Shari Martin - Rafiki Pesa Lyrics

Rafiki Pesa Lyrics

Nilikuwa na rafiki yangu
Rafiki Pesa Tulipendana sana
Maisha yetu yalikuwa mazuri
Nitakacho hunipatia

Nikitaka nyumba nzuri alikuwa anijengea
Nikitaka gari nzuri alikuwa aniletea
Nikitaka nguo nzuri anakimbia dukani aniletea
Nikitaka suti nzuri alikuwa aniletea
Nikitaka wanawake anakimbia Florida aniletea
Nikitaka kunywa beer alikuwa aniletea
(Instruments)

Siku moja nilishikwa na ugonjwa mbaya sana
Nikapelekwa kwa madakitari ugonjwa huo haukupona
Waliposhindwa nikarudishwa nchini kwetu nyumbani kwangu
Nikalazwa kitandani kwangu
Nilikuwa naumwa sana

Siku moja Rafiki Pesa akaja kwangu kunitazama
Akaniambia "Rafiki yangu pole sana kwa ugonjwa
Usijali hata ukifa nitakununulia coffin"
Siku ile nilikufa Rafiki Pesa alitoroka
Watoto wangu waliteseka, Majirani waliwacheka
"Pesa alithamini, sasa maisha kwisha"
Utaenda wapi? Utaenda motoni
Wakati urafiki wako na bwana Pesa unapoisha
Mambo mawili anakufanyia
Anakununua kitamba cheupe na coffin ya kukuingiza ndani
Walevi walikunywa pombe wakashindwa na kutembea
Wakitazama chini waona kuna mashimo
Wavuta bangi walivuta sana
Moshi nao ulipoganda
Hata nywele za vichwa zao wakashindwa kuzichana
Matajiri walipata pesa wakazieka kwa anasa
Nazo pesa zaendelea kuwanunulia sanduku

Matajiri walipata pesa wakazieka kwa anasa
Nazo pesa zaendelea kuwanunulia jeneza
Usithamini pesa Pesa zina mwisho, zina mwisho
Pesa zina mwisho Raha nazo baba
Raha zina mwisho, zina mwisho Raha zina mwisho
Shika Yesu baba Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho
Yesu ndiye mwisho Kwa wokovu Baba
Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho
Yesu ndiye mwisho Kwa wokovu Baba
Yesu ndiye mwisho, ndiye mwisho
Yesu ndiye mwisho


Rafiki Pesa Video

Shari Martin Songs

Related Songs