Sylvia Akoth - Ni Wewe Worship Medley Lyrics
Lyrics
Mungu wangu ni wewe, Jehovah ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana) Mwenye enzi yote na utukufu ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana)
Mwenye nguvu zote, heshima yote ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana) Mwenye enzi yote nakuinulia macho yangu (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana)
Eeh baba niseme nini mbele zako Wema wako niulinganishe na nini bwana Umekuwa kimbilio maishani mwangu Umekuwa tegemeo maishani mwangu
Mali niliyo nayo ni juu ya neema yako Umbali nimefika ni juu ya neema yako Ingekuwa mwanadamu singestahili lolote Ingekuwa mwanadamu singepata chochote
Ni juu yako tuu niko jinsi nilivyo Ni juu yako tu niko hapa leo Eeh Yesu we Yesu we, nani kama wewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana) Alpha na Omega aliyekuwa, atakayekuwa ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana)
Ulinipenda ukaniokoa kwa damu yako (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana) Kila goti lipigwe, kila ulimi ukiri ni weewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana)
Yesu ni wewe, Baba ni wewe
Uliyeniiita na kunikomboa ni wewe Uliyeniiita na kunikomboa ni wewe Niseme nini mbele zako bwana wangu Wewe ndiwe utaoye katikati ya mavumbi
Tena ni wewe uniketishaye na wakuu Ni wewe Mungu wangu ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana) Dawa ya miguu yangu baba ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana)
Uliyenihesabia haki baba ni wewe, ni wewe baba (Ni wewe Bwana ni wewe, ni wewe Bwana)
Sitambui mwingine sijui mwingine, baba ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe Bwana) Wokovu wangu uzima wangu baba ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe Bwana)
Nisipo, kimbilia wewe ni nani mwingine Nisipo, mtazamia wewe ni nani mwingine Vizazi hata vizazi vyakufamu wewe Dunia yote yakufahamu wewe
Ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe Bwana) Kimbilio langu mwamba wangu ni wewe Baba ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe Bwana)
Mungu wa majira yote Hakuna likushindalo kamwe (Ni wewe Bwana ni wewe Bwana) Uliye na haki ya uzima ni wewe, ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe Bwana)
Mungu wa milele, Mungu wa ushindi ni wewe (Ni wewe Bwana ni wewe Bwana) Ni wewe ni wewe Yahweh
Dunia yote iko mabegani mwako Wewe ni nguvu yangu Yesu Umeinuliwa juu Ufalme wako ni wa juu yesu Umejawa na ukweli na haki Hakuna kama wewe
Bila wewe Yesu wee, siwezi Bila uwepo wako, siwezi Bila nguvu zako kwangu, siwezi Nimetambua bila wewe, siwezi
Baba bila bila uzima wako mi siwezi Baba bila kusema nami baba, siwezi Naamini nitakuwa mgeni wa nani bila, siwezi Naamini ni nani anayenipenda mimi bwana, siwezi
Hakuna aliye aliye aliye Hakuna aliye kama wewe Mungu wangu Hakuna aliye aliye aliye Hakuna aliye kama wewe Mungu wangu
Hakuna aliyenifia msalabani Hakuna aliyeniokoa kama wewe Hakuna aliyelipia gharama Hakuna aliyenipenda kama wewe Hakuna aliyee, aliye aliye kama wewe
Kwake Jehovah tumesimama leo Ndiye mwamba ni salama Ndiye mwamba ni salama Ndiye mwamba ni Yesu
Kwake Yahweh tumesimama leo Ndiye mwamba ni salama Ndiye mwamba ni salama Ndiye mwamba ni Yesu
Kwake Messiah tumesimama leo Ndiye mwamba ni salama Ndiye mwamba ni salama Ndiye mwamba ni Yesu
Aliyeniumba ni yeye Bwana wangu Ndiye mwamba ni Yesu Aliyeniita, Ndiye mwamba ni Yesu Aliyenikubali ni yeye bwana Ndiye mwamba ni Yesu
Ndiye mwamba, ndiye mwamba Ndiye mwamba ni Yesu Ndiye mwamba, ndiye mwamba Ndiye mwamba ni Yesu
Ndiye mwamba, ndiye mwamba Ndiye mwamba ni Yesu Ndiye mwamba, ndiye mwamba Ndiye mwamba ni Yesu
Video
Ni Wewe Worship Medley - Sylvia Akoth ft. Ali Mukhwana