bwana akinijalia. 1 Wakorintho 16:7 |
For I do not wish to see you now in passing, but I hope to stay a while with you, if the Lord permits. |
Lakini nitakaa Efeso hata Pentekoste; 1 Wakorintho 16:8 |
But I will stay at Ephesus until Pentecost, |
kwa maana nimefunguliwa mlango mkubwa wa kufaa sana, na wako wengi wanipingao. 1 Wakorintho 16:9 |
for a great and effective door has opened to me, and there are many adversaries. |
Lakini, Timotheo akija, angalieni akae kwenu pasipo hofu; maana anaifanya kazi ya Bwana vile vile kama mimi mwenyewe; 1 Wakorintho 16:10 |
Now if Timothy comes, see that he is with you without fear, for he does the work of the Lord, as I also do. |
basi mtu ye yote asimdharau, lakini msafirisheni kwa amani, ili aje kwangu; maana ninamtazamia pamoja na ndugu zetu. 1 Wakorintho 16:11 |
Therefore let no one despise him. But set him forward on his journey in peace, that he may come to me; for I expect him with the brothers. |
Lakini kwa habari za Apolo, ndugu yetu, nalimsihi sana aende kwenu pamoja na hao ndugu; ambaye si mapenzi yake kwenda sasa; lakini atakuja atakapopata nafasi. 1 Wakorintho 16:12 |
Now concerning Apollos, the brother, I strongly urged him to come to you with the brothers; and it was not at all his desire to come now; but he will come when he has an opportunity. |
Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari. 1 Wakorintho 16:13 |
Watch! Stand firm in the faith! Be courageous! Be strong! |
Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo. 1 Wakorintho 16:14 |
Let all that you do be done in love. |
Tena ndugu, nawasihi; (mnawajua watu wa nyumbani mwa Stefana kwamba ni malimbuko ya Akaya, nao wamejitia katika kazi ya kuwahudumu watakatifu); 1 Wakorintho 16:15 |
Now I beg you, brothers (you know the house of Stephanas, that it is the first fruits of Achaia, and that they have set themselves to minister to the saints), |
watiini watu kama hawa, na kila mtu afanyaye kazi pamoja nao, na kujitaabisha. 1 Wakorintho 16:16 |
that you also be in subjection to such, and to everyone who helps in the work and labors. |
Nami nafurahi kwa sababu ya kuja kwao Stefana na Fortunato na Akaiko; maana hawa wamenikirimia kwa wingi yale niliyopungukiwa kwenu. 1 Wakorintho 16:17 |
I rejoice at the coming of Stephanas, Fortunatus, and Achaicus; for that which was lacking on your part, they supplied. |
Maana wameniburudisha roho yangu, na roho zenu pia; basi wajueni sana watu kama hao. 1 Wakorintho 16:18 |
For they refreshed my spirit and yours. Therefore acknowledge those who are like that. |
Makanisa ya Asia wawasalimu. Akila na Priska wawasalimu sana katika Bwana, pamoja na kanisa lililoko ndani ya nyumba yao. 1 Wakorintho 16:19 |
The assemblies of Asia greet you. Aquila and Priscilla greet you much in the Lord, together with the assembly that is in their house. |
Ndugu wote wawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu. 1 Wakorintho 16:20 |
All the brothers greet you. Greet one another with a holy kiss. |
Hii ni salamu yangu Paulo kwa mkono wangu mwenyewe. 1 Wakorintho 16:21 |
This greeting is by me, Paul, with my own hand. |
Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha. 1 Wakorintho 16:22 |
If any man doesn't love the Lord Jesus Christ, let him be accursed{Greek: anathema.}. Come, Lord!{Aramaic: Maranatha!} |
Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi. 1 Wakorintho 16:23 |
The grace of the Lord Jesus Christ be with you. |
Pendo langu na liwe pamoja nanyi nyote katika Kristo Yesu. 1 Wakorintho 16:24 |
My love to all of you in Christ Jesus. Amen. |