Wakolosai 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
Wakolosai 4 (Swahili) Colossians 4 (English)

Ninyi akina bwana, wapeni watumwa wenu yaliyo haki na ya adili, mkijua ya kuwa ninyi nanyi mna Bwana mbinguni. Wakolosai 4:1

Masters, give to your servants that which is just and equal, knowing that you also have a Master in heaven.

Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani; Wakolosai 4:2

Continue steadfastly in prayer, watching therein with thanksgiving;

mkituombea na sisi pia, kwamba Mungu atufungulie mlango kwa lile neno lake, tuinene siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake nimefungwa, Wakolosai 4:3

praying together for us also, that God may open to us a door for the word, to speak the mystery of Christ, for which I am also in bonds;

ili niidhihirishe, kama inipasavyo kunena. Wakolosai 4:4

that I may reveal it as I ought to speak.

Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. Wakolosai 4:5

Walk in wisdom toward those who are outside, redeeming the time.

Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu. Wakolosai 4:6

Let your speech always be with grace, seasoned with salt, that you may know how you ought to answer each one.

Tikiko, ndugu mpendwa, mtumishi mwaminifu, mjoli wangu katika Bwana, atawaarifu mambo yangu yote; Wakolosai 4:7

All my affairs will be made known to you by Tychicus, the beloved brother, faithful servant, and fellow bondservant in the Lord.

ambaye nimemtuma kwenu kwa sababu iyo hiyo, ili mjue mambo yetu, naye akawafariji mioyo yenu; Wakolosai 4:8

I am sending him to you for this very purpose, that he may know your circumstances and comfort your hearts,

pamoja na Onesimo, ndugu mwaminifu, mpendwa, aliye mtu wa kwenu. Hao watawaarifu mambo yote ya hapa petu. Wakolosai 4:9

together with Onesimus, the faithful and beloved brother, who is one of you. They will make known to you everything that is going on here.

Aristarko, aliyefungwa pamoja nami, awasalimu; na Marko, mjomba wake Barnaba, ambaye mmepokea maagizo kwa habari yake; akifika kwenu mkaribisheni. Wakolosai 4:10

Aristarchus, my fellow prisoner greets you, and Mark, the cousin of Barnabas (concerning whom you received commandments, "if he comes to you, receive him"),

Na Yesu aitwaye Yusto; hao ni watu wa tohara. Tena hao peke yao ni watendaji wa kazi pamoja nami kwa ajili ya ufalme wa Mungu; nao walikuwa faraja kwangu. Wakolosai 4:11

and Jesus who is called Justus, who are of the circumcision. These are my only fellow workers for the Kingdom of God, men who have been a comfort to me.

Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu. Wakolosai 4:12

Epaphras, who is one of you, a servant of Christ, salutes you, always striving for you in his prayers, that you may stand perfect and complete in all the will of God.

Maana namshuhudia kwamba ana juhudi nyingi kwa ajili yenu, na kwa ajili ya hao walioko Laodikia, na kwa ajili ya hao walioko Hierapoli. Wakolosai 4:13

For I testify about him, that he has great zeal for you, and for those in Laodicea, and for those in Hierapolis.

Luka, yule tabibu mpendwa, na Dema, wanawasalimu. Wakolosai 4:14

Luke, the beloved physician, and Demas greet you.

Wasalimuni ndugu walioko Laodikia, na Nimfa, na kanisa lililo katika nyumba yake. Wakolosai 4:15

Greet the brothers who are in Laodicea, and Nymphas, and the assembly that is in his house.

Waraka huu ukiisha kusomwa kwenu fanyeni kwamba usomwe katika kanisa la Walaodikia pia; na ule wa Laodikia usomwe na ninyi. Wakolosai 4:16

When this letter has been read among you, cause it to be read also in the assembly of the Laodiceans; and that you also read the letter from Laodicea.

Mwambieni Arkipo, Iangalie sana huduma ile uliyopewa katika Bwana, ili uitimize. Wakolosai 4:17

Tell Archippus, "Take heed to the ministry which you have received in the Lord, that you fulfill it."

Salamu yangu mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe. Kumbukeni kufungwa kwangu. Neema na iwe pamoja nanyi. Wakolosai 4:18

The salutation of me, Paul, with my own hand: remember my bonds. Grace be with you. Amen.