Wafilipi 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
Wafilipi 4 (Swahili) Philippians 4 (English)

Basi, ndugu zangu, wapendwa wangu, ninaowaonea shauku, furaha yangu, na taji yangu, hivyo simameni imara katika Bwana, wapenzi wangu. Wafilipi 4:1

Therefore, my brothers, beloved and longed for, my joy and crown, so stand firm in the Lord, my beloved.

Namsihi Euodia, namsihi na Sintike, wawe na nia moja katika Bwana. Wafilipi 4:2

I exhort Euodia, and I exhort Syntyche, to think the same way in the Lord.

Naam, nataka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa maana waliishindania Injili pamoja nami, na Klementi naye, na wale wengine waliotenda kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima. Wafilipi 4:3

Yes, I beg you also, true yoke-fellow, help these women, for they labored with me in the Gospel, with Clement also, and the rest of my fellow workers, whose names are in the book of life.

Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini. Wafilipi 4:4

Rejoice in the Lord always! Again I will say, Rejoice!

Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu. Wafilipi 4:5

Let your gentleness be known to all men. The Lord is at hand.

Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Wafilipi 4:6

In nothing be anxious, but in everything, by prayer and petition with thanksgiving, let your requests be made known to God.

Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. Wafilipi 4:7

And the peace of God, which surpasses all understanding, will guard your hearts and your thoughts in Christ Jesus.

Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo. Wafilipi 4:8

Finally, brothers, whatever things are true, whatever things are honorable, whatever things are just, whatever things are pure, whatever things are lovely, whatever things are of good report; if there is any virtue, and if there is any praise, think about these things.

Mambo mliyojifunza kwangu na kuyapokea, na kuyasikia na kuyaona kwangu, yatendeni hayo; na Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi. Wafilipi 4:9

The things which you learned, received, heard, and saw in me: do these things, and the God of peace will be with you.

Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi. Wafilipi 4:10

But I rejoice in the Lord greatly, that now at length you have revived your thought for me; in which you did indeed take thought, but you lacked opportunity.

Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo. Wafilipi 4:11

Not that I speak in respect to lack, for I have learned in whatever state I am, to be content in it.

Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa. Wafilipi 4:12

I know how to be humbled, and I know also how to abound. In everything and in all things I have learned the secret both to be filled and to be hungry, both to abound and to be in need.

Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu. Wafilipi 4:13

I can do all things through Christ, who strengthens me.

Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu. Wafilipi 4:14

However you did well that you shared in my affliction.

Nanyi pia, ninyi wenyewe mnajua, enyi Wafilipi, ya kuwa katika mwanzo wa Injili, nilipotoka Makedonia, hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika habari hii ya kutoa na kupokea, ila ninyi peke yenu. Wafilipi 4:15

You yourselves also know, you Philippians, that in the beginning of the Gospel, when I departed from Macedonia, no assembly shared with me in the matter of giving and receiving but you only.

Kwa kuwa hata huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu, wala si mara moja. Wafilipi 4:16

For even in Thessalonica you sent once and again to my need.

Si kwamba nakitamani kile kipawa, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, katika hesabu yenu. Wafilipi 4:17

Not that I seek for the gift, but I seek for the fruit that increases to your account.

Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu. Wafilipi 4:18

But I have all things, and abound. I am filled, having received from Epaphroditus the things that came from you, a sweet-smelling fragrance, an acceptable and well-pleasing sacrifice to God.

Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. Wafilipi 4:19

My God will supply every need of yours according to his riches in glory in Christ Jesus.

Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amina. Wafilipi 4:20

Now to our God and Father be the glory forever and ever! Amen.

Mnisalimie kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walio pamoja nami wawasalimu. Wafilipi 4:21

Greet every saint in Christ Jesus. The brothers who are with me greet you.

Watakatifu wote wawasalimu, hasa wao walio wa nyumbani mwa Kaisari. Wafilipi 4:22

All the saints greet you, especially those who are of Caesar's household.

Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Wafilipi 4:23

The grace of the Lord Jesus Christ be with you all. Amen.