Erick Smith - Mateso Lyrics

Mateso Lyrics

Kwa kupigwa kwako tumepona 
Msalabani yote yamekwisha 
Kwa kupigwa kwako tumepona 
Msalabani yote yamekwisha 

Nikikumbuka mateso yake Yesu 
Alivyoteseka pale msalabani.
Fimbo, misumari, taji ya miba 
Mkuki ubavuni na kutemewa mate. 

Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 
Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 
Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki 
(rudia) 

Wakamkamata Yesu kama mwizi 
Na kumdharau Yesu mwana wa Mungu. 
Wakamkamata kama mwizi 
Wakumdharau Bwana mwana wa Mungu. 
Wakadhani kuwa ndio mwisho 
Kumbe ndio mwanzo wa wokovu wangu 
Kumbe ndio mwanzo wa wokovu wetu. 

Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 
Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 
Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki 
(rudia) 

Akasulubiwa Yesu Ju ya msalaba 
Akasema Baba, Baba oh wasamehe 
Kwani hawajui walitendalo oh ooh 
Ndipo Bwana wangu akakata roho 
Ndipo Bwana wangu akakata roho  

Kwa kupigwa kwako tumepona 
Msalabani yote yamekwisha 
Kwa kupigwa kwako tumepona 
Msalabani yote yamekwisha 

Mateso yake Yesu ilikuwa ni huzuni 
Mwana wa Mungu kafa bila hatia yeyote 
Ili mimi na wewe tuhesabiwe haki


Mateso Video

Mateso Lyrics -  Erick Smith

Erick Smith Songs

Related Songs