Warumi 16 Swahili & English
Listen/Download AudioWarumi 16 (Swahili) | Romans 16 (English) |
---|---|
Namkabidhi kwenu Fibi, ndugu yetu, aliye mhudumu wa kanisa lililoko Kenkrea; Warumi 16:1 |
I commend to you Phoebe, our sister, who is a servant{literally, deacon} of the assembly that is at Cenchreae, |
kwamba mmpokee katika Bwana, kama iwapasavyo watakatifu; mkamsaidie katika neno lo lote atakalohitaji kwenu; kwa sababu yeye naye amekuwa msaidizi wa watu wengi, akanisaidia mimi pia. Warumi 16:2 |
that you receive her in the Lord, in a way worthy of the saints, and that you assist her in whatever matter she may need from you, for she herself also has been a helper of many, and of my own self. |
Nisalimieni Priska na Akila, watenda kazi pamoja nami katika Kristo Yesu; Warumi 16:3 |
Greet Prisca and Aquila, my fellow workers in Christ Jesus, |
waliokuwa tayari hata kukatwa kichwa kwa ajili ya maisha yangu; ambao ninawashukuru, wala si mimi tu, ila na makanisa ya Mataifa yote pia; nisalimieni na kanisa lililomo katika nyumba yao. Warumi 16:4 |
who for my life, laid down their own necks; to whom not only I give thanks, but also all the assemblies of the Gentiles. |
Nisalimieni Epaineto, mpenzi wangu, aliye malimbuko ya Asia kwa Kristo. Warumi 16:5 |
Greet the assembly that is in their house. Greet Epaenetus, my beloved, who is the first fruits of Achaia to Christ. |
Nisalimieni Mariamu, aliyejitaabisha sana kwa ajili yenu. Warumi 16:6 |
Greet Mary, who labored much for us. |
Nisalimieni Androniko na Yunia, jamaa zangu, waliofungwa pamoja nami, ambao ni maarufu miongoni mwa mitume; nao walikuwa katika Kristo kabla yangu. Warumi 16:7 |
Greet Andronicus and Junias, my relatives and my fellow prisoners, who are notable among the apostles, who also were in Christ before me. |
Nisalimieni Ampliato, mpenzi wangu katika Bwana. Warumi 16:8 |
Greet Amplias, my beloved in the Lord. |
Nisalimieni Urbano, mtenda kazi pamoja nami katika Kristo, na Stakisi, mpenzi wangu. Warumi 16:9 |
Greet Urbanus, our fellow worker in Christ, and Stachys, my beloved. |
Nisalimieni Apele, mwenye kukubaliwa katika Kristo. Nisalimieni watu wa nyumbani mwa Aristobulo. Warumi 16:10 |
Greet Apelles, the approved in Christ. Greet those who are of the household of Aristobulus. |
Nisalimieni Herodioni, jamaa yangu. Nisalimieni watu wa nyumbani mwa Narkiso, walio katika Bwana. Warumi 16:11 |
Greet Herodion, my kinsman. Greet them of the household of Narcissus, who are in the Lord. |
Nisalimieni Trifaina na Trifosa, wenye bidii katika Bwana. Nisalimieni Persisi, mpenzi aliyejitahidi sana katika Bwana. Warumi 16:12 |
Greet Tryphaena and Tryphosa, who labor in the Lord. Greet Persis, the beloved, who labored much in the Lord. |
Nisalimieni Rufo, mteule katika Bwana, na mamaye, aliye mama yangu pia. Warumi 16:13 |
Greet Rufus, the chosen in the Lord, and his mother and mine. |
Nisalimieni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma, na ndugu walio pamoja nao. Warumi 16:14 |
Greet Asyncritus, Phlegon, Hermes, Patrobas, Hermas, and the brothers{The word for "brothers" here and where context allows may also be correctly translated "brothers and sisters" or "siblings."} who are with them. |
Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa, na watakatifu wote walio pamoja nao. Warumi 16:15 |
Greet Philologus and Julia, Nereus and his sister, and Olympas, and all the saints who are with them. |
Salimianeni kwa busu takatifu. Makanisa yote ya Kristo yawasalimu. Warumi 16:16 |
Greet one another with a holy kiss. The assemblies of Christ greet you. |
Ndugu zangu, nawasihi, waangalieni wale wafanyao fitina na mambo ya kukwaza kinyume cha mafundisho mliyojifunza; mkajiepushe nao. Warumi 16:17 |
Now I beg you, brothers, look out for those who are causing the divisions and occasions of stumbling, contrary to the doctrine which you learned, and turn away from them. |
Kwa sababu walio hivyo hawamtumikii Bwana wetu Kristo, bali matumbo yao wenyewe; na kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu. Warumi 16:18 |
For those who are such don't serve our Lord, Jesus Christ, but their own belly; and by their smooth and flattering speech, they deceive the hearts of the innocent. |
Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. Warumi 16:19 |
For your obedience has become known to all. I rejoice therefore over you. But I desire to have you wise in that which is good, but innocent in that which is evil. |
Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.] Warumi 16:20 |
And the God of peace will quickly crush Satan under your feet. The grace of our Lord Jesus Christ be with you. |
Timotheo, mtenda kazi pamoja nami, awasalimu, na Lukio, na Yasoni, na Sosipatro, jamaa zangu. Warumi 16:21 |
Timothy, my fellow worker, greets you, as do Lucius, Jason, and Sosipater, my relatives. |
Mimi Tertio, niliyeandika waraka huu, nawasalimu katika Bwana. Warumi 16:22 |
I, Tertius, who write the letter, greet you in the Lord. |
Gayo, mwenyeji wangu na wa Kanisa lote pia awasalimu. Erasto, wakili wa mji, awasalimu, na Kwarto, ndugu yetu. Warumi 16:23 |
Gaius, my host and host of the whole assembly, greets you. Erastus, the treasurer of the city, greets you, as does Quartus, the brother. |
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.] Warumi 16:24 |
The grace of our Lord Jesus Christ be with you all! Amen. |
Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyositirika tangu zamani za milele, Warumi 16:25 |
{See Romans 14:23} |
ikadhihirishwa wakati huu kwa maandiko ya manabii, ikajulikana na mataifa yote kama alivyoamuru Mungu wa milele, ili waitii Imani. Warumi 16:26 |
{See Romans 14:23} |
Ndiye Mungu mwenye hekima peke yake. Utukufu una yeye kwa Yesu Kristo, milele na milele. Amina. Warumi 16:27 |
{See Romans 14:23} {TR places Romans 14:24-26 at the end of Romans instead of at the end of chapter 14, and numbers these verses 16:25-27.} |