Tito 3 Swahili & English
Listen/Download AudioTito 3 (Swahili) | Titus 3 (English) |
---|---|
Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; Tito 3:1 |
Remind them to be in subjection to rulers and to authorities, to be obedient, to be ready for every good work, |
wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote. Tito 3:2 |
to speak evil of no one, not to be contentious, to be gentle, showing all humility toward all men. |
Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana. Tito 3:3 |
For we were also once foolish, disobedient, deceived, serving various lusts and pleasures, living in malice and envy, hateful, and hating one another. |
Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa; Tito 3:4 |
But when the kindness of God our Savior and his love toward mankind appeared, |
si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; Tito 3:5 |
not by works of righteousness, which we did ourselves, but according to his mercy, he saved us, through the washing of regeneration and renewing by the Holy Spirit, |
ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu; Tito 3:6 |
which he poured out on us richly, through Jesus Christ our Savior; |
ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu. Tito 3:7 |
that, being justified by his grace, we might be made heirs according to the hope of eternal life. |
Ni neno la kuaminiwa; na mambo hayo nataka uyanene kwa nguvu, ili wale waliomwamini Mungu wakumbuke kudumu katika matendo mema. Hayo ni mazuri, tena yana faida kwa wanadamu. Tito 3:8 |
This saying is faithful, and concerning these things I desire that you affirm confidently, so that those who have believed God may be careful to maintain good works. These things are good and profitable to men; |
Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana. Tito 3:9 |
but shun foolish questionings, genealogies, strife, and disputes about the law; for they are unprofitable and vain. |
Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae; Tito 3:10 |
Avoid a factious man after a first and second warning; |
ukijua ya kuwa mtu kama huyo amepotoka, tena atenda dhambi, maana amejihukumu hatia yeye mwenyewe. Tito 3:11 |
knowing that such a one is perverted, and sins, being self-condemned. |
Wakati nitakapomtuma Artema kwako au Tikiko, jitahidi kuja kwangu huku Nikopoli; kwa maana huku nimekusudia kukaa wakati wa baridi. Tito 3:12 |
When I send Artemas to you, or Tychicus, be diligent to come to me to Nicopolis, for I have determined to winter there. |
Zena, yule mwana-sheria, na Apolo, uwasafirishe kwa bidii, wasipungukiwe na cho chote. Tito 3:13 |
Send Zenas, the lawyer, and Apollos on their journey speedily, that nothing may be lacking for them. |
Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda. Tito 3:14 |
Let our people also learn to maintain good works for necessary uses, that they may not be unfruitful. |
Watu wote walio pamoja nami wakusalimu. Tusalimie wale watupendao katika imani. Neema na iwe pamoja nanyi nyote. Tito 3:15 |
All who are with me greet you. Greet those who love us in faith. Grace be with you all. Amen. |