Sifa Lyrics

Nisaidie by Fred Msungu cover art

Fred Msungu - Nisaidie Lyrics

Artist:
Fred Msungu

Lyrics

Mateso yakizidi hofu hutawala 


Hakuna tumaini lini yatakwisha 


Imani yatoweka hakuna tumaini 


Mungu wangu nisaidie 


Hakuna hata moja aniwazia mema 


Adui wamezidi rafiki wageuka 


Sioni hata moja wakunisaidia 


Baba wee Mungu wangu nisaidie 


Ninapoonewa ninapolemewa 


Giza likitanda nuru zikiisha 


Mungu wangu nisaidie 


Mungu nakungoja wewe 


Nipe nguvu mpya 


Nivuke kama tai 


Nitembee bila kuchoka 


Nipige mbio mbele bila kuzimia 


Mungu wangu nisaidie 


Nimeshajinyonyoa manyoya 


Nimeparua kwa mbali 


Nimepunguza uzito kwa bidii 


Niko tayari kuruka tena 


Maisha yangu ya pili nzuri 


Kulinganisha na yale ya kwanza 


Niko tayari ninazo nguvu kama tai 


Ujana wangu umerejea 


Maisha yangu yamerejea 


Sasa niko na nguvu 


Sioni wii tena haleluya 


Ninapoonewa ninapolemewa 


Giza likitanda nuru zikiisha 


Mungu wangu nisaidie 


Nisaidie nisaidie 


Nisaidie nisaidie 


Wale wangojao watapata nguvu mpya 


Watapaa juu kwa mbali kama tai 


Ninapoonewa ninapolemewa 


Giza likitanda nuru zikiisha 


Mungu wangu nisaidie 


Mungu wangu nisaidie 


Ninapoonewa ninapolemewa 


Giza likitanda nuru zikiisha 


Mungu wangu nisaidie 


Video