2 Timotheo 2 Swahili & English
Listen/Download Audio2 Timotheo 2 (Swahili) | 2nd Timothy 2 (English) |
---|---|
Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu. 2 Timotheo 2:1 |
You therefore, my child, be strengthened in the grace that is in Christ Jesus. |
Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine. 2 Timotheo 2:2 |
The things which you have heard from me among many witnesses, commit the same to faithful men, who will be able to teach others also. |
Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu. 2 Timotheo 2:3 |
You therefore must endure hardship, as a good soldier of Christ Jesus. |
Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari. 2 Timotheo 2:4 |
No soldier on service entangles himself in the affairs of life, that he may please him who enrolled him as a soldier. |
Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali. 2 Timotheo 2:5 |
Also, if anyone competes in athletics, he isn't crowned unless he has competed by the rules. |
Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa kwanza wa kupata fungu la matunda. 2 Timotheo 2:6 |
The farmers who labor must be the first to get a share of the crops. |
Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote. 2 Timotheo 2:7 |
Consider what I say, and may the Lord give you understanding in all things. |
Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo injili yangu. 2 Timotheo 2:8 |
Remember Jesus Christ, risen from the dead, of the seed of David, according to my Gospel, |
Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi. 2 Timotheo 2:9 |
in which I suffer hardship to the point of chains as a criminal. But God's word isn't chained. |
Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. 2 Timotheo 2:10 |
Therefore I endure all things for the chosen ones' sake, that they also may obtain the salvation which is in Christ Jesus with eternal glory. |
Ni neno la kuaminiwa. Kwa maana, Kama tukifa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia; 2 Timotheo 2:11 |
This saying is faithful: For if we died with him, We will also live with him. |
Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi; 2 Timotheo 2:12 |
If we endure, We will also reign with him. If we deny him, He also will deny us. |
Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe. 2 Timotheo 2:13 |
If we are faithless, He remains faithful. He can't deny himself. |
Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao. 2 Timotheo 2:14 |
Remind them of these things, charging them in the sight of the Lord, that they don't argue about words, to no profit, to the subverting of those who hear. |
Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli. 2 Timotheo 2:15 |
Give diligence to present yourself approved by God, a workman who doesn't need to be ashamed, properly handling the Word of Truth. |
Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu, 2 Timotheo 2:16 |
But shun empty chatter, for they will proceed further in ungodliness, |
na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto, 2 Timotheo 2:17 |
and their word will consume like gangrene, of whom is Hymenaeus and Philetus; |
walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha. 2 Timotheo 2:18 |
men who have erred concerning the truth, saying that the resurrection is already past, and overthrowing the faith of some. |
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu. 2 Timotheo 2:19 |
However God's firm foundation stands, having this seal, "The Lord knows those who are his," and, "Let every one who names the name of the Lord{TR reads "Christ" instead of "the Lord"} depart from unrighteousness." |
Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina. 2 Timotheo 2:20 |
Now in a great house there are not only vessels of gold and of silver, but also of wood and of clay. Some are for honor, and some for dishonor. |
Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema. 2 Timotheo 2:21 |
If anyone therefore purges himself from these, he will be a vessel for honor, sanctified, and suitable for the master's use, prepared for every good work. |
Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi. 2 Timotheo 2:22 |
Flee from youthful lusts; but pursue righteousness, faith, love, and peace with those who call on the Lord out of a pure heart. |
Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi. 2 Timotheo 2:23 |
But refuse foolish and ignorant questionings, knowing that they generate strife. |
Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu; 2 Timotheo 2:24 |
The Lord's servant must not quarrel, but be gentle towards all, able to teach, patient, |
akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; 2 Timotheo 2:25 |
in gentleness correcting those who oppose him: perhaps God may give them repentance leading to a full knowledge of the truth, |
wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake. 2 Timotheo 2:26 |
and they may recover themselves out of the devil's snare, having been taken captive by him to his will. |