Ezra 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ezra 4 (Swahili) Ezra 4 (English)

Basi adui za Yuda na Benyamini, waliposikia ya kuwa wana wa uhamisho wanamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, hekalu, Ezra 4:1

Now when the adversaries of Judah and Benjamin heard that the children of the captivity were building a temple to Yahweh, the God of Israel;

wakamkaribia Zerubabeli, na wakuu wa mbari za mababa, wakawaambia, Na tujenge sisi nasi pamoja nanyi; kwa maana tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi, nasi twamtolea dhabihu tangu zamani za Esar-hadoni, mfalme wa Ashuru, aliyetupandisha mpaka hapa. Ezra 4:2

then they drew near to Zerubbabel, and to the heads of fathers' [houses], and said to them, Let us build with you; for we seek your God, as you do; and we sacrifice to him since the days of Esar Haddon king of Assyria, who brought us up here.

Lakini Zerubabeli, na Yoshua, na wakuu wengine wa mbari za mababa katika Israeli, wakawaambia, Ninyi haiwahusu kushirikiana nasi katika kumjengea Mungu wetu nyumba; bali sisi wenyewe peke yetu tutamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, nyumba, kama mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi, alivyotuamuru. Ezra 4:3

But Zerubbabel, and Jeshua, and the rest of the heads of fathers' [houses] of Israel, said to them, You have nothing to do with us in building a house to our God; but we ourselves together will build to Yahweh, the God of Israel, as king Cyrus the king of Persia has commanded us.

Ndipo watu wa nchi wakaidhoofisha mikono ya watu wa Yuda, wakawasumbua, walipokuwa wakijenga. Ezra 4:4

Then the people of the land weakened the hands of the people of Judah, and troubled them in building,

Wakawaajiri washauri juu yao, ili kuwapinga kusudi lao, siku zote za Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata wakati wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi. Ezra 4:5

and hired counselors against them, to frustrate their purpose, all the days of Cyrus king of Persia, even until the reign of Darius king of Persia.

Tena, wakati wa kutawala kwake Ahasuero, mwanzo wa kutawala kwake, watu wakaandika mashitaka juu ya wenyeji wa Yuda na Yerusalemu. Ezra 4:6

In the reign of Ahasuerus, in the beginning of his reign, wrote they an accusation against the inhabitants of Judah and Jerusalem.

Na tena, katika siku za Artashasta, Mithredathi, na Tabeeli na mabaki ya wenziwe, wakimwandikia Artashasta, mfalme wa Uajemi, salamu za heri; na mwandiko wa waraka huo, ukaandikwa kwa herufi za Kiaramu, na kunenwa kwa lugha ya Kiaramu. Ezra 4:7

In the days of Artaxerxes wrote Bishlam, Mithredath, Tabeel, and the rest of his companions, to Artaxerxes king of Persia; and the writing of the letter was written in the Syrian [character], and set forth in the Syrian [language].

Nao Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, wakaandika waraka juu ya Yerusalemu kwa Artashasta, mfalme, kama hivi; Ezra 4:8

Rehum the chancellor and Shimshai the scribe wrote a letter against Jerusalem to Artaxerxes the king in this sort:

Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na mabaki ya wenzao, makadhi wa Kiajemi na madiwani wa Kiajemi; na Waarkewi, Wababeli, Washushani, yaani, Waelami; Ezra 4:9

then [wrote] Rehum the chancellor, and Shimshai the scribe, and the rest of their companions, the Dinaites, and the Apharsathchites, the Tarpelites, the Apharsites, the Archevites, the Babylonians, the Shushanchites, the Dehaites, the Elamites,

na mabaki ya mataifa, ambao Asur-bani-pali mkuu, mwenye heshima, aliwavusha, na kuwakalisha katika mji wa Samaria, na mahali penginepo, ng'ambo ya Mto; wakadhalika. Ezra 4:10

and the rest of the nations whom the great and noble Osnappar brought over, and set in the city of Samaria, and in the rest [of the country] beyond the River, and so forth.

Hii ndiyo nakili ya waraka waliyompelekea mfalme Artashasta;watumishi wako,watu walio ng`ambo ya mto wakadhalika. Ezra 4:11

This is the copy of the letter that they sent to Artaxerxes the king: Your servants the men beyond the River, and so forth.

Ijulikane kwa mfalme ya kuwa Wayahudi, waliokwea kutoka kwako, wamefika kwetu Yerusalemu; nao wanaujenga ule mji mwasi, mbaya; wamemaliza kuta zake, na kuitengeneza misingi yake. Ezra 4:12

Be it known to the king, that the Jews who came up from you are come to us to Jerusalem; they are building the rebellious and the bad city, and have finished the walls, and repaired the foundations.

Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara. Ezra 4:13

Be it known now to the king that if this city is built, and the walls finished, they will not pay tribute, custom, or toll, and in the end it will be hurtful to the kings.

Na sisi, kwa kuwa tunakula chumvi ya nyumba ya mfalme, wala si wajibu wetu kumwona mfalme akivunjiwa heshima, basi tumetuma watu na kumwarifu mfalme. Ezra 4:14

Now because we eat the salt of the palace, and it is not appropriate for us to see the king's dishonor, therefore have we sent and informed the king;

Ili habari zitafutwe katika kitabu cha tarehe za baba zako; ndivyo utakavyopata kujua kwa kitabu cha tarehe ya kuwa mji huo ni mji mwasi, wenye kuwadhuru wafalme, na maliwali, na ya kuwa wenyeji wake wamefanya fitina katika mji huo zamani; ndiyo sababu mji huo ukaangamizwa. Ezra 4:15

that search may be made in the book of the records of your fathers: so shall you find in the book of the records, and know that this city is a rebellious city, and hurtful to kings and provinces, and that they have moved sedition within the same of old time; for which cause was this city laid waste.

Twamwarifu mfalme ya kuwa mji huo ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hutakuwa na sehemu ya nchi ng'ambo ya Mto. Ezra 4:16

We inform the king that, if this city be built, and the walls finished, by this means you shall have no portion beyond the River.

Ndipo mfalme akapeleka majibu;Kwa Rehumu,Bwana shauri, na Shimshai,mwandishi na wenzao wengine waliokaa katika Samaria,na penginepo ng`ambo ya mto, Salamu; wakadharika. Ezra 4:17

[Then] sent the king an answer to Rehum the chancellor, and to Shimshai the scribe, and to the rest of their companions who dwell in Samaria, and in the rest [of the country] beyond the River: Peace, and so forth.

Ule waraka mlionipelekea umesomwa mbele yangu, nami nikaelewa na maana yake. Ezra 4:18

The letter which you sent to us has been plainly read before me.

Nikatoa amri, na watu wametafuta habari; ikaonekana ya kuwa mji huu zamani umefanya fitina juu ya wafalme, na ya kuwa uasi na fitina zimefanyika ndani yake. Ezra 4:19

I decreed, and search has been made, and it is found that this city of old time has made insurrection against kings, and that rebellion and sedition have been made therein.

Tena walikuwako wafalme wakuu juu ya Yerusalemu, waliotawala nchi yote iliyo ng'ambo ya Mto; wakapewa kodi, na ada, na ushuru. Ezra 4:20

There have been mighty kings also over Jerusalem, who have ruled over all [the country] beyond the River; and tribute, custom, and toll, was paid to them.

Sasa toeni amri kuwakomesha watu hawa kazi yao, mji huu usijengwe, hata mimi nitakapotoa amri. Ezra 4:21

Make you now a decree to cause these men to cease, and that this city not be built, until a decree shall be made by me.

Tena jihadharini, msilegee katika jambo hili; kwa nini madhara yazidi, na wafalme wapate hasara? Ezra 4:22

Take heed that you not be slack herein: why should damage grow to the hurt of the kings?

Hata nakala ya waraka huo wa mfalme Artashasta uliposomwa mbele ya Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na wenzao, wakaenda Yerusalemu upesi, kwa Wayahudi, wakawakomesha kwa nguvu na kwa kuwashurutisha. Ezra 4:23

Then when the copy of king Artaxerxes' letter was read before Rehum, and Shimshai the scribe, and their companions, they went in haste to Jerusalem to the Jews, and made them to cease by force and power.

Hivyo kazi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu ikakoma; nayo ikakoma hata mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi. Ezra 4:24

Then ceased the work of the house of God which is at Jerusalem; and it ceased until the second year of the reign of Darius king of Persia.