Tito 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
Tito 3 (Swahili) Titus 3 (English)

Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; Tito 3:1

Remind them to be in subjection to rulers and to authorities, to be obedient, to be ready for every good work,

wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote. Tito 3:2

to speak evil of no one, not to be contentious, to be gentle, showing all humility toward all men.

Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana. Tito 3:3

For we were also once foolish, disobedient, deceived, serving various lusts and pleasures, living in malice and envy, hateful, and hating one another.

Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa; Tito 3:4

But when the kindness of God our Savior and his love toward mankind appeared,

si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; Tito 3:5

not by works of righteousness, which we did ourselves, but according to his mercy, he saved us, through the washing of regeneration and renewing by the Holy Spirit,

ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu; Tito 3:6

which he poured out on us richly, through Jesus Christ our Savior;

ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu. Tito 3:7

that, being justified by his grace, we might be made heirs according to the hope of eternal life.

Ni neno la kuaminiwa; na mambo hayo nataka uyanene kwa nguvu, ili wale waliomwamini Mungu wakumbuke kudumu katika matendo mema. Hayo ni mazuri, tena yana faida kwa wanadamu. Tito 3:8

This saying is faithful, and concerning these things I desire that you affirm confidently, so that those who have believed God may be careful to maintain good works. These things are good and profitable to men;

Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana. Tito 3:9

but shun foolish questionings, genealogies, strife, and disputes about the law; for they are unprofitable and vain.

Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae; Tito 3:10

Avoid a factious man after a first and second warning;

ukijua ya kuwa mtu kama huyo amepotoka, tena atenda dhambi, maana amejihukumu hatia yeye mwenyewe. Tito 3:11

knowing that such a one is perverted, and sins, being self-condemned.

Wakati nitakapomtuma Artema kwako au Tikiko, jitahidi kuja kwangu huku Nikopoli; kwa maana huku nimekusudia kukaa wakati wa baridi. Tito 3:12

When I send Artemas to you, or Tychicus, be diligent to come to me to Nicopolis, for I have determined to winter there.

Zena, yule mwana-sheria, na Apolo, uwasafirishe kwa bidii, wasipungukiwe na cho chote. Tito 3:13

Send Zenas, the lawyer, and Apollos on their journey speedily, that nothing may be lacking for them.

Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda. Tito 3:14

Let our people also learn to maintain good works for necessary uses, that they may not be unfruitful.

Watu wote walio pamoja nami wakusalimu. Tusalimie wale watupendao katika imani. Neema na iwe pamoja nanyi nyote. Tito 3:15

All who are with me greet you. Greet those who love us in faith. Grace be with you all. Amen.