Danieli 11 Swahili & English

Listen/Download Audio
Danieli 11 (Swahili) Daniel 11 (English)

Tena mimi, katika mwaka wa kwanza wa Dario, Mmedi, mimi nalisimama nimthibitishe na kumtia nguvu. Danieli 11:1

"As for me, in the first year of Darius the Mede, I stood up to confirm and strengthen him.

Nami sasa nitakuonyesha yaliyo kweli. Tazama, watasimama wafalme watatu katika Uajemi; naye mfalme wa nne atakuwa tajiri kuliko hao wote; naye atakapopata nguvu kwa utajiri wake, atawachochea wote juu ya ufalme wa Uyunani. Danieli 11:2

Now will I show you the truth. Behold, there shall stand up yet three kings in Persia; and the fourth shall be far richer than they all: and when he has grown strong through his riches, he shall stir up all against the realm of Greece.

Na mfalme hodari atasimama, atakayetawala kwa mamlaka kubwa, na kutenda apendavyo. Danieli 11:3

A mighty king shall stand up, who shall rule with great dominion, and do according to his will.

Naye atakaposimama, ufalme wake utavunjika, na kugawanyika katika pepo nne za mbinguni; lakini hautakuwa wa uzao wake, wala hautakuwa kama mamlaka yake ambayo alitawala kwayo; kwa maana ufalme wake utang'olewa, hata kwa ajili ya wengine zaidi ya hao. Danieli 11:4

When he shall stand up, his kingdom shall be broken, and shall be divided toward the four winds of the sky, but not to his posterity, nor according to his dominion with which he ruled; for his kingdom shall be plucked up, even for others besides these.

Na mfalme wa kusini atakuwa hodari; na mmoja wa wakuu wake atakuwa hodari kuliko yeye, naye atakuwa na mamlaka; mamlaka yake itakuwa mamlaka kubwa. Danieli 11:5

The king of the south shall be strong, and [one] of his princes; and he shall be strong above him, and have dominion; his dominion shall be a great dominion.

Na baada ya miaka kadha wa kadha watashirikiana; kwa kuwa binti wa mfalme wa kusini atakuja kwa mfalme wa kaskazini, ili kufanya mapatano naye; lakini hatakuwa na nguvu za mkono wake sikuzote; wala mfalme yule hatasimama, wala mkono wake; lakini yule binti atatolewa, na hao waliomleta, na yeye aliyemzaa, na yeye aliyemtia nguvu, zamani zile. Danieli 11:6

At the end of years they shall join themselves together; and the daughter of the king of the south shall come to the king of the north to make an agreement: but she shall not retain the strength of her arm; neither shall he stand, nor his arm; but she shall be given up, and those who brought her, and he who became the father of her, and he who strengthened her in those times.

Lakini katika chipukizi la mizizi yake atasimama mmoja mahali pake atakayeliendesha jeshi la askari, naye ataingia katika ngome ya mfalme wa kaskazini, na kuwatenda mambo, na kuwashinda; Danieli 11:7

But out of a shoot from her roots shall one stand up in his place, who shall come to the army, and shall enter into the fortress of the king of the north, and shall deal against them, and shall prevail.

na miungu yao, pamoja na sanamu zao, na vyombo vyao vizuri vya fedha na dhahabu atavichukua mpaka Misri; kisha atajizuia miaka kadha wa kadha asimwendee mfalme wa kaskazini. Danieli 11:8

Also their gods, with their molten images, [and] with their goodly vessels of silver and of gold, shall he carry captive into Egypt; and he shall refrain some years from the king of the north.

Naye huyo ataingia katika ufalme wa mfalme wa kusini, lakini atarudi mpaka nchi yake mwenyewe. Danieli 11:9

He shall come into the realm of the king of the south, but he shall return into his own land.

Na wanawe watafanya vita, na kukusanya mkutano wa majeshi makuu; watakaokuja na kufurika na kupita katikati; nao watarudi na kufanya vita mpaka penye ngome yake. Danieli 11:10

His sons shall war, and shall assemble a multitude of great forces, which shall come on, and overflow, and pass through; and they shall return and war, even to his fortress.

Na mfalme wa kusini ataingiliwa na ghadhabu, naye atatoka na kupigana naye, yaani, na mfalme wa kaskazini; naye atapanga jeshi kubwa; na jeshi hilo litawekwa mikononi mwake. Danieli 11:11

The king of the south shall be moved with anger, and shall come forth and fight with him, even with the king of the north; and he shall set forth a great multitude, and the multitude shall be given into his hand.

Atakapokwisha kuchukua lile jeshi, moyo wake utatukuzwa; naye atawaangusha makumi elfu; lakini hataongezewa nguvu. Danieli 11:12

The multitude shall be lifted up, and his heart shall be exalted; and he shall cast down tens of thousands, but he shall not prevail.

Kwa maana mfalme wa kaskazini atarudi, naye atapanga jeshi kubwa kuliko lile la kwanza; naye hakika atakuja mwisho wa zamani zile, yaani, baada ya miaka kadha wa kadha, pamoja na jeshi kubwa na mali nyingi. Danieli 11:13

The king of the north shall return, and shall set forth a multitude greater than the former; and he shall come on at the end of the times, [even of] years, with a great army and with much substance.

Na zamani zile watu wengi watasimama ili kumpinga mfalme wa kusini; pia, wenye jeuri miongoni mwa watu wako watajiinua ili kuyathibitisha maono; lakini wataanguka. Danieli 11:14

In those times there shall many stand up against the king of the south: also the children of the violent among your people shall lift themselves up to establish the vision; but they shall fall.

Basi mfalme wa kaskazini atakuja, na kufanya kilima, na kuupiga mji wenye maboma; na silaha za kusini hazitaweza kumpinga, wala watu wake wateule, wala hapatakuwa na nguvu za kumpinga. Danieli 11:15

So the king of the north shall come, and cast up a mound, and take a well-fortified city: and the forces of the south shall not stand, neither his chosen people, neither shall there be any strength to stand.

Maana ajaye kupigana naye atatenda kadiri apendavyo, wala hapana mtu atakayesimama mbele yake; naye atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi mwake. Danieli 11:16

But he who comes against him shall do according to his own will, and none shall stand before him; and he shall stand in the glorious land, and in his hand shall be destruction.

Naye atakaza uso wake ili aje pamoja na nguvu zote za ufalme wake, naye atafanya mapatano naye; naye atatenda kadiri apendavyo; naye atampa binti wa watu ili amharibu; lakini hilo halitasimama wala kumfaa. Danieli 11:17

He shall set his face to come with the strength of his whole kingdom, and with him equitable conditions; and he shall perform them: and he shall give him the daughter of women, to corrupt her; but she shall not stand, neither be for him.

Baada ya hayo atauelekeza uso wake kwenye visiwa, naye atavipiga visiwa vingi; lakini mkuu mmoja ataikomesha aibu iliyoletwa na yeye; naam, aibu yake hiyo atamrudishia mwenyewe. Danieli 11:18

After this shall he turn his face to the isles, and shall take many: but a prince shall cause the reproach offered by him to cease; yes, moreover, he shall cause his reproach to turn on him.

Ndipo atauelekeza uso wake kwenye ngome za nchi yake mwenyewe; lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena. Danieli 11:19

Then he shall turn his face toward the fortresses of his own land; but he shall stumble and fall, and shall not be found.

Ndipo badala yake atasimama mmoja, atakayepitisha mwenye kutoza ushuru kati ya utukufu wa ufalme wake; lakini katika muda wa siku chache ataangamizwa, si kwa hasira, wala si katika vita. Danieli 11:20

Then shall stand up in his place one who shall cause a tax collector to pass through the kingdom to maintain its glory; but within few days he shall be destroyed, neither in anger, nor in battle.

Kisha badala yake atasimama mmoja, mtu astahiliye kudharauliwa, ambaye hawakumpa heshima ya ufalme; naye atakuja wakati wa amani, naye ataupata ufalme kwa kujipendekeza. Danieli 11:21

In his place shall stand up a contemptible person, to whom they had not given the honor of the kingdom: but he shall come in time of security, and shall obtain the kingdom by flatteries.

Na wale wenye silaha mfano wa gharika watagharikishwa mbele yake, na kuvunjika, naam, mkuu wa maagano pia. Danieli 11:22

The overwhelming forces shall be overwhelmed from before him, and shall be broken; yes, also the prince of the covenant.

Na baada ya maagano atatenda kwa hila; maana atapanda, naye atakuwa hodari pamoja na watu wadogo. Danieli 11:23

After the league made with him he shall work deceitfully; for he shall come up, and shall become strong, with a small people.

Wakati wa amani atapaingia mahali palipofanikiwa sana pa wilaya hiyo; naye atatenda mambo ambayo baba zake hawakuyatenda, wala babu zake; atatawanya kati yao mawindo, na mateka, na mali; naam, atatunga hila zake juu ya ngome, hata wakati ulioamriwa. Danieli 11:24

In time of security shall he come even on the fattest places of the province; and he shall do that which his fathers have not done, nor his fathers' fathers; he shall scatter among them prey, and spoil, and substance: yes, he shall devise his devices against the strongholds, even for a time.

Naye atachochea nguvu zake na ushujaa wake juu ya huyo mfalme wa kusini kwa jeshi kubwa; na mfalme wa kusini atafanya vita kwa jeshi kubwa mno lenye nguvu nyingi; lakini hatasimama; maana watatunga hila juu yake. Danieli 11:25

He shall stir up his power and his courage against the king of the south with a great army; and the king of the south shall war in battle with an exceeding great and mighty army; but he shall not stand; for they shall devise devices against him.

Naam, walao sehemu ya chakula chake watamwangamiza, na jeshi lake litagharikishwa; na wengi wataanguka wameuawa. Danieli 11:26

Yes, they who eat of his dainties shall destroy him, and his army shall overflow; and many shall fall down slain.

Na katika habari za wafalme hao wawili, mioyo yao watanuia kutenda madhara, nao watasema uongo walipo pamoja mezani; lakini hilo halitafanikiwa; maana mwisho utatokea wakati ulioamriwa. Danieli 11:27

As for both these kings, their hearts shall be to do mischief, and they shall speak lies at one table: but it shall not prosper; for yet the end shall be at the time appointed.

Ndipo atakaporudi mpaka nchi yake mwenye utajiri mwingi; na moyo wake utakuwa kinyume cha hilo agano takatifu; naye atafanya kama apendavyo, na kurudi mpaka nchi yake. Danieli 11:28

Then shall he return into his land with great substance; and his heart [shall be] against the holy covenant; and he shall do [his pleasure], and return to his own land.

Kwa wakati ulioamriwa atarudi, na kuingia upande wa kusini; lakini wakati wa mwisho mambo hayatakuwa kama yalivyokuwa wakati wa kwanza. Danieli 11:29

At the time appointed he shall return, and come into the south; but it shall not be in the latter time as it was in the former.

Maana merikebu za Kitimu zitakuja kupigana naye; basi atavunjika moyo, naye atarudi na kulighadhibikia hilo agano takatifu; na kutenda kadiri apendavyo; naam, atarudi, na kuwasikiliza walioacha hilo agano takatifu. Danieli 11:30

For ships of Kittim shall come against him; therefore he shall be grieved, and shall return, and have indignation against the holy covenant, and shall do [his pleasure]: he shall even return, and have regard to those who forsake the holy covenant.

Na wenye silaha watasimama upande wake, nao watapatia unajisi mahali patakatifu, ndiyo ngome, nao wataondoa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, nao watalisimamisha chukizo la uharibifu. Danieli 11:31

Forces shall stand on his part, and they shall profane the sanctuary, even the fortress, and shall take away the continual [burnt offering], and they shall set up the abomination that makes desolate.

Na wao wafanyao maovu juu ya hilo agano atawapotosha kwa maneno ya kujipendekeza; lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu. Danieli 11:32

Such as do wickedly against the covenant shall he pervert by flatteries; but the people who know their God shall be strong, and do [exploits].

Na hao walio wenye hekima katika watu watafundisha wengi; hata hivyo wataanguka kwa upanga, na kwa moto, na kwa kufungwa, na kwa kutekwa nyara, siku nyingi. Danieli 11:33

Those who are wise among the people shall instruct many; yet they shall fall by the sword and by flame, by captivity and by spoil, [many] days.

Basi watakapoanguka, watasaidiwa kwa msaada kidogo; lakini wengi wataambatana nao kwa maneno ya kujipendekeza. Danieli 11:34

Now when they shall fall, they shall be helped with a little help; but many shall join themselves to them with flatteries.

Na baadhi yao wenye hekima wataanguka, ili kuwatakasa, na kuwasafisha, na kuwafanya weupe, hata wakati wa mwisho; kwa maana ni kwa wakati ulioamriwa, ambao haujaja. Danieli 11:35

Some of those who are wise shall fall, to refine them, and to purify, and to make them white, even to the time of the end; because it is yet for the time appointed.

Naye mfalme atafanya kama apendavyo; naye atajitukuza na kujiadhimisha juu ya kila mungu, naye atanena maneno ya ajabu juu ya Mungu wa miungu, naye atafanikiwa mpaka ghadhabu itakapotimia; maana yaliyokusudiwa yatafanyika. Danieli 11:36

The king shall do according to his will; and he shall exalt himself, and magnify himself above every god, and shall speak marvelous things against the God of gods; and he shall prosper until the indignation be accomplished; for that which is determined shall be done.

Wala hataijali miungu ya baba zake; wala yeye aliyetamaniwa na wanawake; wala hatamjali mungu awaye yote; maana atajitukuza mwenyewe juu ya wote. Danieli 11:37

Neither shall he regard the gods of his fathers, nor the desire of women, nor regard any god; for he shall magnify himself above all.

Lakini katika mahali pake atamheshimu mungu wa ngome; na mungu ambaye baba zake hawakumjua atamheshimu, kwa dhahabu, na fedha, na vito vya thamani, na vitu vipendezavyo. Danieli 11:38

But in his place shall he honor the god of fortresses; and a god whom his fathers didn't know shall he honor with gold, and silver, and with precious stones, and pleasant things.

Naye ataziteka nyara ngome zenye nguvu kwa msaada wa mungu mgeni; na yeye atakayemkubali atamwongeza kwa utukufu; naye atawapa kumiliki wengi; naye ataigawa nchi kwa rushwa, Danieli 11:39

He shall deal with the strongest fortresses by the help of a foreign god: whoever acknowledges [him] he will increase with glory; and he shall cause them to rule over many, and shall divide the land for a price.

na wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana naye; na mfalme wa kaskazini atamshambulia kama upepo wa kisulisuli, pamoja na magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi; naye ataingia katika nchi hizo, na kufurika na kupita katikati. Danieli 11:40

At the time of the end shall the king of the south contend with him; and the king of the north shall come against him like a whirlwind, with chariots, and with horsemen, and with many ships; and he shall enter into the countries, and shall overflow and pass through.

Tena ataingia katika hiyo nchi ya uzuri, na nchi nyingi zitapinduliwa; lakini nchi hizi zitaokolewa na mkono wake, Edomu, na Moabu, na wakuu wa watu wa Amoni. Danieli 11:41

He shall enter also into the glorious land, and many [countries] shall be overthrown; but these shall be delivered out of his hand: Edom, and Moab, and the chief of the children of Ammon.

Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, hata na nchi ya Misri haitaokoka. Danieli 11:42

He shall stretch forth his hand also on the countries; and the land of Egypt shall not escape.

Lakini atakuwa na nguvu juu ya hazina za dhahabu na fedha, na juu ya vitu vyote vya Misri vyenye thamani; na Walibia na Wakushi watafuata nyayo zake. Danieli 11:43

But he shall have power over the treasures of gold and of silver, and over all the precious things of Egypt; and the Libyans and the Ethiopians shall be at his steps.

Lakini habari zitokazo mashariki na kaskazini zitamfadhaisha; naye atatoka kwa ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi. Danieli 11:44

But news out of the east and out of the north shall trouble him; and he shall go forth with great fury to destroy and utterly to sweep away many.

Naye ataweka hema zake za kifalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa uzuri; lakini ataifikilia ajali yake, wala hakuna atakayemsaidia. Danieli 11:45

He shall plant the tents of his palace between the sea and the glorious holy mountain; yet he shall come to his end, and none shall help him.