1
Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.
It is for freedom that Christ has set us free. Stand firm, then, and do not be encumbered once more by a yoke of slavery.
2
Tazama, mimi Paulo nawaambia ninyi ya kwamba, mkitahiriwa, Kristo hatawafaidia neno.
Take notice: I, Paul, tell you that if you let yourselves be circumcised, Christ will be of no value to you at all.
3
Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote.
Again I testify to every man who gets himself circumcised that he is obligated to obey the whole law.
4
Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.
You who are trying to be justified by the law have been severed from Christ; you have fallen away from grace.
5
Maana sisi kwa Roho tunalitazamia tumaini la haki kwa njia ya imani.
But by faith we eagerly await through the Spirit the hope of righteousness.
6
Maana katika Kristo Yesu kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa, bali imani itendayo kazi kwa upendo.
For in Christ Jesus neither circumcision nor uncircumcision has any value. What matters is faith expressing itself through love.
7
Mlikuwa mkipiga mbio vizuri; ni nani aliyewazuia msiitii kweli?
You were running so well. Who has obstructed you from obeying the truth?
8
Kushawishi huku hakukutoka kwake yeye anayewaita ninyi.
Such persuasion does not come from the One who calls you.
9
Chachu kidogo huchachua donge zima.
A little leaven works through the whole batch of dough.
10
Nina matumaini kwenu katika Bwana, ya kwamba hamtakuwa na nia ya namna nyingine. Lakini yeye anayewafadhaisha atachukua hukumu yake, awaye yote.
I am confident in the Lord that you will take no other view. The one who is troubling you will bear the judgment, whoever he may be.
11
Nami, ndugu zangu ikiwa ninahubiri habari ya kutahiriwa, kwa nini ningali ninaudhiwa? Hapo kwazo la msalaba limebatilika!
Now, brothers, if I am still preaching circumcision, why am I still being persecuted? In that case the offense of the cross has been abolished.
12
Laiti hao wanaowatia mashaka wangejikata nafsi zao!
As for those who are agitating you, I wish they would proceed to emasculate themselves!
13
Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo.
For you, brothers, were called to freedom; but do not use your freedom as an opportunity for the flesh. Rather, serve one another in love.
14
Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
The entire law is fulfilled in a single decree: “Love your neighbor as yourself.”
15
Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.
But if you keep on biting and devouring one another, watch out, or you will be consumed by one another.
16
Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
So I say, walk by the Spirit, and you will not gratify the desires of the flesh.
17
Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
For the flesh craves what is contrary to the Spirit, and the Spirit what is contrary to the flesh. They are opposed to each other, so that you do not do what you want.
18
Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
But if you are led by the Spirit, you are not under the law.
19
Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
The acts of the flesh are obvious: sexual immorality, impurity, and debauchery;
20
ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
idolatry and sorcery; hatred, discord, jealousy, and rage; rivalries, divisions, factions,
21
husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
and envy; drunkenness, orgies, and the like. I warn you, as I did before, that those who practice such things will not inherit the kingdom of God.
22
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
But the fruit of the Spirit is love, joy, peace, patience, kindness, goodness, faithfulness,
23
upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
gentleness, and self-control. Against such things there is no law.
24
Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.
Those who belong to Christ Jesus have crucified the flesh with its passions and desires.
25
Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.
Since we live by the Spirit, let us walk in step with the Spirit.
26
Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
Let us not become conceited, provoking and envying one another.