Hosea 13

Hosea Chapter 13

Download Audio (Pakua)
« Orodha ya Sura
English Translation
1
Efraimu aliponena, palikuwa na tetemeko; alijitukuza katika Israeli; Lakini alipokosa katika Baali, alikufa.
When Ephraim spoke, there was trembling. He exalted himself in Israel, But when he became guilty in Baal, he died.
2
Na sasa wanazidi kufanya dhambi, nao wamejifanyizia sanamu kwa fedha yao, naam, sanamu kwa kadiri ya akili zao; zote pia ni kazi ya mafundi; nao huzitaja hivi, Wanaume watoao dhabihu na wazibusu ndama.
Now they sin more and more, And have made themselves molten images of their silver, Even idols according to their own understanding, All of them the work of the craftsmen. They say of them, "They offer human sacrifice and kiss the calves."
3
Kwa sababu hiyo watakuwa kama wingu la asubuhi, na kama umande utowekao upesi, kama makapi yaliyopeperushwa na tufani sakafuni, na kama moshi utokao katika bomba.
Therefore they will be like the morning cloud, And like the dew that passes away early, Like the chaff that is driven with the whirlwind out of the threshing floor, And like the smoke out of the chimney.
4
Lakini mimi ni Bwana, Mungu wako tangu nchi ya Misri; wala hutamjua mungu mwingine ila mimi; wala zaidi ya mimi hakuna Mwokozi.
"Yet I am Yahweh your God from the land of Egypt; And you will know no god but me, And besides me there is no savior.
5
Mimi nalikujua katika jangwa, katika nchi yenye kiu nyingi.
I knew you in the wilderness, In the land of great drought.
6
Kwa kadiri ya malisho yao, kwa kadiri iyo hiyo walishiba; walishiba na moyo wao ukatukuka; ndiyo sababu wamenisahau mimi.
According to their pasture, so were they filled; They were filled, and their heart was exalted. Therefore they have forgotten me.
7
Basi nimekuwa kama simba kwao; kama chui nitavizia njiani;
Therefore am I to them like a lion; Like a leopard I will lurk by the path.
8
nitakutana nao kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake; nami nitararua nyama ya mioyo yao; na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.
I will meet them like a bear that is bereaved of her cubs, And will tear the covering of their heart. And there I will devour them like a lioness. The wild animal will tear them.
9
Haya ndiyo maangamizo yako, Ee Israeli, ya kuwa wewe u kinyume changu mimi, kinyume cha msaada wako.
You are destroyed, Israel, because you are against me, Against your help.
10
Yuko wapi sasa mfalme wako, apate kukuokoa katika miji yako yote? Na hao waamuzi wako, uliowanena hivi, Nipe mfalme na wakuu?
Where is your king now, that he may save you in all your cities? And your judges, of whom you said, 'Give me a king and princes?'
11
Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu.
I have given you a king in my anger, And have taken him away in my wrath.
12
Uovu wa Efraimu umefungwa kwa kukazwa; dhambi yake imewekwa akiba.
The guilt of Ephraim is stored up. His sin is stored up.
13
Utungu wa mwanamke mwenye mimba utampata; yeye ni mwana asiye na akili; maana wakati umewadia, ambao haimpasi kukawia mahali wapenyapo watoto.
The sorrows of a travailing woman will come on him. He is an unwise son; For when it is time, he doesn't come to the opening of the womb.
14
Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? Ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako? Kujuta kutafichwa na macho yangu.
I will ransom them from the power of Sheol. I will redeem them from death! Death, where are your plagues? Sheol, where is your destruction? Compassion will be hidden from my eyes.
15
Ajapokuwa yeye ni mwenye kuzaa sana kati ya ndugu zake, upepo wa mashariki utakuja, hiyo pumzi ya Bwana itokayo upande wa nyikani, na kijito chake cha maji kitakauka, na chemchemi yake itakaushwa; yeye atateka nyara hazina ya vyombo vyote vipendezavyo.
Though he is fruitful among his brothers, an east wind will come, The breath of Yahweh coming up from the wilderness; And his spring will become dry, And his fountain will be dried up. He will plunder the storehouse of treasure.
16
Samaria atachukua hatia yake; kwa maana amemwasi Mungu wake; wataanguka kwa upanga; watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande, na wanawake wao wenye mimba watatambuliwa.
Samaria will bear her guilt; For she has rebelled against her God. They will fall by the sword. Their infants will be dashed in pieces, And their pregnant women will be ripped open."
« 12 14 »

Chagua Sura Nyingine (Select Chapter)