Yakobo 2 Swahili & English
Listen/Download AudioYakobo 2 (Swahili) | James 2 (English) |
---|---|
Ndugu zangu, imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe nayo kwa kupendelea watu. Yakobo 2:1 |
My brothers, don't hold the faith of our Lord Jesus Christ of glory with partiality. |
Maana akiingia katika sinagogi lenu mtu mwenye pete ya dhahabu na mavazi mazuri; kisha akiingia na maskini, mwenye mavazi mabovu; Yakobo 2:2 |
For if a man with a gold ring, in fine clothing, comes into your assembly, and a poor man in filthy clothing also comes in; |
nanyi mkimstahi yule aliyevaa mavazi mazuri, na kumwambia, Keti wewe hapa mahali pazuri; na kumwambia yule maskini, Simama wewe pale, au keti miguuni pangu, Yakobo 2:3 |
and you pay special attention to him who wears the fine clothing, and say, "Sit here in a good place;" and you tell the poor man, "Stand there," or "Sit by my footstool;" |
je! Hamkufanya hitilafu mioyoni mwenu, mkawa waamuzi wenye mawazo mabovu? Yakobo 2:4 |
haven't you shown partiality among yourselves, and become judges with evil thoughts? |
Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao? Yakobo 2:5 |
Listen, my beloved brothers. Didn't God choose those who are poor in this world to be rich in faith, and heirs of the Kingdom which he promised to those who love him? |
Bali ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je! Matajiri hawawaonei ninyi na kuwavuta mbele ya viti vya hukumu? Yakobo 2:6 |
But you have dishonored the poor man. Don't the rich oppress you, and personally drag you before the courts? |
Hawalitukani jina lile zuri mliloitwa? Yakobo 2:7 |
Don't they blaspheme the honorable name by which you are called? |
Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema. Yakobo 2:8 |
However, if you fulfill the royal law, according to the Scripture, "You shall love your neighbor as yourself," you do well. |
Bali mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji. Yakobo 2:9 |
But if you show partiality, you commit sin, being convicted by the law as transgressors. |
Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. Yakobo 2:10 |
For whoever shall keep the whole law, and yet stumble in one point, he has become guilty of all. |
Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. Yakobo 2:11 |
For he who said, "Do not commit adultery," said also, "Do not commit murder." Now if you do not commit adultery, but murder, you have become a transgressor of the law. |
Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru. Yakobo 2:12 |
So speak, and so do, as men who are to be judged by a law of freedom. |
Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu. Yakobo 2:13 |
For judgment is without mercy to him who has shown no mercy. Mercy triumphs over judgment. |
Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa? Yakobo 2:14 |
What good is it, my brothers, if a man says he has faith, but has no works? Can faith save him? |
Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki, Yakobo 2:15 |
And if a brother or sister is naked and in lack of daily food, |
na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini? Yakobo 2:16 |
and one of you tells them, "Go in peace, be warmed and filled;" and yet you didn't give them the things the body needs, what good is it? |
Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake. Yakobo 2:17 |
Even so faith, if it has no works, is dead in itself. |
Lakini mtu atasema, Wewe unayo imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu. Yakobo 2:18 |
Yes, a man will say, "You have faith, and I have works." Show me your faith from your works, and I by my works will show you my faith. |
Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. Yakobo 2:19 |
You believe that God is one. You do well. The demons also believe, and shudder. |
Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai? Yakobo 2:20 |
But do you want to know, vain man, that faith apart from works is dead? |
Je! Baba yetu Ibrahimu hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipomtoa Isaka mwanawe juu ya madhabahu? Yakobo 2:21 |
Wasn't Abraham our father justified by works, in that he offered up Isaac his son on the altar? |
Waona kwamba imani ilitenda kazi pamoja na matendo yake, na ya kwamba imani ile ilikamilishwa kwa njia ya matendo yale. Yakobo 2:22 |
You see that faith worked with his works, and by works faith was perfected; |
Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu. Yakobo 2:23 |
and the Scripture was fulfilled which says, "Abraham believed God, and it was accounted to him as righteousness;" and he was called the friend of God. |
Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. Yakobo 2:24 |
You see then that by works, a man is justified, and not only by faith. |
Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine? Yakobo 2:25 |
In like manner wasn't Rahab the prostitute also justified by works, in that she received the messengers, and sent them out another way? |
Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa. Yakobo 2:26 |
For as the body apart from the spirit is dead, even so faith apart from works is dead. |