2 Yohana 1 Swahili & English

Listen/Download Audio
2 Yohana 1 (Swahili) 2nd John 1 (English)

Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuao ile kweli; 2 Yohana 1:1

The elder, to the chosen lady and her children, whom I love in truth; and not I only, but also all those who know the truth;

kwa ajili ya hiyo kweli ikaayo ndani yetu, nayo itakuwa pamoja nasi hata milele. 2 Yohana 1:2

for the truth's sake, which remains in us, and it will be with us forever:

Neema, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo. 2 Yohana 1:3

Grace, mercy, and peace will be with us, from God the Father, and from the Lord Jesus Christ, the Son of the Father, in truth and love.

Nalifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba. 2 Yohana 1:4

I rejoice greatly that I have found some of your children walking in truth, even as we have been commanded by the Father.

Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane. 2 Yohana 1:5

Now I beg you, dear lady, not as though I wrote to you a new commandment, but that which we had from the beginning, that we love one another.

Na huu ndio upendo: tuenende kwa kuzifuata amri zake. Hii ndiyo ile amri, kama mlivyosikia tangu mwanzo kwamba mwenende katika hiyo. 2 Yohana 1:6

This is love, that we should walk according to his commandments. This is the commandment, even as you heard from the beginning, that you should walk in it.

Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea duniani, wasiokiri ya kuwa Yesu Kristo yuaja katika mwili. Huyo ndiye yule mdanganyifu na mpinga Kristo. 2 Yohana 1:7

For many deceivers have gone out into the world, those who don't confess that Jesus Christ came in the flesh. This is the deceiver and the Antichrist.

Jiangalieni nafsi zenu msiyapoteze mliyoyatenda, bali mpokee thawabu timilifu. 2 Yohana 1:8

Watch yourselves, that we don't lose the things which we have accomplished, but that we receive a full reward.

Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia. 2 Yohana 1:9

Whoever transgresses and doesn't remain in the teaching of Christ, doesn't have God. He who remains in the teaching, the same has both the Father and the Son.

Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu. 2 Yohana 1:10

If anyone comes to you, and doesn't bring this teaching, don't receive him into your house, and don't welcome him,

Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu. 2 Yohana 1:11

for he who welcomes him participates in his evil works.

Kwa kuwa ninayo mambo mengi, sitaki kuyaandika kwa karatasi na wino; lakini nataraji kuja kwenu, na kusema nanyi uso kwa uso, ili furaha yetu iwe imetimizwa. 2 Yohana 1:12

Having many things to write to you, I don't want to do so with paper and ink, but I hope to come to you, and to speak face to face, that our joy may be made full.

Watoto wa ndugu yako aliye mteule, wakusalimu. 2 Yohana 1:13

The children of your chosen sister greet you. Amen.