Yakobo 3 Swahili & English
Listen/Download AudioYakobo 3 (Swahili) | James 3 (English) |
---|---|
Ndugu zangu, msiwe waalimu wengi, mkijua ya kuwa mtapata hukumu kubwa zaidi. Yakobo 3:1 |
Let not many of you be teachers, my brothers, knowing that we will receive heavier judgment. |
Maana twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu. Yakobo 3:2 |
For in many things we all stumble. If anyone doesn't stumble in word, the same is a perfect man, able to bridle the whole body also. |
Angalieni, twatia lijamu katika vinywa vya farasi, ili wamtii, hivi twageuza mwili wao wote. Yakobo 3:3 |
Indeed, we put bits into the horses' mouths so that they may obey us, and we guide their whole body. |
Tena angalieni merikebu; ingawa ni kubwa kama nini, na kuchukuliwa na pepo kali, zageuzwa na usukani mdogo sana, ko kote anakoazimia kwenda nahodha. Yakobo 3:4 |
Behold, the ships also, though they are so big and are driven by fierce winds, are yet guided by a very small rudder, wherever the pilot desires. |
Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. Yakobo 3:5 |
So the tongue is also a little member, and boasts great things. See how a small fire can spread to a large forest! |
Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum. Yakobo 3:6 |
And the tongue is a fire. The world of iniquity among our members is the tongue, which defiles the whole body, and sets on fire the course of nature, and is set on fire by Gehenna.{Gehenna is a name that describes a burning Hell with rotting bodies and unclean things in it} |
Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu. Yakobo 3:7 |
For every kind of animal, bird, creeping thing, and thing in the sea, is tamed, and has been tamed by mankind. |
Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti. Yakobo 3:8 |
But nobody can tame the tongue. It is a restless evil, full of deadly poison. |
Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu. Yakobo 3:9 |
With it we bless our God and Father, and with it we curse men, who are made in the image of God. |
Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Yakobo 3:10 |
Out of the same mouth comes forth blessing and cursing. My brothers, these things ought not to be so. |
Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? Yakobo 3:11 |
Does a spring send out from the same opening fresh and bitter water? |
Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu. Yakobo 3:12 |
Can a fig tree, my brothers, yield olives, or a vine figs? Thus no spring yields both salt water and fresh water. |
N'nani aliye na hekima na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole wa hekima. Yakobo 3:13 |
Who is wise and understanding among you? Let him show by his good conduct that his deeds are done in gentleness of wisdom. |
Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. Yakobo 3:14 |
But if you have bitter jealousy and selfish ambition in your heart, don't boast and don't lie against the truth. |
Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. Yakobo 3:15 |
This wisdom is not that which comes down from above, but is earthly, sensual, and demonic. |
Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. Yakobo 3:16 |
For where jealousy and selfish ambition are, there is confusion and every evil deed. |
Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki. Yakobo 3:17 |
But the wisdom that is from above is first pure, then peaceful, gentle, reasonable, full of mercy and good fruits, without partiality, and without hypocrisy. |
Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani. Yakobo 3:18 |
Now the fruit of righteousness is sown in peace by those who make peace. |