Ezra 10 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ezra 10 (Swahili) Ezra 10 (English)

Basi hapo Ezra alipokuwa akiomba na kuungama, akilia, na kujiangusha kifudifudi mbele ya nyumba ya Mungu, wakamkusanyikia katika Israeli wote kusanyiko kubwa sana la wanaume, na wanawake, na watoto; maana watu hao walikuwa wakilia sana. Ezra 10:1

Now while Ezra prayed and made confession, weeping and casting himself down before the house of God, there was gathered together to him out of Israel a very great assembly of men and women and children; for the people wept very sore.

Hata Shekania, mwana wa Yehieli, mmoja wa wana wa Elamu, akajibu, akamwambia Ezra, Sisi tumemkosa Mungu wetu, nasi tumeoa wanawake wageni wa watu wa nchi hizi; lakini kungaliko tumaini kwa Israeli katika jambo hili. Ezra 10:2

Shecaniah the son of Jehiel, one of the sons of Elam, answered Ezra, We have trespassed against our God, and have married foreign women of the peoples of the land: yet now there is hope for Israel concerning this thing.

Haya basi! Na tufanye agano na Mungu wetu, kuachana na wake zetu, na wale waliozaliwa nao, tukilifuata shauri la bwana wangu, na shauri la hao wanaoitetemekea amri ya Mungu wetu; mambo haya na yatendeke kwa kuifuata torati. Ezra 10:3

Now therefore let us make a covenant with our God to put away all the wives, and such as are born of them, according to the counsel of my lord, and of those who tremble at the commandment of our God; and let it be done according to the law.

Inuka; maana shughuli hii yakuhusu wewe; na sisi tu pamoja nawe; uwe na moyo mkuu, ukaitende. Ezra 10:4

Arise; for the matter belongs to you, and we are with you: be of good courage, and do it.

Ndipo Ezra akaondoka, akawaapisha wakuu wa makuhani, na Walawi, na Israeli wote, ya kwamba watafanya kama hayo. Basi wakaapa. Ezra 10:5

Then arose Ezra, and made the chiefs of the priests, the Levites, and all Israel, to swear that they would do according to this word. So they swore.

Kisha Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu, akaingia katika chumba cha Yehohanani, mwana wa Eliashibu; hata, alipofika huko, hakula mkate, wala hakunywa maji; kwa maana alilia kwa sababu ya kosa lile la watu wa uhamisho. Ezra 10:6

Then Ezra rose up from before the house of God, and went into the chamber of Jehohanan the son of Eliashib: and [when] he came there, he ate no bread, nor drink water; for he mourned because of the trespass of them of the captivity.

Wakapiga mbiu katika Yuda yote na Yerusalemu, ya kwamba wana wote wa uhamisho wakusanyike pamoja huko Yerusalemu; Ezra 10:7

They made proclamation throughout Judah and Jerusalem to all the children of the captivity, that they should gather themselves together to Jerusalem;

na ya kwamba mtu awaye yote asiyekuja katika muda wa siku tatu, kwa shauri lile la wakuu na wazee, basi aondolewe mali zake zote, akatengwe yeye mwenyewe na mkutano wa uhamisho. Ezra 10:8

and that whoever didn't come within three days, according to the counsel of the princes and the elders, all his substance should be forfeited, and himself separated from the assembly of the captivity.

Ndipo wanaume wote wa Yuda na Benyamini wakakusanyika katika muda wa siku tatu; ulikuwa mwezi wa kenda, siku ya ishirini ya mwezi; na watu wote wakaketi katika uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakitetemeka kwa sababu ya neno hilo, na kwa sababu ya mvua kubwa. Ezra 10:9

Then all the men of Judah and Benjamin gathered themselves together to Jerusalem within the three days; it was the ninth month, on the twentieth [day] of the month: and all the people sat in the broad place before the house of God, trembling because of this matter, and for the great rain.

Kisha Ezra, kuhani, akasimama, akawaambia, Mmekosa, mmeoa wanawake wageni, kuiongeza hatia ya Israeli. Ezra 10:10

Ezra the priest stood up, and said to them, You have trespassed, and have married foreign women, to increase the guilt of Israel.

Sasa basi, ungameni mbele za Bwana, Mungu wa baba zenu, mkatende alipendalo; mkajitenge na watu wa nchi, tena na wanawake wageni. Ezra 10:11

Now therefore make confession to Yahweh, the God of your fathers, and do his pleasure; and separate yourselves from the peoples of the land, and from the foreign women.

Ndipo mkutano wote wakajibu, wakasema, kwa sauti kuu, Kama ulivyosema katika habari yetu, ndivyo vitupasavyo kutenda. Ezra 10:12

Then all the assembly answered with a loud voice, As you have said concerning us, so must we do.

Lakini watu hawa ni wengi, tena ni wakati wa mvua nyingi, nasi hatuwezi kusimama nje, tena kazi hii si kazi ya siku moja, wala ya siku mbili; maana tumekosa sana katika jambo hili. Ezra 10:13

But the people are many, and it is a time of much rain, and we are not able to stand outside: neither is this a work of one day or two; for we have greatly transgressed in this matter.

Basi maakida wetu na wawekwe kwa ajili ya mkutano wote, na watu wote walio katika miji yetu, waliooa wanawake wageni, na waje nyakati zilizoamriwa, tena pamoja nao na waje wazee wa kila mji, na makadhi wa miji hiyo, hata ghadhabu kali ya Mungu wetu itakapotuondokea mbali, jambo hili likamalizike. Ezra 10:14

Let now our princes be appointed for all the assembly, and let all those who are in our cities who have married foreign women come at appointed times, and with them the elders of every city, and the judges of it, until the fierce wrath of our God be turned from us, until this matter be dispatched.

Yonathani, mwana wa Asaheli, na Yazeya, mwana wa Tikwa, hawa peke yao ndio waliosimama kulipinga neno hilo; na Meshulamu, na Shabethai Mlawi, wakawasaidia. Ezra 10:15

Only Jonathan the son of Asahel and Jahzeiah the son of Tikvah stood up against this [matter]: and Meshullam and Shabbethai the Levite helped them.

Basi wana wa uhamisho wakafanya hivyo. Na Ezra, kuhani, akatengwa, pamoja na baadhi ya wakuu wa mbari za mababa, kwa hesabu ya mbari ya baba zao; na hao wote kwa majina yao. Wakaketi siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, ili kulichunguza jambo hilo. Ezra 10:16

The children of the captivity did so. Ezra the priest, [with] certain heads of fathers' [houses], after their fathers' houses, and all of them by their names, were set apart; and they sat down in the first day of the tenth month to examine the matter.

Wakamaliza mambo ya wanaume wote, waliokuwa wameoa wanawake wageni, siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza. Ezra 10:17

They made an end with all the men who had married foreign women by the first day of the first month.

Basi, miongoni mwa makuhani walionekana wengine waliokuwa wameoa wanawake wageni; wa wana wa Yoshua, mwana wa Yosadaki, na nduguze; Maaseya, na Eliezeri, na Yaribu, na Gedalia. Ezra 10:18

Among the sons of the priests there were found who had married foreign women: [namely], of the sons of Jeshua, the son of Jozadak, and his brothers, Maaseiah, and Eliezer, and Jarib, and Gedaliah.

Nao wakatoa ahadi ya kwamba wataachana na wake zao; na kwa kuwa walikuwa na hatia, wakatoa kondoo mume kwa hatia yao. Ezra 10:19

They gave their hand that they would put away their wives; and being guilty, [they offered] a ram of the flock for their guilt.

Na wa wana wa Imeri; Hanani, na Zebadia. Ezra 10:20

Of the sons of Immer: Hanani and Zebadiah.

Na wa wana wa Harimu; Maaseya, na Eliya, na Shemaya, na Yehieli, na Uzia. Ezra 10:21

Of the sons of Harim: Maaseiah, and Elijah, and Shemaiah, and Jehiel, and Uzziah.

Na wa wana wa Pashuri; Elioenai, na Maaseya, na Ishmaeli, na Nethaneli, na Yozabadi, na Elasa. Ezra 10:22

Of the sons of Pashhur: Elioenai, Maaseiah, Ishmael, Nethanel, Jozabad, and Elasah.

Na wa Walawi; Yozabadi, na Shimei, na Kelaya (ndiye Kelita), na Pethahia, na Yuda, na Eliezeri. Ezra 10:23

Of the Levites: Jozabad, and Shimei, and Kelaiah (the same is Kelita), Pethahiah, Judah, and Eliezer.

Na wa waimbaji; Eliashibu. Na wa mabawabu; Shalumu, na Telemu, na Uri. Ezra 10:24

Of the singers: Eliashib. Of the porters: Shallum, and Telem, and Uri.

Na wa Israeli; wa wana wa Paroshi; Ramia, na Izia, na Malkiya, na Miyamini, na Eleazari, na Malkiya, na Benaya. Ezra 10:25

Of Israel: Of the sons of Parosh: Ramiah, and Izziah, and Malchijah, and Mijamin, and Eleazar, and Malchijah, and Benaiah.

Na wa wana wa Elamu; Matania, na Zekaria, na Yehieli, na Abdi, na Yeremothi, na Eliya. Ezra 10:26

Of the sons of Elam: Mattaniah, Zechariah, and Jehiel, and Abdi, and Jeremoth, and Elijah.

Na wa wana wa Zatu; Elioenai, na Eliashibu, na Matania, na Yeremothi, na Zabadi, na Aziza. Ezra 10:27

Of the sons of Zattu: Elioenai, Eliashib, Mattaniah, and Jeremoth, and Zabad, and Aziza.

Na wa wana wa Bebai; Yehohanani, na Hanania, na Zakai, na Athlai. Ezra 10:28

Of the sons of Bebai: Jehohanan, Hananiah, Zabbai, Athlai.

Na wa wana wa Bani; Meshulamu, na Maluki, na Adaya, na Yashubu, na Sheali, na Yeremothi. Ezra 10:29

Of the sons of Bani: Meshullam, Malluch, and Adaiah, Jashub, and Sheal, Jeremoth.

Na wa wana wa Pahath-Moabu; Adna, na Kelali, na Benaya, na Maaseya, na Matania, na Besaleli, na Binui, na Manase. Ezra 10:30

Of the sons of Pahath-moab: Adna, and Chelal, Benaiah, Maaseiah, Mattaniah, Bezalel, and Binnui, and Manasseh.

Na wa wana wa Harimu; Eliezeri, na Ishiya, na Malkiya, na Shemaya, na Shimeoni, Ezra 10:31

[of] the sons of Harim: Eliezer, Isshijah, Malchijah, Shemaiah, Shimeon,

na Benyamini, na Maluki, na Shemaria. Ezra 10:32

Benjamin, Malluch, Shemariah.

Na wa wana wa Hashumu; Matenai, na Matata, na Zabadi, na Elifeleti, na Yeremai, na Manase, na Shimei. Ezra 10:33

Of the sons of Hashum: Mattenai, Mattattah, Zabad, Eliphelet, Jeremai, Manasseh, Shimei.

Na wa wana wa Bani; Maadai, na Amramu, na Ueli, Ezra 10:34

Of the sons of Bani: Maadai, Amram, and Uel,

na Benaya, na Bedeya, na Keluhi, Ezra 10:35

Benaiah, Bedeiah, Cheluhi,

na Wania, na Meremothi, na Eliashibu, Ezra 10:36

Vaniah, Meremoth, Eliashib,

na Matania, na Matenai, na Yaasu. Ezra 10:37

Mattaniah, Mattenai, and Jaasu,

Na wa wana wa Binui; Shimei, Ezra 10:38

and Bani, and Binnui, Shimei,

na Shelemia, na Nathani, na Adaya, Ezra 10:39

and Shelemiah, and Nathan, and Adaiah,

na Maknadebai, na Shashai, na Sharai, Ezra 10:40

Machnadebai, Shashai, Sharai,

na Azareli, na Shelemia, na Shemaria, Ezra 10:41

Azarel, and Shelemiah, Shemariah,

na Shalumu, na Amaria, na Yusufu. Ezra 10:42

Shallum, Amariah, Joseph.

Na wa wana wa Nebo; Yeieli, na Matithia, na Zabadi, na Zebina, na Ido, na Yoeli, na Benaya. Ezra 10:43

Of the sons of Nebo: Jeiel, Mattithiah, Zabad, Zebina, Iddo, and Joel, Benaiah.

Hao wote walikuwa wameoa wanawake wageni; na wake zao wengine walikuwa wamezaa watoto. Ezra 10:44

All these had taken foreign wives; and some of them had wives by whom they had children.