Yakobo 2 Swahili & English

Listen/Download Audio
Yakobo 2 (Swahili) James 2 (English)

Ndugu zangu, imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe nayo kwa kupendelea watu. Yakobo 2:1

My brothers, don't hold the faith of our Lord Jesus Christ of glory with partiality.

Maana akiingia katika sinagogi lenu mtu mwenye pete ya dhahabu na mavazi mazuri; kisha akiingia na maskini, mwenye mavazi mabovu; Yakobo 2:2

For if a man with a gold ring, in fine clothing, comes into your assembly, and a poor man in filthy clothing also comes in;

nanyi mkimstahi yule aliyevaa mavazi mazuri, na kumwambia, Keti wewe hapa mahali pazuri; na kumwambia yule maskini, Simama wewe pale, au keti miguuni pangu, Yakobo 2:3

and you pay special attention to him who wears the fine clothing, and say, "Sit here in a good place;" and you tell the poor man, "Stand there," or "Sit by my footstool;"

je! Hamkufanya hitilafu mioyoni mwenu, mkawa waamuzi wenye mawazo mabovu? Yakobo 2:4

haven't you shown partiality among yourselves, and become judges with evil thoughts?

Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao? Yakobo 2:5

Listen, my beloved brothers. Didn't God choose those who are poor in this world to be rich in faith, and heirs of the Kingdom which he promised to those who love him?

Bali ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je! Matajiri hawawaonei ninyi na kuwavuta mbele ya viti vya hukumu? Yakobo 2:6

But you have dishonored the poor man. Don't the rich oppress you, and personally drag you before the courts?

Hawalitukani jina lile zuri mliloitwa? Yakobo 2:7

Don't they blaspheme the honorable name by which you are called?

Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema. Yakobo 2:8

However, if you fulfill the royal law, according to the Scripture, "You shall love your neighbor as yourself," you do well.

Bali mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji. Yakobo 2:9

But if you show partiality, you commit sin, being convicted by the law as transgressors.

Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. Yakobo 2:10

For whoever shall keep the whole law, and yet stumble in one point, he has become guilty of all.

Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. Yakobo 2:11

For he who said, "Do not commit adultery," said also, "Do not commit murder." Now if you do not commit adultery, but murder, you have become a transgressor of the law.

Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru. Yakobo 2:12

So speak, and so do, as men who are to be judged by a law of freedom.

Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu. Yakobo 2:13

For judgment is without mercy to him who has shown no mercy. Mercy triumphs over judgment.

Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa? Yakobo 2:14

What good is it, my brothers, if a man says he has faith, but has no works? Can faith save him?

Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki, Yakobo 2:15

And if a brother or sister is naked and in lack of daily food,

na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini? Yakobo 2:16

and one of you tells them, "Go in peace, be warmed and filled;" and yet you didn't give them the things the body needs, what good is it?

Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake. Yakobo 2:17

Even so faith, if it has no works, is dead in itself.

Lakini mtu atasema, Wewe unayo imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu. Yakobo 2:18

Yes, a man will say, "You have faith, and I have works." Show me your faith from your works, and I by my works will show you my faith.

Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. Yakobo 2:19

You believe that God is one. You do well. The demons also believe, and shudder.

Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai? Yakobo 2:20

But do you want to know, vain man, that faith apart from works is dead?

Je! Baba yetu Ibrahimu hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipomtoa Isaka mwanawe juu ya madhabahu? Yakobo 2:21

Wasn't Abraham our father justified by works, in that he offered up Isaac his son on the altar?

Waona kwamba imani ilitenda kazi pamoja na matendo yake, na ya kwamba imani ile ilikamilishwa kwa njia ya matendo yale. Yakobo 2:22

You see that faith worked with his works, and by works faith was perfected;

Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu. Yakobo 2:23

and the Scripture was fulfilled which says, "Abraham believed God, and it was accounted to him as righteousness;" and he was called the friend of God.

Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. Yakobo 2:24

You see then that by works, a man is justified, and not only by faith.

Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine? Yakobo 2:25

In like manner wasn't Rahab the prostitute also justified by works, in that she received the messengers, and sent them out another way?

Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa. Yakobo 2:26

For as the body apart from the spirit is dead, even so faith apart from works is dead.