1 Timotheo 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Timotheo 4 (Swahili) 1st Timothy 4 (English)

Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; 1 Timotheo 4:1

But the Spirit says expressly that in later times some will fall away from the faith, paying attention to seducing spirits and doctrines of demons,

kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; 1 Timotheo 4:2

through the hypocrisy of men who speak lies, branded in their own conscience as with a hot iron;

wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli. 1 Timotheo 4:3

forbidding marriage and commanding to abstain from foods which God created to be received with thanksgiving by those who believe and know the truth.

Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani; 1 Timotheo 4:4

For every creature of God is good, and nothing is to be rejected, if it is received with thanksgiving.

kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba. 1 Timotheo 4:5

For it is sanctified through the word of God and prayer.

Uwakumbushe ndugu mambo hayo, nawe utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, na mzoevu wa maneno ya imani, na mafundisho mazuri yale uliyoyafuata. 1 Timotheo 4:6

If you instruct the brothers of these things, you will be a good servant of Christ Jesus, nourished in the words of the faith, and of the good doctrine which you have followed.

Bali hadithi za kizee, zisizokuwa za dini, uzikatae; nawe ujizoeze kupata utauwa. 1 Timotheo 4:7

But refuse profane and old wives' fables. Exercise yourself toward godliness.

Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye. 1 Timotheo 4:8

For bodily exercise has some value, but godliness has value for all things, having the promise of the life which is now, and of that which is to come.

Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa; 1 Timotheo 4:9

This saying is faithful and worthy of all acceptance.

kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio. 1 Timotheo 4:10

For to this end we both labor and suffer reproach, because we have set our trust in the living God, who is the Savior of all men, especially of those who believe.

Mambo hayo uyaagize na kuyafundisha. 1 Timotheo 4:11

Command and teach these things.

Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi. 1 Timotheo 4:12

Let no man despise your youth; but be an example to those who believe, in word, in your way of life, in love, in spirit, in faith, and in purity.

Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha. 1 Timotheo 4:13

Until I come, pay attention to reading, to exhortation, and to teaching.

Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee. 1 Timotheo 4:14

Don't neglect the gift that is in you, which was given to you by prophecy, with the laying on of the hands of the elders.

Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote. 1 Timotheo 4:15

Be diligent in these things. Give yourself wholly to them, that your progress may be revealed to all.

Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia. 1 Timotheo 4:16

Pay attention to yourself, and to your teaching. Continue in these things, for in doing this you will save both yourself and those who hear you.