1
Hatimaye, ndugu, tuombeeni, neno la Bwana liendelee, na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu;
Finally, brothers, pray for us, that the word of the Lord may spread quickly and be held in honor, just as it was with you.
2
tukaokolewe na watu wasio haki, wabaya; maana si wote walio na imani.
And pray that we may be delivered from wicked and evil men; for not everyone holds to the faith.
3
Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu.
But the Lord is faithful, and He will strengthen you and guard you from the evil one.
4
Nasi tumemtumaini Bwana kwa mambo yenu, kwamba mnayafanya tulivyowaagiza, tena kwamba mtayafanya.
And we have confidence in the Lord that you are doing and will continue to do what we command.
5
Bwana awaongoze mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na saburi ya Kristo.
May the Lord direct your hearts into God’s love and Christ’s perseverance.
6
Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu.
Now we command you, brothers, in the name of our Lord Jesus Christ, to keep away from any brother who leads an undisciplined life that is not in keeping with the tradition you received from us.
7
Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata; kwa sababu hatukuenda bila utaratibu kwenu;
For you yourselves know how you ought to imitate us, because we were not undisciplined among you,
8
wala hatukula chakula kwa mtu ye yote bure; bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili tusimlemee mtu wa kwenu awaye yote.
nor did we eat anyone’s food without paying for it. Instead, in labor and toil, we worked night and day so that we would not be a burden to any of you.
9
Si kwamba hatuna amri, lakini makusudi tufanye nafsi zetu kuwa kielelezo kwenu, mtufuate.
Not that we lack this right, but we wanted to offer ourselves as an example for you to imitate.
10
Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.
For even while we were with you, we gave you this command: “If anyone is unwilling to work, he shall not eat.”
11
Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine.
For we hear that some of you are leading undisciplined lives, accomplishing nothing, but being busybodies.
12
Basi twawaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe.
We command and urge such people by our Lord Jesus Christ to begin working quietly to earn their own living.
13
Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.
But as for you, brothers, do not grow weary in well-doing.
14
Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari;
Take note of anyone who does not obey the instructions we have given in this letter. Do not associate with him, so that he may be ashamed.
15
lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
Yet do not regard him as an enemy, but admonish him as a brother.
16
Sasa, Bwana wa amani mwenyewe na awape amani daima kwa njia zote. Bwana awe pamoja nanyi nyote.
Now may the Lord of peace Himself give you peace at all times and in every way. The Lord be with all of you.
17
Salamu zangu mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndiyo alama katika kila waraka, ndio mwandiko wangu.
This greeting is in my own hand—Paul. This is my mark in every letter; it is the way I write.
18
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi nyote.
The grace of our Lord Jesus Christ be with all of you.