1 Wathesalonike 5 Swahili & English
Listen/Download Audio1 Wathesalonike 5 (Swahili) | 1st Thessalonians 5 (English) |
---|---|
Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. 1 Wathesalonike 5:1 |
But concerning the times and the seasons, brothers, you have no need that anything be written to you. |
Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. 1 Wathesalonike 5:2 |
For you yourselves know well that the day of the Lord comes like a thief in the night. |
Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. 1 Wathesalonike 5:3 |
For when they are saying, "Peace and safety," then sudden destruction will come on them, like birth pains on a pregnant woman; and they will in no way escape. |
Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi. 1 Wathesalonike 5:4 |
But you, brothers, aren't in darkness, that the day should overtake you like a thief. |
Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza. 1 Wathesalonike 5:5 |
You are all children of light, and children of the day. We don't belong to the night, nor to darkness, |
Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi. 1 Wathesalonike 5:6 |
so then let's not sleep, as the rest do, but let's watch and be sober. |
Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 1 Wathesalonike 5:7 |
For those who sleep, sleep in the night, and those who are drunken are drunken in the night. |
Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu. 1 Wathesalonike 5:8 |
But let us, since we belong to the day, be sober, putting on the breastplate of faith and love, and, for a helmet, the hope of salvation. |
Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; 1 Wathesalonike 5:9 |
For God didn't appoint us to wrath, but to the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ, |
ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala. 1 Wathesalonike 5:10 |
who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him. |
Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya. 1 Wathesalonike 5:11 |
Therefore exhort one another, and build each other up, even as you also do. |
Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; 1 Wathesalonike 5:12 |
But we beg you, brothers, to know those who labor among you, and are over you in the Lord, and admonish you, |
mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi. 1 Wathesalonike 5:13 |
and to respect and honor them in love for their work's sake. Be at peace among yourselves. |
Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote. 1 Wathesalonike 5:14 |
We exhort you, brothers, admonish the disorderly, encourage the fainthearted, support the weak, be patient toward all. |
Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote. 1 Wathesalonike 5:15 |
See that no one returns evil for evil to anyone, but always follow after that which is good, for one another, and for all. |
Furahini siku zote; 1 Wathesalonike 5:16 |
Rejoice always. |
ombeni bila kukoma; 1 Wathesalonike 5:17 |
Pray without ceasing. |
shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu. 1 Wathesalonike 5:18 |
In everything give thanks, for this is the will of God in Christ Jesus toward you. |
Msimzimishe Roho; 1 Wathesalonike 5:19 |
Don't quench the Spirit. |
msitweze unabii; 1 Wathesalonike 5:20 |
Don't despise prophesies. |
jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema; 1 Wathesalonike 5:21 |
Test all things, and hold firmly that which is good. |
jitengeni na ubaya wa kila namna. 1 Wathesalonike 5:22 |
Abstain from every form of evil. |
Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo. 1 Wathesalonike 5:23 |
May the God of peace himself sanctify you completely. May your whole spirit, soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ. |
Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya. 1 Wathesalonike 5:24 |
Faithful is he who calls you, who will also do it. |
Ndugu, tuombeeni. 1 Wathesalonike 5:25 |
Brothers, pray for us. |
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu. 1 Wathesalonike 5:26 |
Greet all the brothers with a holy kiss. |
Nawaapisha kwa Bwana, ndugu wote wasomewe waraka huu. 1 Wathesalonike 5:27 |
I solemnly charge you by the Lord that this letter be read to all the holy brothers. |
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. 1 Wathesalonike 5:28 |
The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen. |