1 Wathesalonike 4 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Wathesalonike 4 (Swahili) 1st Thessalonians 4 (English)

Iliyobaki, ndugu, tunakusihini na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana Yesu; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana. 1 Wathesalonike 4:1

Finally then, brothers, we beg and exhort you in the Lord Jesus, that as you received from us how you ought to walk and to please God, that you abound more and more.

Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu. 1 Wathesalonike 4:2

For you know what charge we gave you through the Lord Jesus.

Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; 1 Wathesalonike 4:3

For this is the will of God: your sanctification, that you abstain from sexual immorality,

kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima; 1 Wathesalonike 4:4

that each one of you know how to possess himself of his own vessel in sanctification and honor,

si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu. 1 Wathesalonike 4:5

not in the passion of lust, even as the Gentiles who don't know God;

Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosa katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana. 1 Wathesalonike 4:6

that no one should take advantage of and wrong a brother or sister in this matter; because the Lord is an avenger in all these things, as also we forewarned you and testified.

Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso. 1 Wathesalonike 4:7

For God called us not for uncleanness, but in sanctification.

Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu. 1 Wathesalonike 4:8

Therefore he who rejects doesn't reject man, but God, who has also given his Holy Spirit to you.

Katika habari ya upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana. 1 Wathesalonike 4:9

But concerning brotherly love, you have no need that one write to you. For you yourselves are taught by God to love one another,

Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini twawasihi, ndugu, mzidi sana. 1 Wathesalonike 4:10

for indeed you do it toward all the brothers who are in all Macedonia. But we exhort you, brothers, that you abound more and more;

Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza; 1 Wathesalonike 4:11

and that you make it your ambition to lead a quiet life, and to do your own business, and to work with your own hands, even as we charged you;

ili mwenende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu cho chote. 1 Wathesalonike 4:12

that you may walk properly toward those who are outside, and may have need of nothing.

Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. 1 Wathesalonike 4:13

But we don't want you to be ignorant, brothers, concerning those who have fallen asleep, so that you don't grieve like the rest, who have no hope.

Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. 1 Wathesalonike 4:14

For if we believe that Jesus died and rose again, even so those who have fallen asleep in Jesus will God bring with him.

Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. 1 Wathesalonike 4:15

For this we tell you by the word of the Lord, that we who are alive, who are left to the coming of the Lord, will in no way precede those who have fallen asleep.

Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. 1 Wathesalonike 4:16

For the Lord himself will descend from heaven with a shout, with the voice of the archangel, and with God's trumpet. The dead in Christ will rise first,

Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. 1 Wathesalonike 4:17

then we who are alive, who are left, will be caught up together with them in the clouds, to meet the Lord in the air. So we will be with the Lord forever.

Basi, farijianeni kwa maneno hayo. 1 Wathesalonike 4:18

Therefore comfort one another with these words.