Warumi 10 Swahili & English
Listen/Download AudioWarumi 10 (Swahili) | Romans 10 (English) |
---|---|
Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe. Warumi 10:1 |
Brothers, my heart's desire and my prayer to God is for Israel, that they may be saved. |
Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Warumi 10:2 |
For I testify about them that they have a zeal for God, but not according to knowledge. |
Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu. Warumi 10:3 |
For being ignorant of God's righteousness, and seeking to establish their own righteousness, they didn't subject themselves to the righteousness of God. |
Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. Warumi 10:4 |
For Christ is the fulfillment{or, completion, or end} of the law for righteousness to everyone who believes. |
Kwa maana Musa aliandika juu ya haki itokayo kwa sheria, ya kuwa, Mtu afanyaye hiyo ataishi kwa hiyo. Warumi 10:5 |
For Moses writes about the righteousness of the law, "The one who does them will live by them." |
Bali ile haki ipatikanayo kwa imani yanena hivi, Usiseme moyoni mwako, Ni nani atakayepanda kwenda mbinguni? (Yaani, ni kumleta Kristo chini), Warumi 10:6 |
But the righteousness which is of faith says this, "Don't say in your heart, 'Who will ascend into heaven?' (that is, to bring Christ down); |
au, Ni nani atakayeshuka kwenda kuzimuni? (Yaani, ni kumleta Kristo juu, kutoka kwa wafu.) Warumi 10:7 |
or, 'Who will descend into the abyss?' (that is, to bring Christ up from the dead.)" |
Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo. Warumi 10:8 |
But what does it say? "The word is near you, in your mouth, and in your heart;" that is, the word of faith, which we preach: |
Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Warumi 10:9 |
that if you will confess with your mouth the Lord Jesus, and believe in your heart that God raised him from the dead, you will be saved. |
Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Warumi 10:10 |
For with the heart, one believes unto righteousness; and with the mouth confession is made unto salvation. |
Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. Warumi 10:11 |
For the Scripture says, "Whoever believes in him will not be disappointed." |
Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; Warumi 10:12 |
For there is no distinction between Jew and Greek; for the same Lord is Lord of all, and is rich to all who call on him. |
kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. Warumi 10:13 |
For, "Whoever will call on the name of the Lord will be saved." |
Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? Warumi 10:14 |
How then will they call on him in whom they have not believed? How will they believe in him whom they have not heard? How will they hear without a preacher? |
Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema! Warumi 10:15 |
And how will they preach unless they are sent? As it is written: "How beautiful are the feet of those who preach the Gospel of peace, Who bring glad tidings of good things!" |
Lakini si wote walioitii ile habari njema. Kwa maana Isaya asema, Bwana, ni nani aliyeziamini habari zetu? Warumi 10:16 |
But they didn't all listen to the glad news. For Isaiah says, "Lord, who has believed our report?" |
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo. Warumi 10:17 |
So faith comes by hearing, and hearing by the word of God. |
Lakini nasema, Je! Wao hawakusikia? Naam, wamesikia, Sauti yao imeenea duniani mwote, Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu. Warumi 10:18 |
But I say, didn't they hear? Yes, most assuredly, "Their sound went out into all the earth, Their words to the ends of the world." |
Lakini nasema, Je! Waisraeli hawakufahamu? Kwanza Musa anena, Nitawatia wivu kwa watu ambao si taifa, Kwa taifa lisilo na fahamu nitawaghadhibisha. Warumi 10:19 |
But I ask, didn't Israel know? First Moses says, "I will provoke you to jealousy with that which is no nation, With a nation void of understanding I will make you angry." |
Na Isaya anao ujasiri mwingi, asema, Nalipatikana nao wasionitafuta, Nalidhihirika kwao wasioniulizia. Warumi 10:20 |
Isaiah is very bold, and says, "I was found by those who didn't seek me. I was revealed to those who didn't ask for me." |
Lakini kwa Israeli asema, Mchana kutwa naliwanyoshea mikono watu wasiotii na wakaidi. Warumi 10:21 |
But as to Israel he says, "All day long I stretched out my hands to a disobedient and contrary people." |