Wafilipi BSB

Wafilipi 2

Philippians Chapter 2

1
Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema,
Therefore if you have any encouragement in Christ, if any comfort from His love, if any fellowship with the Spirit, if any affection and compassion,
2
ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja.
then make my joy complete by being like-minded, having the same love, being united in spirit and purpose.
3
Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
Do nothing out of selfish ambition or empty pride, but in humility consider others more important than yourselves.
4
Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
Each of you should look not only to your own interests, but also to the interests of others.
5
Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Let this mind be in you which was also in Christ Jesus:
6
ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
Who, existing in the form of God, did not consider equality with God something to be grasped,
7
bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
but emptied Himself, taking the form of a servant, being made in human likeness.
8
tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
And being found in appearance as a man, He humbled Himself and became obedient to death—even death on a cross.
9
Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Therefore God exalted Him to the highest place and gave Him the name above all names,
10
ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
that at the name of Jesus every knee should bow, in heaven and on earth and under the earth,
11
na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
and every tongue confess that Jesus Christ is Lord, to the glory of God the Father.
12
Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
Therefore, my beloved, just as you have always obeyed, not only in my presence, but now even more in my absence, continue to work out your salvation with fear and trembling.
13
Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
For it is God who works in you to will and to act on behalf of His good purpose.
14
Yatendeni mambo yote pasipo manung'uniko wala mashindano,
Do everything without complaining or arguing,
15
mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,
so that you may be blameless and pure, children of God without fault in a crooked and perverse generation, in which you shine as lights in the world
16
mkishika neno la uzima; nipate sababu ya kuona fahari katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure.
as you hold forth the word of life, in order that I may boast on the day of Christ that I did not run or labor in vain.
17
Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
But even if I am being poured out like a drink offering on the sacrifice and service of your faith, I am glad and rejoice with all of you.
18
Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
So you too should be glad and rejoice with me.
19
Walakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo afike kwenu karibu, nifarijiwe na mimi, nikiijua hali yenu.
Now I hope in the Lord Jesus to send Timothy to you soon, that I also may be cheered when I learn how you are doing.
20
Maana sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli.
I have nobody else like him who will genuinely care for your needs.
21
Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.
For all the others look after their own interests, not those of Jesus Christ.
22
Ila mwajua sifa yake, ya kuwa ametumika pamoja nami kwa ajili ya Injili, kama mwana na baba yake.
But you know Timothy’s proven worth, that as a child with his father he has served with me to advance the gospel.
23
Basi, natumaini kumtuma huyo mara, hapo nitakapojua yatakayonipata.
So I hope to send him as soon as I see what happens with me.
24
Nami naamini katika Bwana ya kuwa nitakuja na mimi mwenyewe hivi karibu.
And I trust in the Lord that I myself will come soon.
25
Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu.
But I thought it necessary to send back to you Epaphroditus, my brother, fellow worker, and fellow soldier, who is also your messenger and minister to my needs.
26
Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi.
For he has been longing for all of you and is distressed because you heard he was ill.
27
Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.
He was sick indeed, nearly unto death. But God had mercy on him, and not only on him but also on me, to spare me sorrow upon sorrow.
28
Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.
Therefore I am all the more eager to send him, so that when you see him again you may rejoice, and I may be less anxious.
29
Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.
Welcome him in the Lord with great joy, and honor men like him,
30
Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu.
because he nearly died for the work of Christ, risking his life to make up for your deficit of service to me.

Chagua Sura

1 2 3 4