2 Petro 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Petro 3 (Swahili) 2nd Peter 3 (English)

Wapenzi, waraka huu ndio wa pili niwaandikiao ninyi; katika zote mbili naziamsha nia zenu safi kwa kuwakumbusha, 2 Petro 3:1

This is now, beloved, the second letter that I have written to you; and in both of them I stir up your sincere mind by reminding you;

mpate kuyakumbuka yale maneno yaliyonenwa zamani na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume wenu. 2 Petro 3:2

that you should remember the words which were spoken before by the holy prophets, and the commandments of us, the apostles of the Lord and Savior:

Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe, 2 Petro 3:3

knowing this first, that in the last days mockers will come, walking after their own lusts,

na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa. 2 Petro 3:4

and saying, "Where is the promise of his coming? For, from the day that the fathers fell asleep, all things continue as they were from the beginning of the creation."

Maana hufumba macho yao wasione neno hili ya kuwa zilikuwako mbingu tangu zamani, na nchi pia, imefanyizwa kutoka katika maji, na ndani ya maji, kwa neno la Mungu; 2 Petro 3:5

For this they willfully forget, that there were heavens from of old, and an earth formed out of water and amid water, by the word of God;

kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia. 2 Petro 3:6

by which means the world that then was, being overflowed with water, perished.

Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu. 2 Petro 3:7

But the heavens that now are, and the earth, by the same word have been stored up for fire, being reserved against the day of judgment and destruction of ungodly men.

Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja. 2 Petro 3:8

But don't forget this one thing, beloved, that one day is with the Lord as a thousand years, and a thousand years as one day.

Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. 2 Petro 3:9

The Lord is not slow concerning his promise, as some count slowness; but is patient with us, not wishing that any should perish, but that all should come to repentance.

Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 2 Petro 3:10

But the day of the Lord will come as a thief in the night; in which the heavens will pass away with a great noise, and the elements will be dissolved with fervent heat, and the earth and the works that are in it will be burned up.

Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 2 Petro 3:11

Therefore since all these things are thus to be destroyed, what manner of persons ought you to be in holy living and godliness,

mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? 2 Petro 3:12

looking for and earnestly desiring the coming of the day of God, by reason of which the heavens being on fire will be dissolved, and the elements will melt with fervent heat?

Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. 2 Petro 3:13

But, according to his promise, we look for new heavens and a new earth, in which dwells righteousness.

Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake. 2 Petro 3:14

Therefore, beloved, seeing that you look for these things, be diligent to be found in peace, without blemish and blameless in his sight.

Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa; 2 Petro 3:15

Regard the patience of our Lord as salvation; even as our beloved brother Paul also, according to the wisdom given to him, wrote to you;

vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe. 2 Petro 3:16

as also in all of his letters, speaking in them of these things. In those are some things hard to be understood, which the ignorant and unsettled twist, as they also do to the other Scriptures, to their own destruction.

Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. 2 Petro 3:17

You therefore, beloved, knowing these things beforehand, beware lest, being carried away with the error of the wicked, you fall from your own steadfastness.

Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele. 2 Petro 3:18

But grow in the grace and knowledge of our Lord and Savior Jesus Christ. To him be the glory both now and forever. Amen.