Ni tabibu wa karibu; tabibu wa ajabu;
na rehema za daima; ni dawa yake njema.
Imbeni, malaika, sifa za Yesu Bwana;
pweke limetukuka jina lake Yesu.
Hatufai kuwa hai, wala hatutumai,
ila yeye kweli ndiye atupumzishaye.
Imbeni, malaika, sifa za Yesu Bwana;
pweke limetukuka jina lake Yesu.
Dhambi pia na hatia ametuchukulia;
Twenendeni na amani hata kwake mbinguni.
Huliona tamu jina, la Yesu kristo Bwana,
yuna sifa mwenye kufa asishindwe na kufa.
Kila mume asimame, sifa zake zivume;
Wanawake na washike kusifu jina lake.
Na vijana wote tena, wampendao sana,
waje kwake wawe wake kwa utumishi wake.
Write a review/comment/correct the lyrics of Ni Tabibu Wa Karibu - Imbeni Malaika Sifa Kwa Yesu Bwana:
Tumsifu na kumwabudu Bwana Yesu daima...maana yeye pekee ndiye anastahili 1 year ago
sifa ziko sawa 1 year ago
Siku zote tuimbe sifa zake mwokozi yesu kwani hilo ndilo jina imara na dhabiti 1 year ago
ongezeni lyrisc za wasanii wa injili kama wakina joel lwaga,godluck gozbert,angel benard n.k ITAWASAIDIA KIBIASHARA
BY
#djvegas 1 year ago
A Very Nice Song With More Blessings. 1 year ago
I'm so blessed thank you 2 years ago
Very blessing songs 3 years ago