Mambo yamebadilika, mambo yamebadilika
Ukieleza mambo yangu eleza ya sasa
Mambo yangu si vile, neema ameniona
Mambo yamebadilika eleza ya leo
Mambo yamebadilika, mambo yamebadilika
Ukieleza mambo yangu eleza ya sasa
Haa, wewe ni kila kitu Yesu
Naa naa naah nimetamwa na mimi
Mungu amenitoa mbali na mimi
Wakati kuzimu ilipanga kila siku nilie
Hivyo mbingu ilipanga nami nifurahi
Nilipochimbiwa shimoni nizame nisitoke tena
Hivyo mbingu ilipanga nitatoka namna gani
Ni vile hukujua ninapendwa na Mungu
Hukutambua nami nimefarijiwa
Ulieleza mabaya kila ulipopita
Naomba na leo tangaza haya mema
Waambie watu Mungu si mwanadamu
Mwambie watu amejawa na huruma
Mwambie Mungu ni wa wote kweli
Hana upendeleo kabisa
Usiwaambie watu mambo mabaya mabaya
Jifunze kusema yaliyo mema
Mambo yamebadilika, mambo yamebadilika
Ukieleza mambo yangu eleza ya sasa
Usiwaambie watu yule ni masikini
Waambie sasa amebarikiwa
Usiwaambie watu ule ni mama mjane tu
Waambie Yesu ni mume wa wajane
Usiwaambie ule ni mtoto yatima tu
Waambie Mungu ni Baba wa yatima
Usiwaambie watu yule ni mgonjwa namjua
Waambie Mungu anaponya kila kitu...
Mambo yamebadilika, mambo yamebadilika
Ukieleza mambo yangu eleza ya sasa