1
Hawa ndio wana wa Israeli; Reubeni, na Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Zabuloni;
These were the sons of Israel: Reuben, Simeon, Levi, Judah, Issachar, Zebulun,
2
na Dani, na Yusufu, na Benyamini, na Naftali, na Gadi, na Asheri.
Dan, Joseph, Benjamin, Naphtali, Gad, and Asher.
3
Wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela; ambao hao watatu alizaliwa na binti Shua, Mkanaani. Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa Bwana; naye akamwua.
The sons of Judah: Er, Onan, and Shelah. These three were born to him by Bath-shua the Canaanite. Er, Judah’s firstborn, was wicked in the sight of the LORD. So the LORD put him to death.
4
Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano.
Tamar, Judah’s daughter-in-law, bore to him Perez and Zerah. Judah had five sons in all.
5
Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli.
The sons of Perez: Hezron and Hamul.
6
Na wana wa Zera; Zabdi, na Ethani, na Hemani, na Kalkoli, na Darda; hao wote ni watano.
The sons of Zerah: Zimri, Ethan, Heman, Calcol, and Dara—five in all.
7
Na wana wa Karmi; Akani, yule mwenye kutaabisha Israeli, aliyekosa katika kitu kilichowekwa wakfu.
The son of Carmi: Achar, who brought trouble upon Israel by violating the ban on devoted things.
8
Na wana wa Ethani; Azaria.
The son of Ethan: Azariah.
9
Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu.
The sons who were born to Hezron: Jerahmeel, Ram, and Caleb.
10
Na Ramu akamzaa Aminadabu; na Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa wana wa Yuda;
Ram was the father of Amminadab, and Amminadab was the father of Nahshon, a leader of the descendants of Judah.
11
na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi;
Nahshon was the father of Salmon, and Salmon was the father of Boaz.
12
na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;
Boaz was the father of Obed, and Obed was the father of Jesse.
13
na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;
Jesse was the father of Eliab his firstborn; Abinadab was born second, Shimea third,
14
na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;
Nethanel fourth, Raddai fifth,
15
na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;
Ozem sixth, and David seventh.
16
na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.
Their sisters were Zeruiah and Abigail. And the three sons of Zeruiah were Abishai, Joab, and Asahel.
17
Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.
Abigail was the mother of Amasa, whose father was Jether the Ishmaelite.
18
Basi Kalebu, mwana wa Hesroni, akazaliwa wana na mkewe Azubu, na Yeriothi, na hawa ndio wanawe wa kiume; Yesheri, na Shobabu, na Ardoni.
Caleb son of Hezron had children by his wife Azubah and by Jerioth. These were the sons of Azubah: Jesher, Shobab, and Ardon.
19
Akafa Azuba, naye Kalebu akamtwaa Efrathi, aliyemzalia Huri.
When Azubah died, Caleb married Ephrath, who bore to him Hur.
20
Naye Huri akamzaa Uri; na Uri akamzaa Besaleli.
Hur was the father of Uri, and Uri was the father of Bezalel.
21
Na baadaye Hesroni akamwingilia binti wa Makiri, babaye Gileadi; ambaye alimtwaa alipokuwa mwenye miaka sitini; naye akamzalia Segubu.
Later, Hezron slept with the daughter of Machir the father of Gilead. He had married her when he was sixty years old, and she bore to him Segub.
22
Na Segubu akamzaa Yairi, aliyekuwa mwenye miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Segub was the father of Jair, who had twenty-three cities in the land of Gilead.
23
Na Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi, pamoja na Kenathi na miji yake, jumla yote miji sitini. Hao wote ni wana wa Makiri, babaye Gileadi.
But Geshur and Aram captured Havvoth-jair, along with Kenath and its sixty surrounding villages. All these were descendants of Machir the father of Gilead.
24
Tena, baada ya kufa kwake Hesroni huko Kalebu-Efrata, ndipo Abia, mkewe Hesroni, alipomzalia Ashuri, babaye Teboa.
After Hezron died in Caleb-ephrathah, his wife Abijah bore to him Ashhur the father of Tekoa.
25
Na wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa Ramu, mzaliwa wa kwanza, na Buna, na Oreni, na Ozemu; kwa Ahiya.
The sons of Jerahmeel the firstborn of Hezron: Ram his firstborn, Bunah, Oren, Ozem, and Ahijah.
26
Naye Yerameeli alikuwa na mke mwingine, jina lake Atara; yeye alikuwa mamaye Onamu.
Jerahmeel had another wife named Atarah, who was the mother of Onam.
27
Na wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, na Yamini, na Ekeri.
The sons of Ram the firstborn of Jerahmeel: Maaz, Jamin, and Eker.
28
Na wana wa Onamu walikuwa Shamai, na Yada; na wana wa Shamai; Nadabu, na Abishuri.
The sons of Onam: Shammai and Jada. The sons of Shammai: Nadab and Abishur.
29
Na mkewe Abishuri aliitwa jina lake Abihaili; naye akamzalia Abani, na Molidi.
Abishur’s wife was named Abihail, and she bore to him Ahban and Molid.
30
Na wana wa Nadabu; Seledi, na Apaimu; walakini Seledi alikufa hana watoto.
The sons of Nadab: Seled and Appaim. Seled died without children.
31
Na wana wa Apaimu; Ishi. Na wana wa Ishi; Sheshani. Na wana wa Sheshani; Alai.
The son of Appaim: Ishi. The son of Ishi: Sheshan. The son of Sheshan: Ahlai.
32
Na wana wa Yada, nduguye Shamai; Yetheri, na Yonathani; naye Yetheri akafa hana watoto.
The sons of Jada the brother of Shammai: Jether and Jonathan. Jether died without children.
33
Na wana wa Yonathani; Pelethi, na Zaza. Hao ndio wana wa Yerameeli.
The sons of Jonathan: Peleth and Zaza. These were the descendants of Jerahmeel.
34
Basi huyo Sheshani alikuwa hana wana wa kiume, ila binti. Naye Sheshani alikuwa na mtumwa, Mmisri, jina lake akiitwa Yarha.
Sheshan had no sons, but only daughters. He also had an Egyptian servant named Jarha.
35
Basi akamwoza binti yake aolewe na Yarha, mtumwa wake; naye akamzalia Atai.
Sheshan gave his daughter in marriage to his servant Jarha, and she bore to him Attai.
36
Na Atai akamzaa Nathani; na Nathani akamzaa Zabadi;
Attai was the father of Nathan, Nathan was the father of Zabad,
37
na Zabadi akamzaa Eflali; na Eflali akamzaa Obedi;
Zabad was the father of Ephlal, Ephlal was the father of Obed,
38
na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria;
Obed was the father of Jehu, Jehu was the father of Azariah,
39
na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa
Azariah was the father of Helez, Helez was the father of Elasah,
40
na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;
Elasah was the father of Sismai, Sismai was the father of Shallum,
41
na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.
Shallum was the father of Jekamiah, and Jekamiah was the father of Elishama.
42
Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.
The sons of Caleb the brother of Jerahmeel: Mesha his firstborn, who was the father of Ziph, and Mareshah his second son, who was the father of Hebron.
43
Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.
The sons of Hebron: Korah, Tappuah, Rekem, and Shema.
44
Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai.
Shema was the father of Raham the father of Jorkeam, and Rekem was the father of Shammai.
45
Na mwana wake Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa babaye Bethsuri.
The son of Shammai was Maon, and Maon was the father of Beth-zur.
46
Naye Efa, suria yake Kalebu, alimzaa Harani, na Mosa, na Gazezi; naye Harani akamzaa Gazezi.
Caleb’s concubine Ephah was the mother of Haran, Moza, and Gazez. Haran was the father of Gazez.
47
Na wana wa Yadai; Regemu, na Yothamu, na Geshani, na Peleti, na Efa, na Shaafu.
The sons of Jahdai: Regem, Jotham, Geshan, Pelet, Ephah, and Shaaph.
48
Naye Maaka, suria yake Kalebu, akamzalia Sheberi, na Tirhana.
Caleb’s concubine Maacah was the mother of Sheber and Tirhanah.
49
Tena akamzaa Shaafu, babaye Madmana; na Sheva babaye Makbena; na babaye Gibea; naye binti Kalebu alikuwa Aksa.
She was also the mother of Shaaph father of Madmannah, and of Sheva father of Machbenah and Gibea. Caleb’s daughter was Acsah.
50
Hao walikuwa wana wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi; Shobali, babaye Kiriath-Yearimu;
These were the descendants of Caleb. The sons of Hur the firstborn of Ephrathah: Shobal the father of Kiriath-jearim,
51
Salma, babaye Bethlehemu; na Harefu, babaye Beth-gaderi.
Salma the father of Bethlehem, and Hareph the father of Beth-gader.
52
Naye Shobali, babaye Kiriath-Yearimu, alikuwa na wana; Haroe, na nusu ya Wamenuhothi.
These were the descendants of Shobal the father of Kiriath-jearim: Haroeh, half the Manahathites,
53
Na jamaa za Kiriath-Yearimu; Waithri, na Waputhi, na Washumathi, na Wamishrai; katika hao walitoka Wasorathi, na Waeshtaoli.
and the clans of Kiriath-jearim—the Ithrites, Puthites, Shumathites, and Mishraites. From these descended the Zorathites and Eshtaolites.
54
Na wana wa Salma; Bethlehemu, na Wanetofathi, Atroth-beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi, na Wazori.
The descendants of Salma: Bethlehem, the Netophathites, Atroth-beth-joab, half the Manahathites, the Zorites,
55
Na jamaa za waandishi waliokaa Yabesi; Watirathi, na Washimeathi, na Wasukathi. Hao ndio Wakeni, waliotoka kwake Hamathi, babaye mbari ya Rekabu.
and the clans of the scribes who lived at Jabez—the Tirathites, Shimeathites, and Sucathites. These are the Kenites who came from Hammath, the father of the house of Rechab.