2 Wathesalonike 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Wathesalonike 3 (Swahili) 2dThessalonians 3 (English)

Hatimaye, ndugu, tuombeeni, neno la Bwana liendelee, na kutukuzwa vile vile kama ilivyo kwenu; 2 Wathesalonike 3:1

Finally, brothers, pray for us, that the word of the Lord may spread rapidly and be glorified, even as also with you;

tukaokolewe na watu wasio haki, wabaya; maana si wote walio na imani. 2 Wathesalonike 3:2

and that we may be delivered from unreasonable and evil men; for not all have faith.

Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu. 2 Wathesalonike 3:3

But the Lord is faithful, who will establish you, and guard you from the evil one.

Nasi tumemtumaini Bwana kwa mambo yenu, kwamba mnayafanya tulivyowaagiza, tena kwamba mtayafanya. 2 Wathesalonike 3:4

We have confidence in the Lord concerning you, that you both do and will do the things we command.

Bwana awaongoze mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na saburi ya Kristo. 2 Wathesalonike 3:5

May the Lord direct your hearts into the love of God, and into the patience of Christ.

Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu. 2 Wathesalonike 3:6

Now we command you, brothers, in the name of our Lord Jesus Christ, that you withdraw yourselves from every brother who walks in rebellion, and not after the tradition which they received from us.

Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata; kwa sababu hatukuenda bila utaratibu kwenu; 2 Wathesalonike 3:7

For you know how you ought to imitate us. For we didn't behave ourselves rebelliously among you,

wala hatukula chakula kwa mtu ye yote bure; bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili tusimlemee mtu wa kwenu awaye yote. 2 Wathesalonike 3:8

neither did we eat bread from anyone's hand without paying for it, but in labor and travail worked night and day, that we might not burden any of you;

Si kwamba hatuna amri, lakini makusudi tufanye nafsi zetu kuwa kielelezo kwenu, mtufuate. 2 Wathesalonike 3:9

not because we don't have the right, but to make ourselves an example to you, that you should imitate us.

Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula. 2 Wathesalonike 3:10

For even when we were with you, we commanded you this: "If anyone will not work, neither let him eat."

Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine. 2 Wathesalonike 3:11

For we hear of some who walk among you in rebellion, who don't work at all, but are busybodies.

Basi twawaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe. 2 Wathesalonike 3:12

Now those who are that way, we command and exhort in the Lord Jesus Christ, that with quietness they work, and eat their own bread.

Lakini ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema. 2 Wathesalonike 3:13

But you, brothers, don't be weary in doing well.

Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari; 2 Wathesalonike 3:14

If any man doesn't obey our word in this letter, note that man, that you have no company with him, to the end that he may be ashamed.

lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu. 2 Wathesalonike 3:15

Don't count him as an enemy, but admonish him as a brother.

Sasa, Bwana wa amani mwenyewe na awape amani daima kwa njia zote. Bwana awe pamoja nanyi nyote. 2 Wathesalonike 3:16

Now may the Lord of peace himself give you peace at all times in all ways. The Lord be with you all.

Salamu zangu mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndiyo alama katika kila waraka, ndio mwandiko wangu. 2 Wathesalonike 3:17

The greeting of me, Paul, with my own hand, which is the sign in every letter: this is how I write.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi nyote. 2 Wathesalonike 3:18

The grace of our Lord Jesus Christ be with you all. Amen.