2 Timotheo 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Timotheo 3 (Swahili) 2nd Timothy 3 (English)

Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Timotheo 3:1

But know this, that in the last days, grievous times will come.

Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 2 Timotheo 3:2

For men will be lovers of self, lovers of money, boastful, arrogant, blasphemers, disobedient to parents, unthankful, unholy,

wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, 2 Timotheo 3:3

without natural affection, unforgiving, slanderers, without self-control, fierce, no lovers of good,

wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; 2 Timotheo 3:4

traitors, headstrong, conceited, lovers of pleasure rather than lovers of God;

wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao. 2 Timotheo 3:5

holding a form of godliness, but having denied the power thereof. Turn away from these, also.

Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi; 2 Timotheo 3:6

For of these are those who creep into houses, and take captive gullible women loaded down with sins, led away by various lusts,

wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli. 2 Timotheo 3:7

always learning, and never able to come to the knowledge of the truth.

Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani. 2 Timotheo 3:8

Even as Jannes and Jambres opposed Moses, so do these also oppose the truth; men corrupted in mind, reprobate concerning the faith.

Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri. 2 Timotheo 3:9

But they will proceed no further. For their folly will be evident to all men, as theirs also came to be.

Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, 2 Timotheo 3:10

But you did follow my teaching, conduct, purpose, faith, patience, love, steadfastness,

na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. 2 Timotheo 3:11

persecutions, and sufferings: those things that happened to me at Antioch, Iconium, and Lystra. I endured those persecutions. Out of them all the Lord delivered me.

Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. 2 Timotheo 3:12

Yes, and all who desire to live godly in Christ Jesus will suffer persecution.

lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. 2 Timotheo 3:13

But evil men and impostors will grow worse and worse, deceiving and being deceived.

Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; 2 Timotheo 3:14

But you remain in the things which you have learned and have been assured of, knowing from whom you have learned them.

na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu. 2 Timotheo 3:15

From infancy, you have known the sacred writings which are able to make you wise for salvation through faith, which is in Christ Jesus.

Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 2 Timotheo 3:16

Every writing inspired by God{literally, God-breathed} is profitable for teaching, for reproof, for correction, and for instruction which is in righteousness,

ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema. 2 Timotheo 3:17

that the man of God may be complete, thoroughly equipped for every good work.