Tito BSB

Tito 2

Titus Chapter 2

1
Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima;
But as for you, speak the things that are consistent with sound doctrine.
2
ya kwamba wazee wawe wenye kiasi, wastahivu, wenye busara, wazima katika imani na katika upendo na katika saburi.
Older men are to be temperate, dignified, self-controlled, and sound in faith, love, and perseverance.
3
Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema;
Older women, likewise, are to be reverent in their behavior, not slanderers or addicted to much wine, but teachers of good.
4
ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;
In this way they can train the young women to love their husbands and children,
5
na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.
to be self-controlled, pure, managers of their households, kind, and submissive to their own husbands, so that the word of God will not be discredited.
6
Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi;
In the same way, urge the younger men to be self-controlled.
7
katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu,
In everything, show yourself to be an example by doing good works. In your teaching show integrity, dignity,
8
na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.
and wholesome speech that is above reproach, so that anyone who opposes us will be ashamed, having nothing bad to say about us.
9
Watumwa na wawatii bwana zao, wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu,
Slaves are to submit to their own masters in everything, to be well-pleasing, not argumentative,
10
wasiwe waibaji; bali wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.
not stealing from them, but showing all good faith, so that in every respect they will adorn the teaching about God our Savior.
11
Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;
For the grace of God has appeared, bringing salvation to everyone.
12
nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;
It instructs us to renounce ungodliness and worldly passions, and to live sensible, upright, and godly lives in the present age,
13
tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;
as we await the blessed hope and glorious appearance of our great God and Savior Jesus Christ.
14
ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.
He gave Himself for us to redeem us from all lawlessness and to purify for Himself a people for His own possession, zealous for good deeds.
15
Nena maneno hayo, onya na kukaripia kwa mamlaka yote; asikudharau mtu awaye yote.
Speak these things as you encourage and rebuke with all authority. Let no one despise you.

Chagua Sura

1 2 3