Maombolezo 3 Swahili & English
Listen/Download AudioMaombolezo 3 (Swahili) | Lamentations 3 (English) |
---|---|
Mimi ni mtu aliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake. Maombolezo 3:1 |
I am the man that has seen affliction by the rod of his wrath. |
Ameniongoza na kuniendesha katika giza Wala si katika nuru. Maombolezo 3:2 |
He has led me and caused me to walk in darkness, and not in light. |
Hakika juu yangu augeuza mkono wake Mara kwa mara mchana wote. Maombolezo 3:3 |
Surely against me he turns his hand again and again all the day. |
Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu; Ameivunja mifupa yangu. Maombolezo 3:4 |
My flesh and my skin has he made old; he has broken my bones. |
Amejenga boma juu yangu, Na kunizungusha uchungu na uchovu. Maombolezo 3:5 |
He has built against me, and compassed me with gall and travail. |
Amenikalisha penye giza, Kama watu waliokufa zamani. Maombolezo 3:6 |
He has made me to dwell in dark places, as those that have been long dead. |
Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka; Ameufanya mnyororo wangu mzito. Maombolezo 3:7 |
He has walled me about, that I can't go forth; he has made my chain heavy. |
Naam, nikilia na kuomba msaada, Huyapinga maombi yangu. Maombolezo 3:8 |
Yes, when I cry, and call for help, he shuts out my prayer. |
Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu. Maombolezo 3:9 |
He has walled up my ways with hewn stone; he has made my paths crooked. |
Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye, Kama simba aliye mafichoni. Maombolezo 3:10 |
He is to me as a bear lying in wait, as a lion in secret places. |
Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua; Amenifanya ukiwa. Maombolezo 3:11 |
He has turned aside my ways, and pulled me in pieces; he has made me desolate. |
Ameupinda upinde wake, Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale. Maombolezo 3:12 |
He has bent his bow, and set me as a mark for the arrow. |
Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake. Maombolezo 3:13 |
He has caused the shafts of his quiver to enter into my reins. |
Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote; Wimbo wao mchana kutwa. Maombolezo 3:14 |
I am become a derision to all my people, and their song all the day. |
Amenijaza uchungu, Amenikinaisha kwa pakanga. Maombolezo 3:15 |
He has filled me with bitterness, he has sated me with wormwood. |
Amenivunja meno kwa changarawe; Amenifunika majivu. Maombolezo 3:16 |
He has also broken my teeth with gravel stones; he has covered me with ashes. |
Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa. Maombolezo 3:17 |
You have removed my soul far off from peace; I forgot prosperity. |
Nikasema, Nguvu zangu zimepotea, Na tumaini langu kwa Bwana. Maombolezo 3:18 |
I said, My strength is perished, and my expectation from Yahweh. |
Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu, Pakanga na nyongo. Maombolezo 3:19 |
Remember my affliction and my misery, the wormwood and the gall. |
Nafsi yangu ikali ikiyakumbuka hayo, Nayo imeinama ndani yangu. Maombolezo 3:20 |
My soul still remembers them, and is bowed down within me. |
Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini. Maombolezo 3:21 |
This I recall to my mind; therefore have I hope. |
Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi. Maombolezo 3:22 |
[It is of] Yahweh's loving kindnesses that we are not consumed, because his compassion doesn't fail. |
Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu. Maombolezo 3:23 |
They are new every morning; great is your faithfulness. |
Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye. Maombolezo 3:24 |
Yahweh is my portion, says my soul; therefore will I hope in him. |
Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo. Maombolezo 3:25 |
Yahweh is good to those who wait for him, to the soul that seeks him. |
Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu. Maombolezo 3:26 |
It is good that a man should hope and quietly wait for the salvation of Yahweh. |
Ni vema mwanadamu aichukue nira Wakati wa ujana wake. Maombolezo 3:27 |
It is good for a man that he bear the yoke in his youth. |
Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake. Maombolezo 3:28 |
Let him sit alone and keep silence, because he has laid it on him. |
Na atie kinywa chake mavumbini; Ikiwa yamkini liko tumaini. Maombolezo 3:29 |
Let him put his mouth in the dust, if so be there may be hope. |
Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu. Maombolezo 3:30 |
Let him give his cheek to him who strikes him; let him be filled full with reproach. |
Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele. Maombolezo 3:31 |
For the Lord will not cast off forever. |
Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake. Maombolezo 3:32 |
For though he cause grief, yet will he have compassion according to the multitude of his loving kindnesses. |
Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha. Maombolezo 3:33 |
For he does not afflict willingly, nor grieve the children of men. |
Kuwaseta chini kwa miguu Wafungwa wote wa duniani, Maombolezo 3:34 |
To crush under foot all the prisoners of the earth, |
Kuipotosha hukumu ya mtu Mbele zake Aliye juu, Maombolezo 3:35 |
To turn aside the right of a man before the face of the Most High, |
Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa. Maombolezo 3:36 |
To subvert a man in his cause, the Lord doesn't approve. |
Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza? Maombolezo 3:37 |
Who is he who says, and it comes to pass, when the Lord doesn't command it? |
Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema? Maombolezo 3:38 |
Doesn't evil and good come out of the mouth of the Most High? |
Mbona anung'unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake? Maombolezo 3:39 |
Why does a living man complain, a man for the punishment of his sins? |
Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, Na kumrudia Bwana tena. Maombolezo 3:40 |
Let us search and try our ways, and turn again to Yahweh. |
Na tumwinulie Mungu aliye mbinguni Mioyo yetu na mikono. Maombolezo 3:41 |
Let us lift up our heart with our hands to God in the heavens. |
Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe. Maombolezo 3:42 |
We have transgressed and have rebelled; you have not pardoned. |
Umetufunika kwa hasira na kutufuatia; Umeua, wala hukuona huruma. Maombolezo 3:43 |
You have covered with anger and pursued us; you have killed, you have not pitied. |
Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite. Maombolezo 3:44 |
You have covered yourself with a cloud, so that no prayer can pass through. |
Umetufanya kuwa takataka, na vifusi Katikati ya mataifa. Maombolezo 3:45 |
You have made us an off-scouring and refuse in the midst of the peoples. |
Juu yetu adui zetu wote Wametupanulia vinywa vyao. Maombolezo 3:46 |
All our enemies have opened their mouth wide against us. |
Hofu imetujilia na shimo, Ukiwa na uharibifu. Maombolezo 3:47 |
Fear and the pit are come on us, devastation and destruction. |
Jicho langu lachuruzika mito ya maji Kwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu. Maombolezo 3:48 |
My eye runs down with streams of water, for the destruction of the daughter of my people. |
Jicho langu latoka machozi lisikome, Wala haliachi; Maombolezo 3:49 |
My eye pours down, and doesn't cease, without any intermission, |
Hata Bwana atakapoangalia Na kutazama toka mbinguni. Maombolezo 3:50 |
Until Yahweh look down, and see from heaven. |
Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa sababu ya binti zote za mji wangu. Maombolezo 3:51 |
My eye affects my soul, because of all the daughters of my city. |
Walio adui zangu bila sababu Wameniwinda sana kama ndege; Maombolezo 3:52 |
They have chased me sore like a bird, those who are my enemies without cause. |
Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu. Maombolezo 3:53 |
They have cut off my life in the dungeon, and have cast a stone on me. |
Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu, Nikasema, Nimekatiliwa mbali. Maombolezo 3:54 |
Waters flowed over my head; I said, I am cut off. |
Naliliitia jina lako, Bwana, kutoka lile shimo Liendalo chini kabisa. Maombolezo 3:55 |
I called on your name, Yahweh, out of the lowest dungeon. |
Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lako Ili usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu. Maombolezo 3:56 |
You heard my voice; don't hide your ear at my breathing, at my cry. |
Ulinikaribia siku ile nilipokulilia; Ukasema, Usiogope. Maombolezo 3:57 |
You drew near in the day that I called on you; you said, Don't be afraid. |
Ee Bwana umenitetea mateto ya nafsi yangu; Umeukomboa uhai wangu. Maombolezo 3:58 |
Lord, you have pleaded the causes of my soul; you have redeemed my life. |
Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee Bwana; Unihukumie neno langu. Maombolezo 3:59 |
Yahweh, you have seen my wrong; judge you my cause. |
Umekiona kisasi chao chote, Na mashauri yao yote juu yangu. Maombolezo 3:60 |
You have seen all their vengeance and all their devices against me. |
Ee Bwana, umeyasikia matukano yao, Na mashauri yao yote juu yangu; Maombolezo 3:61 |
You have heard their reproach, Yahweh, and all their devices against me, |
Midomo yao walioinuka juu yangu Na maazimio yao juu yangu mchana kutwa. Maombolezo 3:62 |
The lips of those that rose up against me, and their device against me all the day. |
Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao; Wimbo wao ndio mimi. Maombolezo 3:63 |
See you their sitting down, and their rising up; I am their song. |
Utawalipa malipo, Ee Bwana, Sawasawa na kazi ya mikono yao. Maombolezo 3:64 |
You will render to them a recompense, Yahweh, according to the work of their hands. |
Utawapa ushupavu wa moyo; Laana yako juu yao. Maombolezo 3:65 |
You will give them hardness of heart, your curse to them. |
Utawafuatia kwa hasira, na kuwaangamiza Wasiwe tena chini ya mbingu za Bwana. Maombolezo 3:66 |
You will pursue them in anger, and destroy them from under the heavens of Yahweh. |