Filemoni 1 Swahili & English
Listen/Download AudioFilemoni 1 (Swahili) | Philemon 1 (English) |
---|---|
Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo aliye ndugu yetu, kwa Filemoni mpendwa wetu, mtenda kazi pamoja nasi, Filemoni 1:1 |
Paul, a prisoner of Christ Jesus, and Timothy our brother, to Philemon, our beloved fellow worker, |
na kwa Afia, ndugu yetu, na kwa Arkipo askari mwenzetu, na kwa kanisa lililo katika nyumba yako. Filemoni 1:2 |
to the beloved Apphia, to Archippus, our fellow soldier, and to the assembly in your house: |
Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu, Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo. Filemoni 1:3 |
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ. |
Namshukuru Mungu wangu sikuzote, nikikukumbuka katika maombi yangu; Filemoni 1:4 |
I thank my God always, making mention of you in my prayers, |
nikisikia habari za upendo wako na imani uliyo nayo kwa Bwana Yesu na kwa watakatifu wote; Filemoni 1:5 |
hearing of your love, and of the faith which you have toward the Lord Jesus, and toward all the saints; |
ili kwamba ushirika wa imani yako ufanye kazi yake, katika ujuzi wa kila kitu chema kilicho kwetu, katika Kristo. Filemoni 1:6 |
that the fellowship of your faith may become effective, in the knowledge of every good thing which is in us in Christ Jesus. |
Maana nalikuwa na furaha nyingi na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa kuwa mioyo ya watakatifu imeburudishwa nawe, ndugu yangu. Filemoni 1:7 |
For we have much joy and comfort in your love, because the hearts of the saints have been refreshed through you, brother. |
Kwa hiyo, nijapokuwa nina ujasiri katika Kristo kukuagiza likupasalo; Filemoni 1:8 |
Therefore, though I have all boldness in Christ to command you that which is appropriate, |
lakini, kwa ajili ya upendo nakusihi, kwa kuwa ni kama nilivyo, Paulo mzee, na sasa mfungwa wa Kristo Yesu pia. Filemoni 1:9 |
yet for love's sake I rather beg, being such a one as Paul, the aged, but also a prisoner of Jesus Christ. |
Nakusihi kwa ajili ya mtoto wangu niliyemzaa katika vifungo vyangu, yaani, Onesimo; Filemoni 1:10 |
I beg you for my child, whom I have become the father of in my chains, Onesimus,{Onesimus means "useful."} |
ambaye zamani alikuwa hakufai, bali sasa akufaa sana, wewe na mimi pia; Filemoni 1:11 |
who once was useless to you, but now is useful to you and to me. |
niliyemtuma kwako, yeye mwenyewe, maana ni moyo wangu hasa; Filemoni 1:12 |
I am sending him back. Therefore receive him, that is, my own heart, |
ambaye mimi nalitaka akae kwangu, apate kunitumikia badala yako katika vifungo vya Injili. Filemoni 1:13 |
whom I desired to keep with me, that on your behalf he might serve me in my chains for the Gospel. |
Lakini sikutaka kutenda neno lo lote isipokuwa kwa shauri lako, ili kwamba wema wako usiwe kama kwa lazima, bali kwa hiari. Filemoni 1:14 |
But I was willing to do nothing without your consent, that your goodness would not be as of necessity, but of free will. |
Maana, labda ndiyo sababu alitengwa nawe kwa muda, ili uwe naye tena milele; Filemoni 1:15 |
For perhaps he was therefore separated from you for a while, that you would have him forever, |
tokea sasa, si kama mtumwa, bali zaidi ya mtumwa, ndugu mpendwa; kwangu mimi sana, na kwako wewe zaidi sana, katika mwili na katika Bwana. Filemoni 1:16 |
no longer as a slave, but more than a slave, a beloved brother, especially to me, but how much rather to you, both in the flesh and in the Lord. |
Basi kama ukiniona mimi kuwa mshirika nawe, mpokee huyu kama mimi mwenyewe. Filemoni 1:17 |
If then you count me a partner, receive him as you would receive me. |
Na kama amekudhulumu, au unamwia kitu, ukiandike hicho juu yangu. Filemoni 1:18 |
But if he has wronged you at all, or owes you anything, put that to my account. |
Mimi Paulo nimeandika kwa mkono wangu mwenyewe, mimi nitalipa. Sikuambii kwamba nakuwia hata nafsi yako. Filemoni 1:19 |
I, Paul, write this with my own hand: I will repay it (not to mention to you that you owe to me even your own self besides). |
Naam, ndugu yangu, nipate faida kwako katika Bwana; uniburudishe moyo wangu katika Kristo. Filemoni 1:20 |
Yes, brother, let me have joy from you in the Lord. Refresh my heart in the Lord. |
Kwa kuwa nakuamini kutii kwako ndiyo maana nimekuandikia, nikijua ya kuwa utafanya zaidi ya hayo nisemayo. Filemoni 1:21 |
Having confidence in your obedience, I write to you, knowing that you will do even beyond what I say. |
Na pamoja na hayo uniwekee tayari mahali pa kukaa; maana nataraji ya kwamba kwa maombi yenu mtajaliwa kunipata. Filemoni 1:22 |
Also, prepare a guest room for me, for I hope that through your prayers I will be restored to you. |
Epafra, aliyefungwa pamoja nami katika Kristo Yesu, akusalimu; Filemoni 1:23 |
Epaphras, my fellow prisoner in Christ Jesus, greets you, |
na Marko, na Aristarko, na Dema, na Luka, watendao kazi pamoja nami. Filemoni 1:24 |
as do Mark, Aristarchus, Demas, and Luke, my fellow workers. |
Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Filemoni 1:25 |
The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit. Amen. |