Wimbo Ulio Bora 6 Swahili & English

Listen/Download Audio
Wimbo Ulio Bora 6 (Swahili) Song Of Songs 6 (English)

Mpendwa wako amekwenda wapi, Wewe uliye mzuri katika wanawake? Mpendwa wako amegeukia upande upi, Ili tumtafute pamoja nawe? Wimbo Ulio Bora 6:1

Where has your beloved gone, you fairest among women? Where has your beloved turned, that we may seek him with you? Beloved

Mpendwa wangu ameshukia bustani yake, Kwenye matuta ya rihani; Ili kulisha penye bustani, Ili kuchuma nyinyoro. Wimbo Ulio Bora 6:2

My beloved has gone down to his garden, To the beds of spices, To feed in the gardens, and to gather lilies.

Mimi ni wake mpendwa wangu, naye ni wangu, Hulisha kundi lake penye nyinyoro. Wimbo Ulio Bora 6:3

I am my beloved's, and my beloved is mine. He browses among the lilies,

Mpenzi wangu, u mzuri kama Tirza, Mwenye kupendeza kama Yerusalemu, Wa kutisha kama wenye bendera. Wimbo Ulio Bora 6:4

You are beautiful, my love, as Tirzah, Lovely as Jerusalem, Awesome as an army with banners.

Uyageuzie macho yako mbali nami, Kwa maana yamenitisha sana. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi, Wakijilaza mbavuni pa Gileadi. Wimbo Ulio Bora 6:5

Turn away your eyes from me, For they have overcome me. Your hair is like a flock of goats, That lie along the side of Gilead.

Meno yako kama kundi la kondoo, Wakipanda kutoka kuoshwa; Ambao kila mmoja amezaa mapacha, Wala hakuna aliyefiwa kati yao. Wimbo Ulio Bora 6:6

Your teeth are like a flock of ewes, Which have come up from the washing; Of which every one has twins; None is bereaved among them.

Mashavu yako ni kama kipande cha komamanga, Nyuma ya barakoa yako. Wimbo Ulio Bora 6:7

Your temples are like a piece of a pomegranate behind your veil.

Wako malkia sitini, na masuria themanini, Na wanawali wasiohesabika; Wimbo Ulio Bora 6:8

There are sixty queens, eighty concubines, And virgins without number.

Hua wangu, mkamilifu wangu, ni mmoja tu, Mtoto wa pekee wa mamaye. Ndiye kipenzi chake aliyemzaa, Binti wakamwona wakamwita heri; Malkia na masuria nao wakamwona, Wakamsifu, wakisema, Wimbo Ulio Bora 6:9

My dove, my perfect one, is unique. She is her mother's only daughter. She is the favorite one of her who bore her. The daughters saw her, and called her blessed, The queens and the concubines, and they praised her.

Ni nani huyu atazamaye kama alfajiri, Mzuri kama mwezi, safi kama jua, Wa kutisha kama wenye bendera? Wimbo Ulio Bora 6:10

Who is she who looks forth as the morning, Beautiful as the moon, Clear as the sun, Awesome as an army with banners?

Nalishukia bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua. Wimbo Ulio Bora 6:11

I went down into the nut tree grove, To see the green plants of the valley, To see whether the vine budded, And the pomegranates were in flower.

Kabla sijajua, roho yangu ilinileta Katikati ya magari ya wakuu wangu. Wimbo Ulio Bora 6:12

Without realizing it, My desire set me with my royal people's chariots. Friends

Rudi, rudi, Mshulami, Rudi, rudi, ili sisi tukutazame. Wimbo Ulio Bora 6:13

Return, return, Shulammite! Return, return, that we may gaze at you. Lover Why do you desire to gaze at the Shulammite, As at the dance of Mahanaim?