Maombolezo 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
Maombolezo 3 (Swahili) Lamentations 3 (English)

Mimi ni mtu aliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake. Maombolezo 3:1

I am the man that has seen affliction by the rod of his wrath.

Ameniongoza na kuniendesha katika giza Wala si katika nuru. Maombolezo 3:2

He has led me and caused me to walk in darkness, and not in light.

Hakika juu yangu augeuza mkono wake Mara kwa mara mchana wote. Maombolezo 3:3

Surely against me he turns his hand again and again all the day.

Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu; Ameivunja mifupa yangu. Maombolezo 3:4

My flesh and my skin has he made old; he has broken my bones.

Amejenga boma juu yangu, Na kunizungusha uchungu na uchovu. Maombolezo 3:5

He has built against me, and compassed me with gall and travail.

Amenikalisha penye giza, Kama watu waliokufa zamani. Maombolezo 3:6

He has made me to dwell in dark places, as those that have been long dead.

Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka; Ameufanya mnyororo wangu mzito. Maombolezo 3:7

He has walled me about, that I can't go forth; he has made my chain heavy.

Naam, nikilia na kuomba msaada, Huyapinga maombi yangu. Maombolezo 3:8

Yes, when I cry, and call for help, he shuts out my prayer.

Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu. Maombolezo 3:9

He has walled up my ways with hewn stone; he has made my paths crooked.

Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye, Kama simba aliye mafichoni. Maombolezo 3:10

He is to me as a bear lying in wait, as a lion in secret places.

Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua; Amenifanya ukiwa. Maombolezo 3:11

He has turned aside my ways, and pulled me in pieces; he has made me desolate.

Ameupinda upinde wake, Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale. Maombolezo 3:12

He has bent his bow, and set me as a mark for the arrow.

Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake. Maombolezo 3:13

He has caused the shafts of his quiver to enter into my reins.

Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote; Wimbo wao mchana kutwa. Maombolezo 3:14

I am become a derision to all my people, and their song all the day.

Amenijaza uchungu, Amenikinaisha kwa pakanga. Maombolezo 3:15

He has filled me with bitterness, he has sated me with wormwood.

Amenivunja meno kwa changarawe; Amenifunika majivu. Maombolezo 3:16

He has also broken my teeth with gravel stones; he has covered me with ashes.

Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa. Maombolezo 3:17

You have removed my soul far off from peace; I forgot prosperity.

Nikasema, Nguvu zangu zimepotea, Na tumaini langu kwa Bwana. Maombolezo 3:18

I said, My strength is perished, and my expectation from Yahweh.

Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu, Pakanga na nyongo. Maombolezo 3:19

Remember my affliction and my misery, the wormwood and the gall.

Nafsi yangu ikali ikiyakumbuka hayo, Nayo imeinama ndani yangu. Maombolezo 3:20

My soul still remembers them, and is bowed down within me.

Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini. Maombolezo 3:21

This I recall to my mind; therefore have I hope.

Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi. Maombolezo 3:22

[It is of] Yahweh's loving kindnesses that we are not consumed, because his compassion doesn't fail.

Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu. Maombolezo 3:23

They are new every morning; great is your faithfulness.

Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye. Maombolezo 3:24

Yahweh is my portion, says my soul; therefore will I hope in him.

Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo. Maombolezo 3:25

Yahweh is good to those who wait for him, to the soul that seeks him.

Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu. Maombolezo 3:26

It is good that a man should hope and quietly wait for the salvation of Yahweh.

Ni vema mwanadamu aichukue nira Wakati wa ujana wake. Maombolezo 3:27

It is good for a man that he bear the yoke in his youth.

Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake. Maombolezo 3:28

Let him sit alone and keep silence, because he has laid it on him.

Na atie kinywa chake mavumbini; Ikiwa yamkini liko tumaini. Maombolezo 3:29

Let him put his mouth in the dust, if so be there may be hope.

Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu. Maombolezo 3:30

Let him give his cheek to him who strikes him; let him be filled full with reproach.

Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele. Maombolezo 3:31

For the Lord will not cast off forever.

Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake. Maombolezo 3:32

For though he cause grief, yet will he have compassion according to the multitude of his loving kindnesses.

Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha. Maombolezo 3:33

For he does not afflict willingly, nor grieve the children of men.

Kuwaseta chini kwa miguu Wafungwa wote wa duniani, Maombolezo 3:34

To crush under foot all the prisoners of the earth,

Kuipotosha hukumu ya mtu Mbele zake Aliye juu, Maombolezo 3:35

To turn aside the right of a man before the face of the Most High,

Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa. Maombolezo 3:36

To subvert a man in his cause, the Lord doesn't approve.

Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza? Maombolezo 3:37

Who is he who says, and it comes to pass, when the Lord doesn't command it?

Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema? Maombolezo 3:38

Doesn't evil and good come out of the mouth of the Most High?

Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake? Maombolezo 3:39

Why does a living man complain, a man for the punishment of his sins?

Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, Na kumrudia Bwana tena. Maombolezo 3:40

Let us search and try our ways, and turn again to Yahweh.

Na tumwinulie Mungu aliye mbinguni Mioyo yetu na mikono. Maombolezo 3:41

Let us lift up our heart with our hands to God in the heavens.

Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe. Maombolezo 3:42

We have transgressed and have rebelled; you have not pardoned.

Umetufunika kwa hasira na kutufuatia; Umeua, wala hukuona huruma. Maombolezo 3:43

You have covered with anger and pursued us; you have killed, you have not pitied.

Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite. Maombolezo 3:44

You have covered yourself with a cloud, so that no prayer can pass through.

Umetufanya kuwa takataka, na vifusi Katikati ya mataifa. Maombolezo 3:45

You have made us an off-scouring and refuse in the midst of the peoples.

Juu yetu adui zetu wote Wametupanulia vinywa vyao. Maombolezo 3:46

All our enemies have opened their mouth wide against us.

Hofu imetujilia na shimo, Ukiwa na uharibifu. Maombolezo 3:47

Fear and the pit are come on us, devastation and destruction.

Jicho langu lachuruzika mito ya maji Kwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu. Maombolezo 3:48

My eye runs down with streams of water, for the destruction of the daughter of my people.

Jicho langu latoka machozi lisikome, Wala haliachi; Maombolezo 3:49

My eye pours down, and doesn't cease, without any intermission,

Hata Bwana atakapoangalia Na kutazama toka mbinguni. Maombolezo 3:50

Until Yahweh look down, and see from heaven.

Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa sababu ya binti zote za mji wangu. Maombolezo 3:51

My eye affects my soul, because of all the daughters of my city.

Walio adui zangu bila sababu Wameniwinda sana kama ndege; Maombolezo 3:52

They have chased me sore like a bird, those who are my enemies without cause.

Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu. Maombolezo 3:53

They have cut off my life in the dungeon, and have cast a stone on me.

Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu, Nikasema, Nimekatiliwa mbali. Maombolezo 3:54

Waters flowed over my head; I said, I am cut off.

Naliliitia jina lako, Bwana, kutoka lile shimo Liendalo chini kabisa. Maombolezo 3:55

I called on your name, Yahweh, out of the lowest dungeon.

Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lako Ili usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu. Maombolezo 3:56

You heard my voice; don't hide your ear at my breathing, at my cry.

Ulinikaribia siku ile nilipokulilia; Ukasema, Usiogope. Maombolezo 3:57

You drew near in the day that I called on you; you said, Don't be afraid.

Ee Bwana umenitetea mateto ya nafsi yangu; Umeukomboa uhai wangu. Maombolezo 3:58

Lord, you have pleaded the causes of my soul; you have redeemed my life.

Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee Bwana; Unihukumie neno langu. Maombolezo 3:59

Yahweh, you have seen my wrong; judge you my cause.

Umekiona kisasi chao chote, Na mashauri yao yote juu yangu. Maombolezo 3:60

You have seen all their vengeance and all their devices against me.

Ee Bwana, umeyasikia matukano yao, Na mashauri yao yote juu yangu; Maombolezo 3:61

You have heard their reproach, Yahweh, and all their devices against me,

Midomo yao walioinuka juu yangu Na maazimio yao juu yangu mchana kutwa. Maombolezo 3:62

The lips of those that rose up against me, and their device against me all the day.

Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao; Wimbo wao ndio mimi. Maombolezo 3:63

See you their sitting down, and their rising up; I am their song.

Utawalipa malipo, Ee Bwana, Sawasawa na kazi ya mikono yao. Maombolezo 3:64

You will render to them a recompense, Yahweh, according to the work of their hands.

Utawapa ushupavu wa moyo; Laana yako juu yao. Maombolezo 3:65

You will give them hardness of heart, your curse to them.

Utawafuatia kwa hasira, na kuwaangamiza Wasiwe tena chini ya mbingu za Bwana. Maombolezo 3:66

You will pursue them in anger, and destroy them from under the heavens of Yahweh.