1 Yohana 3 Swahili & English

Listen/Download Audio
1 Yohana 3 (Swahili) 1st John 3 (English)

Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 1 Yohana 3:1

Behold, how great a love the Father has bestowed on us, that we should be called children of God! For this cause the world doesn't know us, because it didn't know him.

Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 1 Yohana 3:2

Beloved, now we are children of God, and it is not yet revealed what we will be. But we know that, when he is revealed, we will be like him; for we will see him just as he is.

Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu. 1 Yohana 3:3

Everyone who has this hope set on him purifies himself, even as he is pure.

Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi. 1 Yohana 3:4

Everyone who sins also commits lawlessness. Sin is lawlessness.

Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake. 1 Yohana 3:5

You know that he was revealed to take away our sins, and in him is no sin.

Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua. 1 Yohana 3:6

Whoever remains in him doesn't sin. Whoever sins hasn't seen him, neither knows him.

Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki; 1 Yohana 3:7

Little children, let no one lead you astray. He who does righteousness is righteous, even as he is righteous.

atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. 1 Yohana 3:8

He who sins is of the devil, for the devil has been sinning from the beginning. To this end the Son of God was revealed, that he might destroy the works of the devil.

Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu. 1 Yohana 3:9

Whoever is born of God doesn't commit sin, because his seed remains in him; and he can't sin, because he is born of God.

Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake. 1 Yohana 3:10

In this the children of God are revealed, and the children of the devil. Whoever doesn't do righteousness is not of God, neither is he who doesn't love his brother.

Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi; 1 Yohana 3:11

For this is the message which you heard from the beginning, that we should love one another;

si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki. 1 Yohana 3:12

unlike Cain, who was of the evil one, and killed his brother. Why did he kill him? Because his works were evil, and his brother's righteous.

Ndugu zangu, msistaajabu, ulimwengu ukiwachukia. 1 Yohana 3:13

Don't be surprised, my brothers, if the world hates you.

Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana twawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti. 1 Yohana 3:14

We know that we have passed out of death into life, because we love the brothers. He who doesn't love his brother remains in death.

Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake. 1 Yohana 3:15

Whoever hates his brother is a murderer, and you know that no murderer has eternal life remaining in him.

Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu. 1 Yohana 3:16

By this we know love, because he laid down his life for us. And we ought to lay down our lives for the brothers.

Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 1 Yohana 3:17

But whoever has the world's goods, and sees his brother in need, and closes his heart of compassion against him, how does the love of God remain in him?

Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli. 1 Yohana 3:18

My little children, let's not love in word only, neither with the tongue only, but in deed and truth.

Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake, 1 Yohana 3:19

And by this we know that we are of the truth, and persuade our hearts before him,

ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote. 1 Yohana 3:20

because if our heart condemns us, God is greater than our heart, and knows all things.

Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; 1 Yohana 3:21

Beloved, if our hearts don't condemn us, we have boldness toward God;

na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake. 1 Yohana 3:22

and whatever we ask, we receive from him, because we keep his commandments and do the things that are pleasing in his sight.

Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri. 1 Yohana 3:23

This is his commandment, that we should believe in the name of his Son, Jesus Christ, and love one another, even as he commanded.

Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa. 1 Yohana 3:24

He who keeps his commandments remains in him, and he in him. By this we know that he remains in us, by the Spirit which he gave us.