Yakobo 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yakobo 3 (Swahili) James 3 (English)

Ndugu zangu, msiwe waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi. Yakobo 3:1

Let not many of you be teachers, my brothers, knowing that we will receive heavier judgment.

Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu. Yakobo 3:2

For in many things we all stumble. If anyone doesn't stumble in word, the same is a perfect man, able to bridle the whole body also.

Angalieni, twatia lijamu katika vinywa vya farasi, ili wamtii, hivi twageuza mwili wao wote. Yakobo 3:3

Indeed, we put bits into the horses' mouths so that they may obey us, and we guide their whole body.

Tena angalieni merikebu; ingawa ni kubwa kama nini, na kuchukuliwa na pepo kali, zageuzwa na usukani mdogo sana, ko kote anakoazimia kwenda nahodha. Yakobo 3:4

Behold, the ships also, though they are so big and are driven by fierce winds, are yet guided by a very small rudder, wherever the pilot desires.

Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. Yakobo 3:5

So the tongue is also a little member, and boasts great things. See how a small fire can spread to a large forest!

Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum. Yakobo 3:6

And the tongue is a fire. The world of iniquity among our members is the tongue, which defiles the whole body, and sets on fire the course of nature, and is set on fire by Gehenna.{Gehenna is a name that describes a burning Hell with rotting bodies and unclean things in it}

Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu. Yakobo 3:7

For every kind of animal, bird, creeping thing, and thing in the sea, is tamed, and has been tamed by mankind.

Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti. Yakobo 3:8

But nobody can tame the tongue. It is a restless evil, full of deadly poison.

Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu. Yakobo 3:9

With it we bless our God and Father, and with it we curse men, who are made in the image of God.

Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Yakobo 3:10

Out of the same mouth comes forth blessing and cursing. My brothers, these things ought not to be so.

Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? Yakobo 3:11

Does a spring send out from the same opening fresh and bitter water?

Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu. Yakobo 3:12

Can a fig tree, my brothers, yield olives, or a vine figs? Thus no spring yields both salt water and fresh water.

N'nani aliye na hekima na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole wa hekima. Yakobo 3:13

Who is wise and understanding among you? Let him show by his good conduct that his deeds are done in gentleness of wisdom.

Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. Yakobo 3:14

But if you have bitter jealousy and selfish ambition in your heart, don't boast and don't lie against the truth.

Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. Yakobo 3:15

This wisdom is not that which comes down from above, but is earthly, sensual, and demonic.

Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. Yakobo 3:16

For where jealousy and selfish ambition are, there is confusion and every evil deed.

Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki. Yakobo 3:17

But the wisdom that is from above is first pure, then peaceful, gentle, reasonable, full of mercy and good fruits, without partiality, and without hypocrisy.

Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani. Yakobo 3:18

Now the fruit of righteousness is sown in peace by those who make peace.