2 Timotheo 2 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Timotheo 2 (Swahili) 2nd Timothy 2 (English)

Basi wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu. 2 Timotheo 2:1

You therefore, my child, be strengthened in the grace that is in Christ Jesus.

Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine. 2 Timotheo 2:2

The things which you have heard from me among many witnesses, commit the same to faithful men, who will be able to teach others also.

Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu. 2 Timotheo 2:3

You therefore must endure hardship, as a good soldier of Christ Jesus.

Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari. 2 Timotheo 2:4

No soldier on service entangles himself in the affairs of life, that he may please him who enrolled him as a soldier.

Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali. 2 Timotheo 2:5

Also, if anyone competes in athletics, he isn't crowned unless he has competed by the rules.

Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa kwanza wa kupata fungu la matunda. 2 Timotheo 2:6

The farmers who labor must be the first to get a share of the crops.

Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote. 2 Timotheo 2:7

Consider what I say, and may the Lord give you understanding in all things.

Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo injili yangu. 2 Timotheo 2:8

Remember Jesus Christ, risen from the dead, of the seed of David, according to my Gospel,

Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa kama mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi. 2 Timotheo 2:9

in which I suffer hardship to the point of chains as a criminal. But God's word isn't chained.

Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. 2 Timotheo 2:10

Therefore I endure all things for the chosen ones' sake, that they also may obtain the salvation which is in Christ Jesus with eternal glory.

Ni neno la kuaminiwa. Kwa maana, Kama tukifa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia; 2 Timotheo 2:11

This saying is faithful: For if we died with him, We will also live with him.

Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi; 2 Timotheo 2:12

If we endure, We will also reign with him. If we deny him, He also will deny us.

Kama sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe. 2 Timotheo 2:13

If we are faithless, He remains faithful. He can't deny himself.

Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao. 2 Timotheo 2:14

Remind them of these things, charging them in the sight of the Lord, that they don't argue about words, to no profit, to the subverting of those who hear.

Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli. 2 Timotheo 2:15

Give diligence to present yourself approved by God, a workman who doesn't need to be ashamed, properly handling the Word of Truth.

Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu, 2 Timotheo 2:16

But shun empty chatter, for they will proceed further in ungodliness,

na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto, 2 Timotheo 2:17

and their word will consume like gangrene, of whom is Hymenaeus and Philetus;

walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata kuipindua imani ya watu kadha wa kadha. 2 Timotheo 2:18

men who have erred concerning the truth, saying that the resurrection is already past, and overthrowing the faith of some.

Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu. 2 Timotheo 2:19

However God's firm foundation stands, having this seal, "The Lord knows those who are his," and, "Let every one who names the name of the Lord{TR reads "Christ" instead of "the Lord"} depart from unrighteousness."

Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina. 2 Timotheo 2:20

Now in a great house there are not only vessels of gold and of silver, but also of wood and of clay. Some are for honor, and some for dishonor.

Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, kimetengenezwa kwa kila kazi iliyo njema. 2 Timotheo 2:21

If anyone therefore purges himself from these, he will be a vessel for honor, sanctified, and suitable for the master's use, prepared for every good work.

Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi. 2 Timotheo 2:22

Flee from youthful lusts; but pursue righteousness, faith, love, and peace with those who call on the Lord out of a pure heart.

Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi. 2 Timotheo 2:23

But refuse foolish and ignorant questionings, knowing that they generate strife.

Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu; 2 Timotheo 2:24

The Lord's servant must not quarrel, but be gentle towards all, able to teach, patient,

akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; 2 Timotheo 2:25

in gentleness correcting those who oppose him: perhaps God may give them repentance leading to a full knowledge of the truth,

wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake. 2 Timotheo 2:26

and they may recover themselves out of the devil's snare, having been taken captive by him to his will.