Wagalatia BSB

Wagalatia 6

Galatians Chapter 6

1
Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
Brothers, if someone is caught in a trespass, you who are spiritual should restore him with a spirit of gentleness. But watch yourself, or you also may be tempted.
2
Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.
Carry one another’s burdens, and in this way you will fulfill the law of Christ.
3
Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.
If anyone thinks he is something when he is nothing, he deceives himself.
4
Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake.
Each one should test his own work. Then he will have reason to boast in himself alone, and not in someone else.
5
Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.
For each one should carry his own load.
6
Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote.
Nevertheless, the one who receives instruction in the word must share in all good things with his instructor.
7
Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.
Do not be deceived: God is not to be mocked. Whatever a man sows, he will reap in return.
8
Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.
The one who sows to please his flesh, from the flesh will reap destruction; but the one who sows to please the Spirit, from the Spirit will reap eternal life.
9
Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.
Let us not grow weary in well-doing, for in due time we will reap a harvest if we do not give up.
10
Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.
Therefore, as we have opportunity, let us do good to everyone, and especially to the family of faith.
11
Tazameni ni kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe!
See what large letters I am using to write to you with my own hand!
12
Wote watakao kuonekana ni wazuri kwa mambo ya mwili, ndio wanaowashurutisha kutahiriwa; makusudi wasiudhiwe kwa ajili ya msalaba wa Kristo, hilo tu.
Those who want to make a good impression outwardly are trying to compel you to be circumcised. They only do this to avoid persecution for the cross of Christ.
13
Kwa maana hata wao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; bali wanataka ninyi mtahiriwe, wapate kuona fahari katika miili yenu.
For the circumcised do not even keep the law themselves, yet they want you to be circumcised that they may boast in your flesh.
14
Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu.
But as for me, may I never boast, except in the cross of our Lord Jesus Christ, through which the world has been crucified to me, and I to the world.
15
Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya.
For neither circumcision nor uncircumcision means anything. What counts is a new creation.
16
Na wote watakaoenenda kwa kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu.
Peace and mercy to all who walk by this rule, even to the Israel of God.
17
Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.
From now on let no one cause me trouble, for I bear on my body the marks of Jesus.
18
Ndugu zangu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu. Amina.
The grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit, brothers. Amen.

Chagua Sura

1 2 3 4 5 6