Esta 10 Swahili & English

Listen/Download Audio
Esta 10 (Swahili) Esther 10 (English)

Basi mfalme Ahasuero alitoza kodi katika nchi na katika visiwa vya bahari. Esta 10:1

The king Ahasuerus laid a tribute on the land, and on the isles of the sea.

Na matendo yake yote yenye nguvu na ya ushujaa, na habari zote za ukuu wake Mordekai ambao alipewa na mfalme, hazikuandikwa katika kitabu-cha-taarifa cha wafalme wa Umedi na Uajemi? Esta 10:2

All the acts of his power and of his might, and the full account of the greatness of Mordecai, whereunto the king advanced him, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Media and Persia?

Kwa maana Mordekai Myahudi akawa wa pili wake mfalme Ahasuero, na mkuu wa Wayahudi, amependeza mbele ya jamii ya ndugu zake; ambaye aliwatafuta watu wake wema, na kuiangalia hali njema ya wazao wao wote. Esta 10:3

For Mordecai the Jew was next to king Ahasuerus, and great among the Jews, and accepted of the multitude of his brothers, seeking the good of his people, and speaking peace to all his seed.