2 Wathesalonike BSB

2 Wathesalonike 2

2dThessalonians Chapter 2

1
Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake,
Now concerning the coming of our Lord Jesus Christ and our being gathered together to Him, we ask you, brothers,
2
kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo.
not to be easily disconcerted or alarmed by any spirit or message or letter seeming to be from us, alleging that the Day of the Lord has already come.
3
Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;
Let no one deceive you in any way, for it will not come until the rebellion occurs and the man of lawlessness—the son of destruction—is revealed.
4
yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.
He will oppose and exalt himself above every so-called god or object of worship. So he will seat himself in the temple of God, proclaiming himself to be God.
5
Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?
Do you not remember that I told you these things while I was still with you?
6
Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
And you know what is now restraining him, so that he may be revealed at the proper time.
7
Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.
For the mystery of lawlessness is already at work, but the one who now restrains it will continue until he is taken out of the way.
8
Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;
And then the lawless one will be revealed, whom the Lord Jesus will slay with the breath of His mouth and annihilate by the majesty of His arrival.
9
yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;
The coming of the lawless one will be accompanied by the working of Satan, with every kind of power, sign, and false wonder,
10
na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
and with every wicked deception directed against those who are perishing, because they refused the love of the truth that would have saved them.
11
Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
For this reason God will send them a powerful delusion so that they believe the lie,
12
ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.
in order that judgment may come upon all who have disbelieved the truth and delighted in wickedness.
13
Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu sikuzote kwa ajili yenu, ndugu mliopendwa na Bwana, kwa kuwa Mungu amewachagua tangu mwanzo mpate wokovu, katika kutakaswa na Roho, na kuiamini kweli;
But we should always thank God for you, brothers who are loved by the Lord, because God chose you from the beginning to be saved by the sanctification of the Spirit and by faith in the truth.
14
aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
To this He called you through our gospel, so that you may share in the glory of our Lord Jesus Christ.
15
Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu.
Therefore, brothers, stand firm and cling to the traditions we taught you, whether by speech or by letter.
16
Na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu, aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,
Now may our Lord Jesus Christ Himself and God our Father, who by grace has loved us and given us eternal comfort and good hope,
17
awafariji mioyo yenu, na kuwafanya imara katika kila neno na tendo jema.
encourage your hearts and strengthen you in every good word and deed.

Chagua Sura

1 2 3