Wafilipi 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
Wafilipi 3 (Swahili) Philippians 3 (English)

Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana. Kuwaandikieni mambo yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa ninyi. Wafilipi 3:1

Finally, my brothers, rejoice in the Lord. To write the same things to you, to me indeed is not tiresome, but for you it is safe.

Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao. Wafilipi 3:2

Beware of the dogs, beware of the evil workers, beware of the false circumcision.

Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili. Wafilipi 3:3

For we are the circumcision, who worship God in the Spirit, and rejoice in Christ Jesus, and have no confidence in the flesh;

Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu ye yote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi. Wafilipi 3:4

though I myself might have confidence even in the flesh. If any other man thinks that he has confidence in the flesh, I yet more:

Nalitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli, wa kabila ya Benyamini, Mwebrania wa Waebrania, kwa habari ya kuishika torati, ni Farisayo, Wafilipi 3:5

circumcised the eighth day, of the stock of Israel, of the tribe of Benjamin, a Hebrew of Hebrews; concerning the law, a Pharisee;

kwa habari ya juhudi, mwenye kuliudhi Kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na hatia. Wafilipi 3:6

concerning zeal, persecuting the assembly; concerning the righteousness which is in the law, found blameless.

Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. Wafilipi 3:7

However, what things were gain to me, these have I counted loss for Christ.

Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo; Wafilipi 3:8

Yes most assuredly, and I count all things to be loss for the excellency of the knowledge of Christ Jesus, my Lord, for whom I suffered the loss of all things, and count them nothing but refuse, that I may gain Christ

tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani; Wafilipi 3:9

and be found in him, not having a righteousness of my own, that which is of the law, but that which is through faith in Christ, the righteousness which is from God by faith;

ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake; Wafilipi 3:10

that I may know him, and the power of his resurrection, and the fellowship of his sufferings, becoming conformed to his death;

ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu. Wafilipi 3:11

if by any means I may attain to the resurrection from the dead.

Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. Wafilipi 3:12

Not that I have already obtained, or am already made perfect; but I press on, if it is so that I may take hold of that for which also I was taken hold of by Christ Jesus.

Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; Wafilipi 3:13

Brothers, I don't regard myself as yet having taken hold, but one thing I do. Forgetting the things which are behind, and stretching forward to the things which are before,

nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu. Wafilipi 3:14

I press on toward the goal for the prize of the high calling of God in Christ Jesus.

Basi sisi tulio wakamilifu na tuwaze hayo; na hata mkiwaza mengine katika jambo lo lote, Mungu atawafunulia hilo nalo. Wafilipi 3:15

Let us therefore, as many as are perfect, think this way. If in anything you think otherwise, God will also reveal that to you.

Lakini, hapo tulipofika na tuenende katika lilo hilo. Wafilipi 3:16

Nevertheless, to the extent that we have already attained, let us walk by the same rule. Let us be of the same mind.

Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi. Wafilipi 3:17

Brothers, be imitators together of me, and note those who walk this way, even as you have us for an example.

Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo; Wafilipi 3:18

For many walk, of whom I told you often, and now tell you even weeping, as the enemies of the cross of Christ,

mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani. Wafilipi 3:19

whose end is destruction, whose god is the belly, and whose glory is in their shame, who think about earthly things.

Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; Wafilipi 3:20

For our citizenship is in heaven, from where we also wait for a Savior, the Lord Jesus Christ;

atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake. Wafilipi 3:21

who will change the body of our humiliation to be conformed to the body of his glory, according to the working by which he is able even to subject all things to himself.