2 Petro 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Petro 1 (Swahili) 2nd Peter 1 (English)

Simoni Petro, mtumwa na mtume wa Yesu Kristo, kwa wale waliopata imani moja na sisi, yenye thamani, katika hali ya Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo. 2 Petro 1:1

Simon Peter, a servant and apostle of Jesus Christ, to those who have obtained a like precious faith with us in the righteousness of our God and Savior, Jesus Christ:

Neema na iwe kwenu na amani iongezwe katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu. 2 Petro 1:2

Grace to you and peace be multiplied in the knowledge of God and of Jesus our Lord,

Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. 2 Petro 1:3

seeing that his divine power has granted to us all things that pertain to life and godliness, through the knowledge of him who called us by his own glory and virtue;

Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa. 2 Petro 1:4

by which he has granted to us his precious and exceedingly great promises; that through these you may become partakers of the divine nature, having escaped from the corruption that is in the world by lust.

Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa, 2 Petro 1:5

Yes, and for this very cause adding on your part all diligence, in your faith supply moral excellence; and in moral excellence, knowledge;

na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa, 2 Petro 1:6

and in knowledge, self-control; and in self-control patience; and in patience godliness;

na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo. 2 Petro 1:7

and in godliness brotherly affection; and in brotherly affection, love.

Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo. 2 Petro 1:8

For if these things are yours and abound, they make you to be not idle nor unfruitful to the knowledge of our Lord Jesus Christ.

Maana yeye asiyekuwa na hayo ni kipofu, hawezi kuona vitu vilivyo mbali, amesahau kule kutakaswa dhambi zake za zamani. 2 Petro 1:9

For he who lacks these things is blind, seeing only what is near, having forgotten the cleansing from his old sins.

Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe. 2 Petro 1:10

Therefore, brothers,{The word for "brothers" here and where context allows may also be correctly translated "brothers and sisters" or "siblings."} be more diligent to make your calling and election sure. For if you do these things, you will never stumble.

Maana hivi mtaruzukiwa kwa ukarimu kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana wetu, Mwokozi wetu Yesu Kristo. 2 Petro 1:11

For thus will be richly supplied to you the entrance into the eternal Kingdom of our Lord and Savior, Jesus Christ.

Kwa hiyo nitakuwa tayari kuwakumbusha hayo siku zote, ijapokuwa mnayajua na kuthibitishwa katika kweli mliyo nayo. 2 Petro 1:12

Therefore I will not be negligent to remind you of these things, though you know them, and are established in the present truth.

Nami naona ni haki, maadamu nipo mimi katika maskani hii, kuwaamsha kwa kuwakumbusha. 2 Petro 1:13

I think it right, as long as I am in this tent, to stir you up by reminding you;

Nikijua kwamba kule kuwekea mbali maskani yangu kwaja upesi, kama Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha. 2 Petro 1:14

knowing that the putting off of my tent comes swiftly, even as our Lord Jesus Christ made clear to me.

Walakini nitajitahidi, kwamba kila wakati baada ya kufariki kwangu mpate kuyakumbuka mambo hayo. 2 Petro 1:15

Yes, I will make every effort that you may always be able to remember these things even after my departure.

Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake. 2 Petro 1:16

For we did not follow cunningly devised fables, when we made known to you the power and coming of our Lord Jesus Christ, but we were eyewitnesses of his majesty.

Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. 2 Petro 1:17

For he received from God the Father honor and glory, when the voice came to him from the Majestic Glory, "This is my beloved Son, in whom I am well pleased."

Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu. 2 Petro 1:18

This voice we heard come out of heaven when we were with him in the holy mountain.

Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing'aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu. 2 Petro 1:19

We have the more sure word of prophecy; whereunto you do well that you take heed, as to a lamp shining in a dark place, until the day dawns, and the day star arises in your hearts:

Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. 2 Petro 1:20

knowing this first, that no prophecy of Scripture is of private interpretation.

Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. 2 Petro 1:21

For no prophecy ever came by the will of man: but holy men of God spoke, being moved by the Holy Spirit.