Ruthu 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ruthu 4 (Swahili) Ruth 4 (English)

Basi Boazi akakwea kwenda mpaka langoni, akaketi pale; na tazama, yule mtu wa jamaa aliyekuwa karibu, ambaye Boazi amemnena, akapita. Naye akamwita, Haya! Wewe, karibu, uketi hapa. Naye akaja akaketi. Ruthu 4:1

Now Boaz went up to the gate, and sat him down there: and, behold, the near kinsman of whom Boaz spoke came by; to whom he said, Ho, such a one! turn aside, sit down here. He turned aside, and sat down.

Kisha akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, Ninyi nanyi, ketini hapa. Wakaketi. Ruthu 4:2

He took ten men of the elders of the city, and said, Sit you down here. They sat down.

Kisha akamwambia yule jamaa, Huyu Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi aliyokuwa nayo ndugu yetu, Elimeleki; Ruthu 4:3

He said to the near kinsman, Naomi, who has come back out of the country of Moab, is selling the parcel of land, which was our brother Elimelech's:

nami ilikuwa nia yangu nikujulishe wewe, na kukuambia, Uinunue mbele ya hawa waliopo na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya, uikomboe; lakini kama hutaikomboa, uniambie ili nijue mimi; kwa kuwa hakuna mtu wa kuikomboa ila wewe, na baada yako ni mimi. Naye akasema, Nitaikomboa mimi. Ruthu 4:4

I thought to disclose it to you, saying, Buy it before those who sit here, and before the elders of my people. If you will redeem it, redeem it: but if you will not redeem it, then tell me, that I may know; for there is none to redeem it besides you; and I am after you. He said, I will redeem it.

Ndipo Boazi aliposema, Siku ile utakapolinunua shamba mkononi mwa Naomi, unamnunua Ruthuu pia, huyu Mmoabi, mkewe marehemu, ili makusudi umwinulie marehemu jina katika urithi wake. Ruthu 4:5

Then said Boaz, What day you buy the field of the hand of Naomi, you must buy it also of Ruth the Moabitess, the wife of the dead, to raise up the name of the dead on his inheritance.

Basi yule jamaa aliyekuwa wa karibu akasema, Mimi sitaweza kulikomboa kwa nafsi yangu, nisije nikauharibu urithi wangu mwenyewe; basi haki yangu ya kulikomboa ujichukulie wewe, maana mimi sitaweza kulikomboa. Ruthu 4:6

The near kinsman said, I can't redeem it for myself, lest I mar my own inheritance: take my right of redemption on you; for I can't redeem it.

Basi hii ilikuwa desturi zamani za kale katika Israeli, kwa habari ya kukomboa na kubadiliana, ili kuyahakikisha yote; mtu huvua kiatu chake na kumpa mwenziwe; ndivyo walivyohakikisha neno katika Israeli. Ruthu 4:7

Now this was [the custom] in former time in Israel concerning redeeming and concerning exchanging, to confirm all things: a man drew off his shoe, and gave it to his neighbor; and this was the [manner of] attestation in Israel.

Basi yule jamaa akamwambia Boazi, Wewe ujinunulie mwenyewe. Akavua kiatu chake. Ruthu 4:8

So the near kinsman said to Boaz, Buy it for yourself. He drew off his shoe.

Naye Boazi akawaambia wale wazee na watu wote, Leo hivi ninyi ni mashahidi ya kwamba mimi nimenunua yote yaliyokuwa ya Elimeleki, na yote yaliyokuwa ya Kilioni na Maloni, mkononi mwa Naomi. Ruthu 4:9

Boaz said to the elders, and to all the people, You are witnesses this day, that I have bought all that was Elimelech's, and all that was Chilion's and Mahlon's, of the hand of Naomi.

Tena, huyu Ruthuu Mmoabi, mkewe Maloni, nimemnunua awe mke wangu, makusudi nipate kumwinulia marehemu jina katika urithi wake, jina lake marehemu lisikatike miongoni mwa ndugu zake, wala langoni pa mji wake; leo hivi ninyi ni mashahidi. Ruthu 4:10

Moreover Ruth the Moabitess, the wife of Mahlon, have I purchased to be my wife, to raise up the name of the dead on his inheritance, that the name of the dead not be cut off from among his brothers, and from the gate of his place: you are witnesses this day.

Na watu wote waliokuwapo langoni, na wale wazee, wakasema, Naam, sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wawili walioijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrata, na kuwa mashuhuri katika Bethlehemu. Ruthu 4:11

All the people who were in the gate, and the elders, said, We are witnesses. Yahweh make the woman who has come into your house like Rachel and like Leah, which two built the house of Israel: and do you worthily in Ephrathah, and be famous in Bethlehem:

Nyumba yako na ifanane na nyumba yake Peresi, ambaye kwamba Tamari alimzalia Yuda, kwa wazao atakaokupa Bwana katika mwanamke huyu. Ruthu 4:12

and let your house be like the house of Perez, whom Tamar bore to Judah, of the seed which Yahweh shall give you of this young woman.

Basi Boazi akamtwaa Ruthuu, naye akawa mke wake; naye akaingia kwake, na Bwana akamjalia kuchukua mimba, naye akazaa mtoto wa kiume. Ruthu 4:13

So Boaz took Ruth, and she became his wife; and he went in to her, and Yahweh gave her conception, and she bore a son.

Nao wale wanawake wakamwambia Naomi, Na ahimidiwe Bwana, asiyekuacha leo hali huna wa jamaa aliye karibu; jina lake huyu na liwe kuu katika Israeli. Ruthu 4:14

The women said to Naomi, Blessed be Yahweh, who has not left you this day without a near kinsman; and let his name be famous in Israel.

Naye atakurejezea uhai wako, na kukuangalia katika uzee wako; kwa maana mkweo, ambaye akupenda, naye anakufaa kuliko watoto saba, ndiye aliyemzaa. Ruthu 4:15

He shall be to you a restorer of life, and sustain you in your old age, for your daughter-in-law, who loves you, who is better to you than seven sons, has borne him.

Basi Naomi akamtwaa yule mtoto, akamweka kifuani pake, akawa mlezi wake. Ruthu 4:16

Naomi took the child, and laid it in her bosom, and became nurse to it.

Nao wale wanawake waliokuwa jirani zake wakampa jina, wakisema, Naomi amezaliwa mwana; wakamwita jina lake Obedi; yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi. Ruthu 4:17

The women her neighbors gave it a name, saying, There is a son born to Naomi; and they named him Obed: he is the father of Jesse, the father of David.

Hivi ndivyo vizazi vya Peresi; Peresi alimzaa Hesroni; Ruthu 4:18

Now this is the history of the generations of Perez: Perez became the father of Hezron,

na Hesroni akamzaa Ramu; na Ramu akamzaa Aminadabu; Ruthu 4:19

and Hezron became the father of Ram, and Ram became the father of Amminadab,

na Aminadabu akamzaa Nashoni; na Nashoni akamzaa Salmoni; Ruthu 4:20

and Amminadab became the father of Nahshon, and Nahshon became the father of Salmon,

na Salmoni akamzaa Boazi; na Boazi akamzaa Obedi; Ruthu 4:21

and Salmon became the father of Boaz, and Boaz became the father of Obed,

na Obedi akamzaa Yese; na Yese akamzaa Daudi. Ruthu 4:22

and Obed became the father of Jesse, and Jesse became the father of David.