2 Timotheo 3 Swahili & English
Listen/Download Audio2 Timotheo 3 (Swahili) | 2nd Timothy 3 (English) |
---|---|
Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Timotheo 3:1 |
But know this, that in the last days, grievous times will come. |
Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 2 Timotheo 3:2 |
For men will be lovers of self, lovers of money, boastful, arrogant, blasphemers, disobedient to parents, unthankful, unholy, |
wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, 2 Timotheo 3:3 |
without natural affection, unforgiving, slanderers, without self-control, fierce, no lovers of good, |
wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; 2 Timotheo 3:4 |
traitors, headstrong, conceited, lovers of pleasure rather than lovers of God; |
wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao. 2 Timotheo 3:5 |
holding a form of godliness, but having denied the power thereof. Turn away from these, also. |
Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi; 2 Timotheo 3:6 |
For of these are those who creep into houses, and take captive gullible women loaded down with sins, led away by various lusts, |
wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli. 2 Timotheo 3:7 |
always learning, and never able to come to the knowledge of the truth. |
Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani. 2 Timotheo 3:8 |
Even as Jannes and Jambres opposed Moses, so do these also oppose the truth; men corrupted in mind, reprobate concerning the faith. |
Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri. 2 Timotheo 3:9 |
But they will proceed no further. For their folly will be evident to all men, as theirs also came to be. |
Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, 2 Timotheo 3:10 |
But you did follow my teaching, conduct, purpose, faith, patience, love, steadfastness, |
na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. 2 Timotheo 3:11 |
persecutions, and sufferings: those things that happened to me at Antioch, Iconium, and Lystra. I endured those persecutions. Out of them all the Lord delivered me. |
Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. 2 Timotheo 3:12 |
Yes, and all who desire to live godly in Christ Jesus will suffer persecution. |
lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. 2 Timotheo 3:13 |
But evil men and impostors will grow worse and worse, deceiving and being deceived. |
Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; 2 Timotheo 3:14 |
But you remain in the things which you have learned and have been assured of, knowing from whom you have learned them. |
na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu. 2 Timotheo 3:15 |
From infancy, you have known the sacred writings which are able to make you wise for salvation through faith, which is in Christ Jesus. |
Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 2 Timotheo 3:16 |
Every writing inspired by God{literally, God-breathed} is profitable for teaching, for reproof, for correction, and for instruction which is in righteousness, |
ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema. 2 Timotheo 3:17 |
that the man of God may be complete, thoroughly equipped for every good work. |