Hosea 7 Swahili & English
Listen/Download AudioHosea 7 (Swahili) | Hosea 7 (English) |
---|---|
Wakati nitakapo kumponya Israeli, ndipo yafunuliwapo maovu ya Efraimu, na ubaya wa Samaria; maana wanatenda uongo, na mwivi huvunja nyumba za watu, na kundi la wanyang'anyi hushambulia nje. Hosea 7:1 |
When I would heal Israel, Then the iniquity of Ephraim is uncovered, Also the wickedness of Samaria; For they commit falsehood, And the thief enters in, And the gang of robbers ravages outside. |
Wala hawafikiri mioyoni mwao ya kwamba naukumbuka uovu wao wote; sasa matendo yao wenyewe yamewazunguka pande zote; yako mbele za uso wangu. Hosea 7:2 |
They don't consider in their hearts that I remember all their wickedness. Now their own deeds have engulfed them. They are before my face. |
Humfurahisha mfalme kwa uovu wao, na wakuu wao kwa uongo wao. Hosea 7:3 |
They make the king glad with their wickedness, And the princes with their lies. |
Hao wote ni wazinzi; wamekuwa kama tanuu iliyotiwa moto na mwokaji; huacha kuuchochea moto, tangu kuukanda unga hata umekwisha kutiwa chachu. Hosea 7:4 |
They are all adulterers. They are burning like an oven that the baker stops stirring, From the kneading of the dough, until it is leavened. |
Sikukuu ya mfalme wetu, wakuu walijitapisha kwa ukali wa divai; alinyosha mkono wake pamoja na wenye mzaha. Hosea 7:5 |
On the day of our king, the princes made themselves sick with the heat of wine. He joined his hand with mockers. |
Maana wamefanya moyo wao kuwa tayari kama tanuu, wakati waoteapo; hasira yao hulala usiku kucha; asubuhi yawaka kama moto utoao miali. Hosea 7:6 |
For they have made ready their heart like an oven, While they lie in wait. Their baker sleeps all the night. In the morning it burns as a flaming fire. |
Wote wamepata moto kama tanuu, nao hula makadhi wao; wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao aniitaye mimi. Hosea 7:7 |
They are all hot as an oven, And devour their judges. All their kings have fallen. There is no one among them who calls to me. |
Efraimu ajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate usiogeuzwa. Hosea 7:8 |
Ephraim, he mixes himself among the nations. Ephraim is a pancake not turned over. |
Wageni wamekula nguvu zake, naye hana habari; naam, nywele za mvi zimeonekana huko na huko juu yake, naye hana habari. Hosea 7:9 |
Strangers have devoured his strength, And he doesn't realize it. Indeed, gray hairs are here and there on him, And he doesn't realize it. |
Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; ila hata hivyo hawakumrudia Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta kwa ajili ya hayo yote. Hosea 7:10 |
The pride of Israel testifies to his face; Yet they haven't returned to Yahweh their God, Nor sought him, for all this. |
Naye Efraimu amekuwa kama njiwa mpumbavu, asiye na fahamu; humwita Misri, huenda Ashuru. Hosea 7:11 |
"Ephraim is like an easily deceived dove, without understanding. They call to Egypt. They go to Assyria. |
Watakapokwenda nitatandika wavu wangu juu yao; nitawashusha kama ndege wa angani; nitawarudi, kama vile mkutano wao ulivyosikia. Hosea 7:12 |
When they go, I will spread my net on them. I will bring them down like the birds of the sky. I will chastise them, as their congregation has heard. |
Ole wao! Kwa kuwa wamenikimbia; uharibifu na uwapate! Kwa kuwa wameniasi; ingawa ninataka kuwakomboa, hata hivyo wamenena uongo juu yangu. Hosea 7:13 |
Woe to them! For they have wandered from me. Destruction to them! For they have trespassed against me. Though I would redeem them, Yet they have spoken lies against me. |
Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi. Hosea 7:14 |
They haven't cried to me with their heart, But they howl on their beds. They assemble themselves for grain and new wine. They turn away from me. |
Ingawa nimewafundisha na kuwatia nguvu mikono yao, hata hivyo hukusudia udhalimu juu yangu. Hosea 7:15 |
Though I have taught and strengthened their arms, Yet they plot evil against me. |
Wao hurudi, lakini si kwake Aliye juu; wamekuwa kama upinde usiotumainika; wakuu wao wataanguka kwa upanga, kwa sababu ya jeuri ya ndimi zao; jambo hili litakuwa kwao sababu ya kuchekwa katika nchi ya Misri. Hosea 7:16 |
They return, but not to the Most High. They are like a faulty bow. Their princes will fall by the sword for the rage of their tongue. This will be their derision in the land of Egypt. |