1 Wathesalonike 5 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Wathesalonike 5 (Swahili) 1st Thessalonians 5 (English)

Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. 1 Wathesalonike 5:1

But concerning the times and the seasons, brothers, you have no need that anything be written to you.

Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. 1 Wathesalonike 5:2

For you yourselves know well that the day of the Lord comes like a thief in the night.

Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. 1 Wathesalonike 5:3

For when they are saying, "Peace and safety," then sudden destruction will come on them, like birth pains on a pregnant woman; and they will in no way escape.

Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi. 1 Wathesalonike 5:4

But you, brothers, aren't in darkness, that the day should overtake you like a thief.

Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza. 1 Wathesalonike 5:5

You are all children of light, and children of the day. We don't belong to the night, nor to darkness,

Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi. 1 Wathesalonike 5:6

so then let's not sleep, as the rest do, but let's watch and be sober.

Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 1 Wathesalonike 5:7

For those who sleep, sleep in the night, and those who are drunken are drunken in the night.

Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu. 1 Wathesalonike 5:8

But let us, since we belong to the day, be sober, putting on the breastplate of faith and love, and, for a helmet, the hope of salvation.

Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; 1 Wathesalonike 5:9

For God didn't appoint us to wrath, but to the obtaining of salvation through our Lord Jesus Christ,

ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala. 1 Wathesalonike 5:10

who died for us, that, whether we wake or sleep, we should live together with him.

Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya. 1 Wathesalonike 5:11

Therefore exhort one another, and build each other up, even as you also do.

Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; 1 Wathesalonike 5:12

But we beg you, brothers, to know those who labor among you, and are over you in the Lord, and admonish you,

mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi. 1 Wathesalonike 5:13

and to respect and honor them in love for their work's sake. Be at peace among yourselves.

Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote. 1 Wathesalonike 5:14

We exhort you, brothers, admonish the disorderly, encourage the fainthearted, support the weak, be patient toward all.

Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote. 1 Wathesalonike 5:15

See that no one returns evil for evil to anyone, but always follow after that which is good, for one another, and for all.

Furahini siku zote; 1 Wathesalonike 5:16

Rejoice always.

ombeni bila kukoma; 1 Wathesalonike 5:17

Pray without ceasing.

shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu. 1 Wathesalonike 5:18

In everything give thanks, for this is the will of God in Christ Jesus toward you.

Msimzimishe Roho; 1 Wathesalonike 5:19

Don't quench the Spirit.

msitweze unabii; 1 Wathesalonike 5:20

Don't despise prophesies.

jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema; 1 Wathesalonike 5:21

Test all things, and hold firmly that which is good.

jitengeni na ubaya wa kila namna. 1 Wathesalonike 5:22

Abstain from every form of evil.

Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo. 1 Wathesalonike 5:23

May the God of peace himself sanctify you completely. May your whole spirit, soul, and body be preserved blameless at the coming of our Lord Jesus Christ.

Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya. 1 Wathesalonike 5:24

Faithful is he who calls you, who will also do it.

Ndugu, tuombeeni. 1 Wathesalonike 5:25

Brothers, pray for us.

Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu. 1 Wathesalonike 5:26

Greet all the brothers with a holy kiss.

Nawaapisha kwa Bwana, ndugu wote wasomewe waraka huu. 1 Wathesalonike 5:27

I solemnly charge you by the Lord that this letter be read to all the holy brothers.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. 1 Wathesalonike 5:28

The grace of our Lord Jesus Christ be with you. Amen.