2 Petro 2 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Petro 2 (Swahili) 2nd Peter 2 (English)

Lakini kuliondokea manabii wa uongo katika wale watu, kama vile kwenu kutakavyokuwako waalimu wa uongo, watakaoingiza kwa werevu uzushi wa kupoteza, wakimkana hata Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usiokawia. 2 Petro 2:1

But there also arose false prophets among the people, as among you also there will be false teachers, who will secretly bring in destructive heresies, denying even the Master who bought them, bringing on themselves swift destruction.

Na wengi watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa. 2 Petro 2:2

Many will follow their immoral{TR reads "destructive" instead of "immoral"} ways, and as a result, the way of the truth will be maligned.

Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii. 2 Petro 2:3

In covetousness they will exploit you with deceptive words: whose sentence now from of old doesn't linger, and their destruction will not slumber.

Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu; 2 Petro 2:4

For if God didn't spare angels when they sinned, but cast them down to Tartarus{Tartarus is another name for Hell}, and committed them to pits of darkness, to be reserved to judgment;

wala hakuuachilia ulimwengu wa kale, bali alimhifadhi Nuhu, mjumbe wa haki, na watu wengine saba, hapo alipoleta Gharika juu ya ulimwengu wa wasiomcha Mungu; 2 Petro 2:5

and didn't spare the ancient world, but preserved Noah with seven others, a preacher of righteousness, when he brought a flood on the world of the ungodly;

tena akaihukumu miji ya Sodoma na Gomora, akiipindua na kuifanya majivu, akaifanya iwe ishara kwa watu watakaokuwa hawamchi Mungu baada ya haya; 2 Petro 2:6

and turning the cities of Sodom and Gomorrah into ashes, condemned them to destruction, having made them an example to those who would live ungodly;

akamwokoa Lutu, yule mwenye haki aliyehuzunishwa sana na mwenendo wa ufisadi wa hao wahalifu; 2 Petro 2:7

and delivered righteous Lot, who was very distressed by the lustful life of the wicked

maana mtu huyu mwenye haki akikaa kati yao, kwa kuona na kusikia, alijitesa roho yake yenye haki, siku baada ya siku, kwa matendo yao yasiyo na sheria; 2 Petro 2:8

(for that righteous man dwelling among them, was tormented in his righteous soul from day to day with seeing and hearing lawless deeds):

basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu; 2 Petro 2:9

the Lord knows how to deliver the godly out of temptation and to keep the unrighteous under punishment for the day of judgment;

na hasa wale waufuatao mwili katika tamaa ya mambo machafu. na kudharau mamlaka. 2 Petro 2:10

but chiefly those who walk after the flesh in the lust of defilement, and despise authority. Daring, self-willed, they are not afraid to speak evil of dignitaries;

Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; ijapokuwa malaika ambao ni wakuu zaidi kwa uwezo na nguvu, hawaleti mashitaka mabaya juu yao mbele za Bwana. 2 Petro 2:11

whereas angels, though greater in might and power, don't bring a railing judgment against them before the Lord.

Lakini hao kama wanyama wasio na akili, ambao walizaliwa kama wanyama tu wa kukamatwa na kupotezwa, wakikufuru katika mambo wasiyoyajua, wataangamizwa katika maangamizo yao; 2 Petro 2:12

But these, as unreasoning creatures, born natural animals to be taken and destroyed, speaking evil in matters about which they are ignorant, will in their destroying surely be destroyed,

Wakipatikana na madhara, ambayo ni ujira wa udhalimu wao, wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa; wamekuwa ni mawaa na aibu wakifuata anasa zisizo kiasi katika karamu zao za upendo, wafanyapo karamu pamoja nanyi; 2 Petro 2:13

receiving the wages of unrighteousness; people who count it pleasure to revel in the day-time, spots and blemishes, reveling in their deceit while they feast with you;

wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana; 2 Petro 2:14

having eyes full of adultery, and who can't cease from sin; enticing unsettled souls; having a heart trained in greed; children of cursing;

wakiiacha njia iliyonyoka, wakapotea, wakiifuata njia ya Balaamu, mwana wa Beori, aliyependa ujira wa udhalimu; 2 Petro 2:15

forsaking the right way, they went astray, having followed the way of Balaam the son of Beor, who loved the wages of wrong-doing;

lakini alikaripiwa kwa uhalifu wake mwenyewe; punda, asiyeweza kusema, akinena kwa sauti ya kibinadamu, aliuzuia wazimu wa nabii yule. 2 Petro 2:16

but he was rebuked for his own disobedience. A mute donkey spoke with man's voice and stopped the madness of the prophet.

Hawa ni visima visivyo na maji, na mawingu yachukuliwayo na tufani, ambao weusi wa giza ni akiba waliyowekewa. 2 Petro 2:17

These are wells without water, clouds driven by a storm; for whom the blackness of darkness has been reserved forever.

Maana wakinena maneno makuu mno ya kiburi, kwa tamaa za mwili na kwa ufisadi huwahadaa watu walioanza kuwakimbia wale wanaoenenda katika udanganyifu; 2 Petro 2:18

For, uttering great swelling words of emptiness, they entice in the lusts of the flesh, by licentiousness, those who are indeed escaping from those who live in error;

wakiwaahidia uhuru, nao wenyewe ni watumwa wa uharibifu, maana mtu akishindwa na mtu huwa mtumwa wa mtu yule. 2 Petro 2:19

promising them liberty, while they themselves are bondservants of corruption; for by whom a man is overcome, by the same is he also brought into bondage.

Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza. 2 Petro 2:20

For if, after they have escaped the defilement of the world through the knowledge of the Lord and Savior Jesus Christ, they are again entangled therein and overcome, the last state has become worse with them than the first.

Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa. 2 Petro 2:21

For it would be better for them not to have known the way of righteousness, than, after knowing it, to turn back from the holy commandment delivered to them.

Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni. 2 Petro 2:22

But it has happened to them according to the true proverb, "The dog turns to his own vomit again," and "the sow that had washed to wallowing in the mire."