Fred Msungu - Nisaidie Lyrics

Nisaidie Lyrics

Mateso yakizidi hofu hutawala 
Hakuna tumaini lini yatakwisha 
Imani yatoweka hakuna tumaini 
Mungu wangu nisaidie 

Hakuna hata moja aniwazia mema 
Adui wamezidi rafiki wageuka 
Sioni hata moja wakunisaidia 
Baba wee Mungu wangu nisaidie 

Ninapoonewa ninapolemewa 
Giza likitanda nuru zikiisha 
Mungu wangu nisaidie 

Mungu nakungoja wewe 
Nipe nguvu mpya 
Nivuke kama tai 
Nitembee bila kuchoka 
Nipige mbio mbele bila kuzimia 
Mungu wangu nisaidie 

Nimeshajinyonyoa manyoya 
Nimeparua kwa mbali 
Nimepunguza uzito kwa bidii 
Niko tayari kuruka tena 
Maisha yangu ya pili nzuri 
Kulinganisha na yale ya kwanza 
Niko tayari ninazo nguvu kama tai 
Ujana wangu umerejea 
Maisha yangu yamerejea 
Sasa niko na nguvu 
Sioni wii tena haleluya 

Ninapoonewa ninapolemewa 
Giza likitanda nuru zikiisha 
Mungu wangu nisaidie 

Nisaidie nisaidie 
Nisaidie nisaidie 

Wale wangojao watapata nguvu mpya 
Watapaa juu kwa mbali kama tai 

Ninapoonewa ninapolemewa 
Giza likitanda nuru zikiisha 
Mungu wangu nisaidie 
Mungu wangu nisaidie 

Ninapoonewa ninapolemewa 
Giza likitanda nuru zikiisha 
Mungu wangu nisaidie 


Nisaidie Video

Nisaidie Lyrics -  Fred Msungu

Fred Msungu Songs

Related Songs