Obby Alpha - Vibaya Lyrics

Lyrics

Matatizo, yasikie kwa jirani

Yakikufika utanielewa

Kulala njaa, we sikia kwa jirani

Ukilala njaa, utanielewa

Kukataliwa, we sikia kwa jirani

Ukakataliwa, utanielewa

Usaliti usaliti, we sikia kwa jirani

Ukisalitiwa, utanielewa


Hapo ulipo

Ndugu yangu si kwa nguvu zako

Hivyo chunga kinywa chako

Usiwabeze walio chini yako

Hapo apo ulipo

Ndugu yangu si kwa nguvu zako

Hivyo chunga kinywa chako

Usiwabeze walio chini yako


Hivyo tusisemane (vibaya)

Tusiombeane (mabaya)

Tusisemane (vibaya vibaya vibaya)


Ooooh tusisemane (vibaya)

Tusiombeane (mabaya)

Tusisemane (vibaya vibaya vibaya)


Hauujuii haujuii

Kesho utakuwa wapi

Nami sijui sijui

Kesho nitakuwa wapi


Waweza niona mkosi

Kesho nikawa baraka

hivyo,Weka akiba ya maneno yako

Utanishukuru baadaye


Kwa leo ninaweza nikose

Ipo kesho nitapata

Hivyo, Weka akiba ya maneno yako

Utanishukuru baadaye


Apo ulipo

Ndugu yangu si kwa nguvu zako

Hivyo chunga kinywa chako

Usiwabeze walio chini yako


Apo ulipo

Ndugu yangu si kwa nguvu zako

Hivyo chunga kinywa chako

Usiwabeze walio chini yako


Hivyo tusisemane (vibaya)

Tusiombeane (mabaya)

Tusisemane (vibaya vibaya vibaya)


Ooooh tusisemane (vibaya)

Tusiombeane (mabaya)

Tusisemane (vibaya vibaya vibaya)

Video

Obby Alpha -Vibaya ( Official Video ) For SKIZA SMS 6989854 To 811

Thumbnail for Vibaya video
Loading...
In Queue
View Lyrics