Waebrania 3 Swahili & English
Listen/Download AudioWaebrania 3 (Swahili) | Hebrews 3 (English) |
---|---|
Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu, Waebrania 3:1 |
Therefore, holy brothers, partakers of a heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our confession, Jesus; |
aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, kama Musa naye alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu. Waebrania 3:2 |
who was faithful to him who appointed him, as also was Moses in all his house. |
Kwa maana huyo amehesabiwa kuwa amestahili utukufu zaidi kuliko Musa, kama vile yeye aitengenezaye nyumba alivyo na heshima zaidi ya hiyo nyumba. Waebrania 3:3 |
For he has been counted worthy of more glory than Moses, inasmuch as he who built the house has more honor than the house. |
Maana kila nyumba imetengenezwa na mtu; ila yeye aliyevitengeneza vitu vyote ni Mungu. Waebrania 3:4 |
For every house is built by someone; but he who built all things is God. |
Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, awe ushuhuda wa mambo yatakayonenwa baadaye; Waebrania 3:5 |
Moses indeed was faithful in all his house as a servant, for a testimony of those things which were afterward to be spoken, |
bali Kristo, kama mwana, juu ya nyumba ya Mungu; ambaye nyumba yake ni sisi, kama tukishikamana sana na ujasiri wetu na fahari ya taraja letu mpaka mwisho. Waebrania 3:6 |
but Christ is faithful as a Son over his house; whose house we are, if we hold fast our confidence and the glorying of our hope firm to the end. |
Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake, Waebrania 3:7 |
Therefore, even as the Holy Spirit says, "Today if you will hear his voice, |
Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha, Siku ya kujaribiwa katika jangwa, Waebrania 3:8 |
Don't harden your hearts, as in the provocation, Like as in the day of the trial in the wilderness, |
Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arobaini. Waebrania 3:9 |
Where your fathers tested me by proving me, And saw my works for forty years. |
Kwa hiyo nalichukizwa na kizazi hiki, Nikasema, Sikuzote ni watu waliopotoka mioyo hawa; Hawakuzijua njia zangu; Waebrania 3:10 |
Therefore I was displeased with that generation, And said, 'They always err in their heart, But they didn't know my ways;' |
Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu. Waebrania 3:11 |
As I swore in my wrath, 'They will not enter into my rest.'" |
Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu moyo mbovu wa kutokuamini, kwa kujitenga na Mungu aliye hai. Waebrania 3:12 |
Beware, brothers, lest perhaps there be in any one of you an evil heart of unbelief, in falling away from the living God; |
Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi. Waebrania 3:13 |
but exhort one another day by day, so long as it is called "today;" lest any one of you be hardened by the deceitfulness of sin. |
Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho; Waebrania 3:14 |
For we have become partakers of Christ, if we hold fast the beginning of our confidence firm to the end: |
hapo inenwapo, Leo, kama mtaisikia sauti yake, Msifanye migumu mioyo yenu, Kama wakati wa kukasirisha. Waebrania 3:15 |
while it is said, "Today if you will hear his voice, Don't harden your hearts, as in the rebellion." |
Maana ni akina nani waliokasirisha, waliposikia? Si wale wote waliotoka Misri wakiongozwa na Musa? Waebrania 3:16 |
For who, when they heard, rebelled? No, didn't all those who came out of Egypt by Moses? |
Tena ni akina nani aliochukizwa nao miaka arobaini? Si wale waliokosa, ambao mizoga yao ilianguka katika jangwa? Waebrania 3:17 |
With whom was he displeased forty years? Wasn't it with those who sinned, whose bodies fell in the wilderness? |
Tena ni akina nani aliowaapia ya kwamba hawataingia katika raha yake, ila wale walioasi? Waebrania 3:18 |
To whom did he swear that they wouldn't enter into his rest, but to those who were disobedient? |
Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao. Waebrania 3:19 |
We see that they were not able to enter in because of unbelief. |