Martha Mwaipaja - Nashukuru Lyrics

Lyrics

Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu

Yesu, Yesu wangu, Yesu Machozi ya furaha yananitoka Machozi ya shangwe yananitoka Jana nililia machozi ya uchungu sana Jana nililia machozi ya mateso sana

Lakini leo nalia machozi ya furaha Leo natoa machozi ya furaha Mahali umenisaidia niseme nini? Mahali umenivusha niseme nini mimi?

Jana nilipiga magoti kwa ajili ya maombi Leo napiga goti langu baba ninakushukuru Jana niliomba sana haaa Na leo ninakushukuru sana haaa Umbali umenileta wewe ni Ebenezer kwangu Umbali umenileta wewe ni Bwana wa mimi

Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu

[Boaz K] Nilipopita kwenye bonde ulikuwa nami Nilipopita kwenye bonde ulikuwa nami Safari ilipokuwa ndefu ulikuwa nami Safari ilipokuwa ndefu ulikuwa nami

Kila dua niliyopiga ulikuwa nami Kila dua niliyopiga ulikuwa nami Asante Yesu, Asante Mungu Mi nashukuru kwa neema yako

Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu

[Boaz K] Umekuwa mwema kwangu niseme nini Umekuwa msaada kwangu niseme nini? Uinuliwe Jehovah upewe sifa Wengi walishasema eti mimi siwezi Wengi walishasema eti mimi siwezi Kwa neema zako, kwa neema

Mimi sijui ulinitoaje Kwnye lile shimo (Yesu) Sijui ulininasua vipi Kwenye mtego (Yesu)

[Martha Mwaipaja] Nimejikuta tu niko salama aha Nimejikuta tu mimi nimepona Hata nikiulizwa kwa nini nimeinuliwa Wakiniuliza mbona Martha umeinuliwa Sina hata cha kusema nimejikuta niko hivi Yesu umenishangaza (Yesu)

Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu Nakushukuru Mungu, nakushukuru Mungu Asante Yesu, Asante Yesu

Video

NASHUKURU BY BOAZ K Ft MARTHA MWAIPA (Official Video) skiza code 7639272

Thumbnail for Nashukuru video
Loading...
In Queue
View Lyrics