Hosea 7 Swahili & English

Listen/Download Audio
Hosea 7 (Swahili) Hosea 7 (English)

Wakati nitakapo kumponya Israeli, ndipo yafunuliwapo maovu ya Efraimu, na ubaya wa Samaria; maana wanatenda uongo, na mwivi huvunja nyumba za watu, na kundi la wanyang'anyi hushambulia nje. Hosea 7:1

When I would heal Israel, Then the iniquity of Ephraim is uncovered, Also the wickedness of Samaria; For they commit falsehood, And the thief enters in, And the gang of robbers ravages outside.

Wala hawafikiri mioyoni mwao ya kwamba naukumbuka uovu wao wote; sasa matendo yao wenyewe yamewazunguka pande zote; yako mbele za uso wangu. Hosea 7:2

They don't consider in their hearts that I remember all their wickedness. Now their own deeds have engulfed them. They are before my face.

Humfurahisha mfalme kwa uovu wao, na wakuu wao kwa uongo wao. Hosea 7:3

They make the king glad with their wickedness, And the princes with their lies.

Hao wote ni wazinzi; wamekuwa kama tanuu iliyotiwa moto na mwokaji; huacha kuuchochea moto, tangu kuukanda unga hata umekwisha kutiwa chachu. Hosea 7:4

They are all adulterers. They are burning like an oven that the baker stops stirring, From the kneading of the dough, until it is leavened.

Sikukuu ya mfalme wetu, wakuu walijitapisha kwa ukali wa divai; alinyosha mkono wake pamoja na wenye mzaha. Hosea 7:5

On the day of our king, the princes made themselves sick with the heat of wine. He joined his hand with mockers.

Maana wamefanya moyo wao kuwa tayari kama tanuu, wakati waoteapo; hasira yao hulala usiku kucha; asubuhi yawaka kama moto utoao miali. Hosea 7:6

For they have made ready their heart like an oven, While they lie in wait. Their baker sleeps all the night. In the morning it burns as a flaming fire.

Wote wamepata moto kama tanuu, nao hula makadhi wao; wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao aniitaye mimi. Hosea 7:7

They are all hot as an oven, And devour their judges. All their kings have fallen. There is no one among them who calls to me.

Efraimu ajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate usiogeuzwa. Hosea 7:8

Ephraim, he mixes himself among the nations. Ephraim is a pancake not turned over.

Wageni wamekula nguvu zake, naye hana habari; naam, nywele za mvi zimeonekana huko na huko juu yake, naye hana habari. Hosea 7:9

Strangers have devoured his strength, And he doesn't realize it. Indeed, gray hairs are here and there on him, And he doesn't realize it.

Na kiburi cha Israeli chamshuhudia mbele ya uso wake; ila hata hivyo hawakumrudia Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta kwa ajili ya hayo yote. Hosea 7:10

The pride of Israel testifies to his face; Yet they haven't returned to Yahweh their God, Nor sought him, for all this.

Naye Efraimu amekuwa kama njiwa mpumbavu, asiye na fahamu; humwita Misri, huenda Ashuru. Hosea 7:11

"Ephraim is like an easily deceived dove, without understanding. They call to Egypt. They go to Assyria.

Watakapokwenda nitatandika wavu wangu juu yao; nitawashusha kama ndege wa angani; nitawarudi, kama vile mkutano wao ulivyosikia. Hosea 7:12

When they go, I will spread my net on them. I will bring them down like the birds of the sky. I will chastise them, as their congregation has heard.

Ole wao! Kwa kuwa wamenikimbia; uharibifu na uwapate! Kwa kuwa wameniasi; ingawa ninataka kuwakomboa, hata hivyo wamenena uongo juu yangu. Hosea 7:13

Woe to them! For they have wandered from me. Destruction to them! For they have trespassed against me. Though I would redeem them, Yet they have spoken lies against me.

Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi. Hosea 7:14

They haven't cried to me with their heart, But they howl on their beds. They assemble themselves for grain and new wine. They turn away from me.

Ingawa nimewafundisha na kuwatia nguvu mikono yao, hata hivyo hukusudia udhalimu juu yangu. Hosea 7:15

Though I have taught and strengthened their arms, Yet they plot evil against me.

Wao hurudi, lakini si kwake Aliye juu; wamekuwa kama upinde usiotumainika; wakuu wao wataanguka kwa upanga, kwa sababu ya jeuri ya ndimi zao; jambo hili litakuwa kwao sababu ya kuchekwa katika nchi ya Misri. Hosea 7:16

They return, but not to the Most High. They are like a faulty bow. Their princes will fall by the sword for the rage of their tongue. This will be their derision in the land of Egypt.