Ezra 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ezra 3 (Swahili) Ezra 3 (English)

Hata ulipowadia mwezi wa saba, na wana wa Israeli walipokuwa katika miji yao, watu wakakusanyika pamoja huko Yerusalemu kama mtu mmoja. Ezra 3:1

When the seventh month was come, and the children of Israel were in the cities, the people gathered themselves together as one man to Jerusalem.

Ndipo akasimama Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zake makuhani, na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na ndugu zake, nao wakaijenga madhabahu ya Mungu wa Israeli, ili kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, mtu wa Mungu. Ezra 3:2

Then stood up Jeshua the son of Jozadak, and his brothers the priests, and Zerubbabel the son of Shealtiel, and his brothers, and built the altar of the God of Israel, to offer burnt offerings thereon, as it is written in the law of Moses the man of God.

Wakaiweka madhabahu juu ya msingi wake; maana hofu imewashika kwa sababu ya watu wa nchi; wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu yake, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni. Ezra 3:3

They set the altar on its base; for fear was on them because of the peoples of the countries: and they offered burnt offerings thereon to Yahweh, even burnt offerings morning and evening.

Wakaishika Sikukuu ya Vibanda, kama ilivyoandikwa, wakatoa sadaka za kuteketezwa za kila siku kwa hesabu yake, kama ilivyoagizwa, kama ilivyopasa kila siku; Ezra 3:4

They kept the feast of tents, as it is written, and [offered] the daily burnt offerings by number, according to the ordinance, as the duty of every day required;

na baadaye sadaka ya kuteketezwa ya daima, na za mwandamo wa mwezi, na za sikukuu za Bwana, zilizoamriwa na kuwekwa wakfu, na za kila mtu aliyemtolea Bwana sadaka kwa hiari yake. Ezra 3:5

and afterward the continual burnt-offering, and [the offerings] of the new moons, and of all the set feasts of Yahweh that were consecrated, and of everyone who willingly offered a freewill-offering to Yahweh.

Tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba walianza kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa, lakini msingi wa hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa bado. Ezra 3:6

From the first day of the seventh month began they to offer burnt offerings to Yahweh: but the foundation of the temple of Yahweh was not yet laid.

Tena waliwapa waashi na maseremala fedha; wakawapa watu wa Sidoni, na watu wa Tiro, chakula, na vinywaji, na mafuta, ili walete mierezi kutoka Lebanoni mpaka Yafa kwa njia ya bahari, kwa kadiri walivyopewa ruhusa na Koreshi, mfalme wa Uajemi. Ezra 3:7

They gave money also to the masons, and to the carpenters; and food, and drink, and oil, to them of Sidon, and to them of Tyre, to bring cedar trees from Lebanon to the sea, to Joppa, according to the grant that they had of Cyrus king of Persia.

Hata mwaka wa pili wa kufika kwao nyumbani kwa Mungu, huko Yerusalemu, mwezi wa pili, Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zao wengine, makuhani na Walawi, na watu wote, waliotoka katika uhamisho na kufika Yerusalemu, wakaanza; nao wakawaweka Walawi, hao wenye miaka ishirini na waliozidi, ili kuisimamia kazi ya nyumba ya Bwana. Ezra 3:8

Now in the second year of their coming to the house of God at Jerusalem, in the second month, began Zerubbabel the son of Shealtiel, and Jeshua the son of Jozadak, and the rest of their brothers the priests and the Levites, and all those who were come out of the captivity to Jerusalem, and appointed the Levites, from twenty years old and upward, to have the oversight of the work of the house of Yahweh.

Ndipo wakasimama Yeshua, na wanawe na ndugu zake, Kadmieli, na wanawe, wana wa Hodavia, pamoja, ili kuwasimamia hao wafanyao kazi katika nyumba ya Mungu; wana wa Henadadi, pamoja na wana wao, na ndugu zao, Walawi. Ezra 3:9

Then stood Jeshua with his sons and his brothers, Kadmiel and his sons, the sons of Judah, together, to have the oversight of the workmen in the house of God: the sons of Henadad, with their sons and their brothers the Levites.

Hata wajenzi walipouweka msingi wa hekalu la Bwana, wakawaweka makuhani, wamevaa mavazi yao, wenye baragumu, na Walawi, wana wa Asafu, wenye matoazi, ili wamhimidi Bwana, kama alivyoagiza Daudi, mfalme wa Israeli. Ezra 3:10

When the builders laid the foundation of the temple of Yahweh, they set the priests in their clothing with trumpets, and the Levites the sons of Asaph with cymbals, to praise Yahweh, after the order of David king of Israel.

Wakaimbiana, wakimhimidi Bwana, na kumshukuru, wakasema, Kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake kwa Israeli ni za milele. Kisha watu wote wakapaza sauti zao, na kupiga kelele, walipomhimidi Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana umekwisha kuwekwa. Ezra 3:11

They sang one to another in praising and giving thanks to Yahweh, [saying], For he is good, for his loving kindness endures forever toward Israel. All the people shouted with a great shout, when they praised Yahweh, because the foundation of the house of Yahweh was laid.

Bali makuhani wengi, na Walawi, na wakuu wa mbari za mababa, waliokuwa wameiona nyumba ya kwanza, wakati msingi wa nyumba hii ulipowekwa mbele ya macho yao, walilia kwa sauti kuu; na watu wengi walipiga kelele za furaha; Ezra 3:12

But many of the priests and Levites and heads of fathers' [houses], the old men who had seen the first house, when the foundation of this house was laid before their eyes, wept with a loud voice; and many shouted aloud for joy:

hata watu wasiweze kupambanua kelele za furaha, na kelele za vilio vya watu; maana watu walipiga kelele kwa sauti kuu, na kelele zao zikasikilikana mbali sana. Ezra 3:13

so that the people could not discern the noise of the shout of joy from the noise of the weeping of the people; for the people shouted with a loud shout, and the noise was heard afar off.