Lyrics
Verse 1
Msalabani pa mwokozi, hapo niliomba upozi,
akaniokoa mpenzi, mwana wa Mungu.
Chorus
Mwana wa Mungu, mwokozi wangu,
akaniokoa mpenzi, mwana wa Mungu
Verse 2
Chini ya mti msumbufu, niliomba utakatifu,
alinikomboa kwa damu, mwana wa Mungu.
Verse 3
Aliniokoa dhambini, ikawa kunikaa ndani,
aliponifia mtini, mwana wa Mungu.
Verse 4
Damu ya Yesu ya thamani, huniokoa makosani,
huniendesha wokovuni, mwana wa Mungu.
Verse 5
Hicho kijito cha gharama, leo jivike kwa kuzama,
kwake uuone uzima, mwana wa Mungu.
Credits & Song Information
Video
Meaning & Inspiration
Katika rekodi hii, Daudi Petro anaimba Tenzi za Rohoni Na. 77 kama ushuhuda wa kumwelekea Mwokozi msalabani. Mistari inaunganisha ombi la uponyaji na utakatifu na shukrani kwa ukombozi, huku kiitikio kikisisitiza kwamba tumaini la mwimbaji limo kwa Mwana wa Mungu.